MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Habari ndugu
Mimi huwa si mpenzi wa Udakus but kichwa cha habari kilinishawishi ...................... Hivi ni wapi tunapoelekea watanzania wenzangu?
Siyo siri tena, akiangua kilio nyumbani kwa mama yake mkubwa katika Mtaa wa Miningani Kondoa mkoani hapa, mbele ya Mwandishi wa Uwazi, Binti huyo alieleza kuwa, Baba yake mzazi ambaye ni Mpiga debe katika Stendi ya Mabasi yaendayo mikoani Mjini Dodoma, amekuwa akimlazimisha kuwa katika uhusiano wa kimapenzi kwa muda mrefu toka mama yake afariki hadi pale alipomkubalia na kujikuta akiambulia mimba ambayo hata hivyo mtoto alifariki mara baada ya mimba kuharibika.
Akieleza mkasa mzima ulivyoanza, Msichana huyo alisema, alilazimika kusoma huko Kondoa, japo yeye ni Mzaliwa wa Chamwino Manispaa ya Dodoma, baada ya wazazi wake kutengana na baadaye kwa bahati mbaya mama yake alifariki dunia kwa kile alichodai kuwa ni Ugonjwa wa UKIMWI, hivyo kujikuta akipata malezi ya baba peke yake.
Huku akimwaga machozi, Binti huyo alisema baada ya kumaliza Elimu ya Msingi, mwaka 2008 alichaguliwa kujiunga na Shule moja ya Wasichana iliyoko Iringa, ndipo Baba yake Mzazi alipomuahidi kumsomesha ambapo alimpatia mahitaji yote ya shule na kufanikiwa kuanza Kidato cha Kwanza mwaka huo.
Alisema wakati wa likizo, Baba yake alikuwa akimlipia nauli ya kwenda Iringa na kurudi Dodoma na hata likizo ilipomalizika, alifanya vivyo hivyo, lakini mwishoni mwa mwaka huo mwezi wa kumi na moja, alipata taarifa kutoka kwa baba huyo kuwa Mama yake alikuwa amefariki dunia huko nyumbani kwao Kondoa na aliweza kufika na kumzika Mama yake.
Kwa masikitiko alisema, baada ya kufunga shule mwezi wa kumi na mbili alirejea Chamwino, Dodoma kwa Baba yake Mzazi na akawa akilala chumba na kitanda kimoja na mzazi wake huyo kwa kisingizio kuwa, hakuwa na namna nyingine kwani aliishi kwa ukata.
Akasema. Ilikuwa Desemba 12, mwaka jana, Baba yake alirudi usiku wa saa nne na kumlazimisha kufanya ngono na alipojaribu kumkatalia, mzazi wake huyo alimwambia endapo angekataa, angemuua, jambo lililomfanya aingiwe na hofu hivyo kubaki na mshangao mkubwa akiwa haamini kile alichokuwa akifafanyiwa na mzazi wake huyo.
Maskini wa Mungu, Binti huyo anasema alikuwa katika siku za hatari (siku zake) kushika mimba, kwa hiyo baba yake alipogusa tu (kufanya naye mapenzi) akajua tayari amenasa mimba.
Msichana huyo alisema baada ya kitendo hicho, alikwenda Kondoa kumalizia msiba wa mama yake na aliogopa kurejea kwa baba yake na kulazimika kurudi tena shuleni lakini baada ya kufika huko shuleni huwa kuna kawaida ya wanafunzi kufanyiwa vipimo kujua kama wapo wenye ujauzito lakini cha ajabu vipimo havikuonesha kama alikuwa na ujauzito.
MIEZI MIWILI BAADAYE Binti huyo alianza kujisikia vibaya lakini aliogopa kuwaambia walimu na kubaki na hali hiyo mpaka aliporudi nyumbani mwaka huu likizo ya mwezi wa sita na kwenda kwa mama yake mkubwa aishie Area A, mjini hapa na kumwelezea mwanzo hadi mwisho wa mkasa huo, ndipo alipompeleka katika Hospitali ya Matovolwa na kugundulika kuwa alikuwa na ujauzito wa miezi sita. Akasema, alijaribu kumueleza baba yake lakini mzazi huyo alimtisha kwa kumwambia asimtaje yeye bali amsingizie mtu mwingine, jambo ambalo alimkatalia na kumwambia kuwa amemweleza mama yake mkubwa.
WIKI MBILI BAADAYE Alisema, alipigiwa simu na mama yake mkubwa wa Kondoa akijulishwa kuwa taarifa za kulala na baba yake Mzazi kwa wanafamilia wote na zaidi akilaumiwa kuwa mama yake alikufa kwa UKIMWI ambao aliukwaa kutoka kwa baba huyo. Akasema, hali hiyo imekuwa ikimsumbua kwakuwa hata yeye anajua jinsi mama yake mzazi alivyofariki kwa mateso makuu.
SIKU ZA HIVI KARIBUNI Msichana huyo anasema kwa sasa anasumbuliwa na kupanda kwa presha iliyopelekea yeye kulazwa siku sita katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwasababu ya mawazo, hali iliyosababisha mimba yake ya mtoto wa kiume kuchoropoka.
Binti huyo alisema baada ya kuruhusiwa alirudi kwa mama yake mkubwa wa Area A Dodoma lakini alianza kusumbuliwa na miguu kuwaka moto hadi kufikia hatua ya kuiloweka kwenye maji ya baridi na kushindwa kutembea.
Baada ya Mama yake Mkubwa kuona hali hiyo, ilimbidi amuarifu dada yake aliyeko Kondoa na kumpeleka huko na ndipo alipo sasa akiendelea na matibabu hivyo kushindwa kurejea shuleni kuendelea na masomo.
Kwa mujibu wa mama yake mkubwa wa Kondoa, alimchukua binti huyo baada ya kusikia matatizo yaliyompata na kusema kuwa, wakati wa uhai wa marehemu mama yake walihangaika kimatibabu mpaka walipompeleka Hospitali ya Wilaya ya Kondoa na kugundulika kuwa aliambukizwa Virusi Vya UKIMWI na kwa kuwa walimchelewesha, walishindwa kupata matibabu sahihi hivyo kupoteza uhai. Anasema, alimwita binti huyo na kumweleza kuwa, kwakuwa alifanya ngono na baba yake, ni vizuri wakahakikishe juu ya Afya yake.
Tarehe 14, mwezi huu, wawili hao walikwenda katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa na kuchukua vipimo vya HIV na kutakiwa kurudi tena kupima mwezi ujao ili kuhakikisha mara ya pili.
Source: http://www.globalpublisherstz.com/2009/08/25/baba_kanibaka_kanipa_mimba_na_ukimwi.html
Mimi huwa si mpenzi wa Udakus but kichwa cha habari kilinishawishi ...................... Hivi ni wapi tunapoelekea watanzania wenzangu?
Siyo siri tena, akiangua kilio nyumbani kwa mama yake mkubwa katika Mtaa wa Miningani Kondoa mkoani hapa, mbele ya Mwandishi wa Uwazi, Binti huyo alieleza kuwa, Baba yake mzazi ambaye ni Mpiga debe katika Stendi ya Mabasi yaendayo mikoani Mjini Dodoma, amekuwa akimlazimisha kuwa katika uhusiano wa kimapenzi kwa muda mrefu toka mama yake afariki hadi pale alipomkubalia na kujikuta akiambulia mimba ambayo hata hivyo mtoto alifariki mara baada ya mimba kuharibika.
Akieleza mkasa mzima ulivyoanza, Msichana huyo alisema, alilazimika kusoma huko Kondoa, japo yeye ni Mzaliwa wa Chamwino Manispaa ya Dodoma, baada ya wazazi wake kutengana na baadaye kwa bahati mbaya mama yake alifariki dunia kwa kile alichodai kuwa ni Ugonjwa wa UKIMWI, hivyo kujikuta akipata malezi ya baba peke yake.
Huku akimwaga machozi, Binti huyo alisema baada ya kumaliza Elimu ya Msingi, mwaka 2008 alichaguliwa kujiunga na Shule moja ya Wasichana iliyoko Iringa, ndipo Baba yake Mzazi alipomuahidi kumsomesha ambapo alimpatia mahitaji yote ya shule na kufanikiwa kuanza Kidato cha Kwanza mwaka huo.
Alisema wakati wa likizo, Baba yake alikuwa akimlipia nauli ya kwenda Iringa na kurudi Dodoma na hata likizo ilipomalizika, alifanya vivyo hivyo, lakini mwishoni mwa mwaka huo mwezi wa kumi na moja, alipata taarifa kutoka kwa baba huyo kuwa Mama yake alikuwa amefariki dunia huko nyumbani kwao Kondoa na aliweza kufika na kumzika Mama yake.
Kwa masikitiko alisema, baada ya kufunga shule mwezi wa kumi na mbili alirejea Chamwino, Dodoma kwa Baba yake Mzazi na akawa akilala chumba na kitanda kimoja na mzazi wake huyo kwa kisingizio kuwa, hakuwa na namna nyingine kwani aliishi kwa ukata.
Akasema. Ilikuwa Desemba 12, mwaka jana, Baba yake alirudi usiku wa saa nne na kumlazimisha kufanya ngono na alipojaribu kumkatalia, mzazi wake huyo alimwambia endapo angekataa, angemuua, jambo lililomfanya aingiwe na hofu hivyo kubaki na mshangao mkubwa akiwa haamini kile alichokuwa akifafanyiwa na mzazi wake huyo.
Maskini wa Mungu, Binti huyo anasema alikuwa katika siku za hatari (siku zake) kushika mimba, kwa hiyo baba yake alipogusa tu (kufanya naye mapenzi) akajua tayari amenasa mimba.
Msichana huyo alisema baada ya kitendo hicho, alikwenda Kondoa kumalizia msiba wa mama yake na aliogopa kurejea kwa baba yake na kulazimika kurudi tena shuleni lakini baada ya kufika huko shuleni huwa kuna kawaida ya wanafunzi kufanyiwa vipimo kujua kama wapo wenye ujauzito lakini cha ajabu vipimo havikuonesha kama alikuwa na ujauzito.
MIEZI MIWILI BAADAYE Binti huyo alianza kujisikia vibaya lakini aliogopa kuwaambia walimu na kubaki na hali hiyo mpaka aliporudi nyumbani mwaka huu likizo ya mwezi wa sita na kwenda kwa mama yake mkubwa aishie Area A, mjini hapa na kumwelezea mwanzo hadi mwisho wa mkasa huo, ndipo alipompeleka katika Hospitali ya Matovolwa na kugundulika kuwa alikuwa na ujauzito wa miezi sita. Akasema, alijaribu kumueleza baba yake lakini mzazi huyo alimtisha kwa kumwambia asimtaje yeye bali amsingizie mtu mwingine, jambo ambalo alimkatalia na kumwambia kuwa amemweleza mama yake mkubwa.
WIKI MBILI BAADAYE Alisema, alipigiwa simu na mama yake mkubwa wa Kondoa akijulishwa kuwa taarifa za kulala na baba yake Mzazi kwa wanafamilia wote na zaidi akilaumiwa kuwa mama yake alikufa kwa UKIMWI ambao aliukwaa kutoka kwa baba huyo. Akasema, hali hiyo imekuwa ikimsumbua kwakuwa hata yeye anajua jinsi mama yake mzazi alivyofariki kwa mateso makuu.
SIKU ZA HIVI KARIBUNI Msichana huyo anasema kwa sasa anasumbuliwa na kupanda kwa presha iliyopelekea yeye kulazwa siku sita katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwasababu ya mawazo, hali iliyosababisha mimba yake ya mtoto wa kiume kuchoropoka.
Binti huyo alisema baada ya kuruhusiwa alirudi kwa mama yake mkubwa wa Area A Dodoma lakini alianza kusumbuliwa na miguu kuwaka moto hadi kufikia hatua ya kuiloweka kwenye maji ya baridi na kushindwa kutembea.
Baada ya Mama yake Mkubwa kuona hali hiyo, ilimbidi amuarifu dada yake aliyeko Kondoa na kumpeleka huko na ndipo alipo sasa akiendelea na matibabu hivyo kushindwa kurejea shuleni kuendelea na masomo.
Kwa mujibu wa mama yake mkubwa wa Kondoa, alimchukua binti huyo baada ya kusikia matatizo yaliyompata na kusema kuwa, wakati wa uhai wa marehemu mama yake walihangaika kimatibabu mpaka walipompeleka Hospitali ya Wilaya ya Kondoa na kugundulika kuwa aliambukizwa Virusi Vya UKIMWI na kwa kuwa walimchelewesha, walishindwa kupata matibabu sahihi hivyo kupoteza uhai. Anasema, alimwita binti huyo na kumweleza kuwa, kwakuwa alifanya ngono na baba yake, ni vizuri wakahakikishe juu ya Afya yake.
Tarehe 14, mwezi huu, wawili hao walikwenda katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa na kuchukua vipimo vya HIV na kutakiwa kurudi tena kupima mwezi ujao ili kuhakikisha mara ya pili.
Source: http://www.globalpublisherstz.com/2009/08/25/baba_kanibaka_kanipa_mimba_na_ukimwi.html