Baba Askofu anapowashughulikia wajane..........

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,424
911,172
Ama kwa hakika kweli kufa ni kufaana kikabisa-kabisa
Yawaje haya yawasibu wajane ambao kilio chao ni kanisa lao?
Nilifikiri wajane ni wa kuwaangalia kwa jicho la huruma.,.
Kumbe huyu Baba Askofu kaona ni kivuno...
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane.........

Kiama kimetufika na wanaumme tunateketea.......
Kiama cha wanaumme sasa harusi ya Baba Askofu..........
Kiama cha wanaumme chadhoofisha familia......
Kiama cha wanaumme chazalisha wajane........
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane............

Waumme wanapotoweka si kilio tu huacha bali familia huyumba.......
Yule "bread winner" akiwa kapuni mjane humlazimu kurithi mikoba yake.....
Lishe, pango, matibabu, karo na usafiri ni baadhi ya kero zake.....
Sasa kero za mjane Baba Askofu kwake ni kitoweo.........
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane.............

Pesa za wafadhili za kuhudumia wajane sasa hutolewa kwa masharti.....
Masharti ya Baba Askofu ni moto na mchezo hataki............
Bila ya wajane kumtuliza kiu yake, patupu huambulia mgao wao.......
Kwa kubanwa kila upande wajane waona bora wamtumikie kafiri wapate mradi wao.....
Wajamani Baba Askofu acha kuwashughulikia wajane.........
 
Mkuu kuna wajane ambao wao wanalilia kupoteza mume............

Mali na mfumo wa maisha tayari walishajiwekea thabiti na askofu wala mafimaji hawana nafasi mpaka apende yeye.

Wajane unaowasema ni wale wa zamani ambapo mwanamke alikuwa kama mama wa nyumbani lakini siku hizi kidogo hali imebadilika.

Na huyo askofu ni fagia fagia hachagui? Maana kila mtu anavigezo vyake vya kula nyama ile, ni sharti uchague iliyonona. Kama unataka kusema wajane wote wamenona sawa askofu atafanya kazi yake.

Siku hizi kajamaa kale nako kitisho, maana penzi ili linoge na uonje utamu wa sukari ni sharti upekue kavukavu!!!!!

Na ikiwa hivyo askofu naye siyo mzima anataka kuleta msiba mzito zaidi kwa familia kwa kufanya hata mama aliyebaki kupotea kabisa na kuacha mayatima!!!!!!
 
Mkuu kuna wajane ambao wao wanalilia kupoteza mume............

Mali na mfumo wa maisha tayari walishajiwekea thabiti na askofu wala mafimaji hawana nafasi mpaka apende yeye.

Wajane unaowasema ni wale wa zamani ambapo mwanamke alikuwa kama mama wa nyumbani lakini siku hizi kidogo hali imebadilika.

Na huyo askofu ni fagia fagia hachagui? Maana kila mtu anavigezo vyake vya kula nyama ile, ni sharti uchague iliyonona. Kama unataka kusema wajane wote wamenona sawa askofu atafanya kazi yake.

Siku hizi kajaa kale nako kitisho, maana penzi ili linoge na uonje utamu wa sukari ni sharti upekue kavukavu!!!!!

Na ikiwa hivyo askofu naye siyo mzima anataka kuleta msiba mzito zaidi kwa familia kwa kufanya hata mama aliyebaki kupotea kabisa na kuacha mayatima!!!!!!

losambo ukweli lazima tuuseme nao ni kuwa wengi ya wajane ni hoehae.............na waumme zao wameishia bila kuwaachia msingi wa kujivaragua hata chembe matokeo yake hawawezi kufurukuta kwa Baba Askofu........Baba Askofu ni wote wale ambao wanashughulikia wajane kwa kukidhi mahitaji ya kuishi.....ushahidi angalia NGO nyingi zimeanzishwa za kuwahudumia wajane................kumbe ni akina Baba Askofu ambao ndiyo huona ganda la mwua la jana chungu kuona ni kivuno kwao..... Losambo
 
Last edited by a moderator:
mi naona si kwa wajane tu hata wale ambao hawajaolewa Baba askofu anashugulika nao

Vaislay umeamkaje? Umeng'atwa usiku wa leo au umelala fofo tu...............wajane kabali yao ni kali kwa sababu tofauti na hao wasichana ni kuwa wajane wengi saa zimesogea na hawapo sana sokoni kwa hiyo wana aina fulani ya kujikuta lupango na wanapopewa masharti hujikuta hawana namna bali kujisalimisha kwa Baba Askofu....[MENTION]@Vaislay[/MENTION]
 
Vaislay umeamkaje? Umeng'atwa usiku wa leo au umelala fofo tu...............wajane kabali yao ni kali kwa sababu tofauti na hao wasichana ni kuwa wajane wengi saa zimesogea na hawapo sana sokoni kwa hiyo wana aina fulani ya kujikuta lupango na wanapopewa masharti hujikuta hawana namna bali kujisalimisha kwa Baba Askofu... Vaislay
fofooffoooo hadi asubuhi......Ruta ujue baba mchungaji amepunguza kasi kabisa kwa wajane,hujagundua tu.:amen:
 
