abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu amesema ombi la serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Umoja wa Mataifa kuomba nyongeza ya mpaka katika Bahari ya Hindi ni kuipokonya Zanzibar haki yake. Jussa amekusudia kuwasilisha hoja ya binafsi katika Baraza la Wawakilishi Jumatatu, akitaka lazima kuwepo na mazungumzo ya kuamua nani anamiliki nini kati ya Tanzania na Zanzibar kabla ya ombi hilo kuwasilishwa katika Umoja huo.
Ombi hilo tayari limeshawasilishwa katika Umoja wa Mataifa, New York, na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi wa Tanzania, Professa Anna Tibaijuka, akitaka kilomita 150 zaidi za bahari. Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe, Ismail Jussa aliyeliibua suala hilo kwenye Baraza la Wawakilishi hapo juzi, Amina Abubakar amezungumza na Ismail Jussa kuhusiana na msimamo huo kwa kusikiliza mahojiano hayo.
Ombi hilo tayari limeshawasilishwa katika Umoja wa Mataifa, New York, na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi wa Tanzania, Professa Anna Tibaijuka, akitaka kilomita 150 zaidi za bahari. Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe, Ismail Jussa aliyeliibua suala hilo kwenye Baraza la Wawakilishi hapo juzi, Amina Abubakar amezungumza na Ismail Jussa kuhusiana na msimamo huo kwa kusikiliza mahojiano hayo.