The Planner
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 357
- 118
Kila kitu katika dunia hii kina hatua zake toka kuzaliwa (kuanzishwa) mpaka kufa kwake, Katika kila hatua kuna changamoto zake lukuki, lakini changamoto ndo zinafanya hatua inayofuata iwe bora zaidi, lakini mmh si katika muvi za Bongo. Leo nataka japo kwa ufupi kujadili suala la "Bongo Movies" jamani maproduza wetu hata kama tupo katika hatua za awali katika tasnia hii hebu basi jaribuni kuweka uhalisia kidogo, kuna baadhi ya movie zinachefua kwa kweli, yaani unakuta watu wako makaburini ndugu wa marehemu anakunywa bia na kucheka pembeni yake kitu ambacho katika utamaduni wetu wa kitanzania hakipo. Halafu tusiponunua mnalalamika hatuna uzalendo wala hatuwasapoti, jamani mnachefuaaaaaaa.................jirekebisheni!