Last edited by a moderator:
fofooffoooo hadi asubuhi......Ruta ujue baba mchungaji amepunguza kasi kabisa kwa wajane,hujagundua tu.:amen:

kwa hiyo wataka kuniambia ya kuwa baba Askofu sasa kahamia wapi? isije ikawa kahamia kwako..................LOL............nitalia mie kama ndivyo hivyo.........[MENTION]@Vaislay[/MENTION]
 
ndio maana nasema ni bora hawa viongozi wa dini wasiooa bora nao waoe tu-maana wengine wanashindwa kuhimili tamaa zao

huyu askofu ana mke na watoto wakubwa tu na hata wajukuu anao..........tatizo mwanadamu haridhiki na alichonacho ataka na vinginevyo navyo atafune kama khali yaruhusu..........
 
Hii reference haiwalengi wajane tu, kama tafsiri yako ya askofu ndiyo hiyo uliyoiweka ambayo inazigusa pia na NGO. Kwa hakika wasichana wabichi na wake za watu ambao wanahangaika kutafuta kazi na pengine wanakwenda kwa hawa watu ambao wanasimamia mashirika ya misaada, na hujikuta wakilazimika kuweka rehani hiyo mali yao adhimu ili kupata kile wanachokitaka. Ni bahati mbaya sana kwamba watu hawa wanaotaka kila kinachoonekana, huwa si wazima. Sasa mkeo atapolazimishwa kumegwa ili mradi wake ufike, ndipo atakapoleta maradhi humo nyumbani. Naye binti kigoli anayemegwa na maaskofu wa aina hii, atajikuta kwenye akiingia kwenye ndoa akiwa na virusi. Na bahati mbaya vijana wengi hawapimi virusi kabla ya kufunga ndoa. Hii ni hatari sana.
 
Vaislay umeamkaje? Umeng'atwa usiku wa leo au umelala fofo tu...............wajane kabali yao ni kali kwa sababu tofauti na hao wasichana ni kuwa wajane wengi saa zimesogea na hawapo sana sokoni kwa hiyo wana aina fulani ya kujikuta lupango na wanapopewa masharti hujikuta hawana namna bali kujisalimisha kwa Baba Askofu....[MENTION]@Vaislay[/MENTION]

Ikiwa hivyo baba askofu hajambo na wapo wengi kweli. Hofu yangu ni kumaliza hata mzizi ulibaki maana usalama ni lazima utakuwa ni mdogo sana.
 
Hii reference haiwalengi wajane tu, kama tafsiri yako ya askofu ndiyo hiyo uliyoiweka ambayo inazigusa pia na NGO. Kwa hakika wasichana wabichi na wake za watu ambao wanahangaika kutafuta kazi na pengine wanakwenda kwa hawa watu ambao wanasimamia mashirika ya misaada, na hujikuta wakilazimika kuweka rehani hiyo mali yao adhimu ili kupata kile wanachokitaka. Ni bahati mbaya sana kwamba watu hawa wanaotaka kila kinachoonekana, huwa si wazima. Sasa mkeo atapolazimishwa kumegwa ili mradi wake ufike, ndipo atakapoleta maradhi humo nyumbani. Naye binti kigoli anayemegwa na maaskofu wa aina hii, atajikuta kwenye akiingia kwenye ndoa akiwa na virusi. Na bahati mbaya vijana wengi hawapimi virusi kabla ya kufunga ndoa. Hii ni hatari sana.

Baba Askofu hapa ni yule ambaye kashika mpini na mnyonge kakamata ncha ya makali......ninaafiki khoja zako zote.
 
Ikiwa hivyo baba askofu hajambo na wapo wengi kweli. Hofu yangu ni kumaliza hata mzizi ulibaki maana usalama ni lazima utakuwa ni mdogo sana.

losambo uko juu sana................
 
Hawa jamaa ni noma, wanawakamuaje! Sitaki hata kuwasikia
Ta Kamugisha hawa waheshimiwa hudai kama wanataka kula basi kwanza nao waliwe.................na hawa mababa Askofu hata kwenye siasa wamefurika...............[MENTION]@Ta Kamugisha[/MENTION]
 
Nisingependa niwe mnafiki, utamu (pengine hata mahitaji tu) hauchagui dini.
Baba Askofu ikiwa zake ndio hizo hatachagua kama ni mjane, kigoli au mke wa mtu,
halmuradi tu kaombwa na alisikiliza maneno ya mkuu wa kaya - ukitaka kula, uliwe.

Ninachomlaumu Baba Askofu ni kucheza pekupeku. Anaweza kuambukiza, anaweza
kuambukizwa. Pia asijeshangaa siku moja anapelekewa timu ya watoto wake; matunda
ya uzinifu wake. Kwakuwa ameikiuka amri ya "usizini", basi angalau afuate amri ya 11,
"Ukishindwa kujizuwia, tumia kondom," au ile ya "Ukijipenda, utajilinda.
 

Similar Discussions

16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom