Baadhi ya mambo ya msingi yanayopaswa kuwemo kwenye katiba mpya; nionavyo mimi, wewe je!

MAJOKA

New Member
May 3, 2012
2
1
Ndugu wanaJF salamu

Kutokana na mchakato tulionao hivi sasa kuhusu mabadiliko ya katiba yetu, leo nimependa nitoe maoni yangu kuhusu baadhi ya mambo ambayo ningipenda yaingizwe kwenye katiba mpya tunayoitaka.

Fuatana nami na utoe na yako ili tuweze kuboresha katiba ijayo.

1. katika katiba ijayo ningependa idadi ya wizara zipungue mpaka 10 to15 tu, zitajwe na ziwe "fixed". Sio leo anakuja Raisi huyu na wizara zake kulingana na anavyoona yeye. Mara Wizara ya Uwezeshaji, mahusiano nk, ilimradi tu kupeana ulaji. Hii siyo sawa hata kidogo, lazima kuwe na utaratibu unaoeleweka wa kufuatwa na kila mtawala.

2. katiba ijayo izungumzie sera za nchi kwa kila wizara, idara na mashirika ya umma. siyo leo anakuja mkubwa huyu anakuja na mipango yake. Sote ni mashahidi ktk haya; Mungai alikuja na sera ya kufuta michezo mashuleni na kuunganisha masomo mashuleni, leo tunashuhudia mabadiliko mengine tena. yaana hakuna la kueleweka.

3. Katiba mpya iwaondoe wabunge kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya. Raisi ateue mawaziri kutoka uraiani.
4. Wakuu wa idara na tasisi za umma wateuliwe na raisi na kuthibitishwa na bunge ama mabaraza ya madiwani katika ngazi husika.
5. katiba mpya itamke wazi kuwa kila kiongozi wa kisiasa aweke maslahi kwanza kwa nchi na si kwa chama. kwa maana hiyo lazima kuwa na wagombea uongozi huru.
6.Katiba mpya itamke uwepo wa serikali ya Tanganyika
7. katiba mpya itamke adhabu ya kifo kwa mafisadi wa mali ya umma.
8. katiba mpya itamke mali zote zilizohodhiwa na CCM ambazo zilipatikana wakati wa chama kimoja zirudi serikalini na ziwe za umma wote wa waTZ na si ilivyo sasa kw CCM kumiliki mali zote km viwanja vya mpira, majengo, viwanja nk

Ndgu wanaJF hayo ni baadhi tu ya mambo mengi ninavyoona mie yawemo kwenye katiba mpya ijayo. Wewe je, unayoya kwako?

Tujadili!
 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa. Nikianza na ya tatu na nne nadhani iboreshwe zaidi. Iwe kama ya katiba mpya ya Kenya. Hao jamaa wafanye application kabisa na interview yao ifanyiwe bungeni tena live kabisa. Ili kila mtanzania ajue mbabaishaji na mzuri. Na maswali yaulizwe na wataalamu waliobobea na wala sio wabunge kama Lusinde.
Hiyo ya sita nilikuwa naona uiboreshe vizuri. Kuwa kama haitamki uwepo wa serekali ya Tanganyika, basi isiwepo serekali ya Zanzibar. Leo hii JK ameteua kamati ya kukusanya maoni ambayo nusu wanatoka Zanzibar ili Wazanzibari watuamulie mambo ya maji, aridhi yetu, tawala za mikoa yetu, na wizara kibao ambazo sio za muungano.
Katiba iondoe kinga ya kushitakiwa kwa maraisi wastaafu. Kwa sababu naona Ikulu imekuwa sehemu ya kufanyia ufisadi kwa sababu hata raisi akiondoka anayo Kinga. Mpaka sasa maraisi Mwinyi, Mkapa na JK wamefanya mambo ambayo wangetakiwa washtakiwe lakini hiyo haipo.
Madaraka ya raisi yapunguzwe saana na yale ya waziri Mkuu yaongezwe kidogo ili tuondokane na tatizo kama lile la David Jairo.
Wananchi wamiliki aridhi yao kama Zanzibar. Kuwe na tofauti kati ya aridhi ya serekali na ile ya wananchi.
 
maana ya wateule kuthibitishwa na bunge ni kuhitaji uungwaji mkono wa wateule kwa umma kupitia wawakilishi wao.
ili nione mantiki kwenye mapendekezo yako, chakata, ni vipi wabunge watawajibika kwa wananchi (wapiga kura wao) na sii kuwajibika kwa vyama, chakata ni vipi rais atawajibika kwa nchi yake na sii kwa nchi nyingine, Nakutolea mfano mmoja wenye lengo la kuboresha huduma za afya na ushirikiano wa kimataifa.

ITAKUWA NI MARUFUKU KWA WATUMISHI WA UMMA KUTIBIWA NJE YA NCHI.
ATAHESABIKA AMEJIFUTA KAZI MTUMISHI ATAKAYEKIUKA IBARA HII.

MIKATABA YOTE YA SERIKALI ITAANDIKWA KWA KISWAHILI, NA LAZIMA IWE NA KIPENGELE KINACHOWAPA MAMLAKA WANANCHI KUPITIA WAWAKILISHI WAO AMA MWANANCHI MMOJA MMOJA AU KIKUNDI CHA WANANCHI YA KUUPITIA ILI KUBAINI KAMA KUNA HASARA AMA UDANGANYIFU, WAWE NA MAMLAKA YA KUUSITISHA MKATABA KWA AMRI YA MAHAKAMA KUU.

nimekutolea mfano.
 
· NAPENDEKEZA YAFUATAYO KATIKA KATIBA MPYA

MIKATABA YOTE INAYOHUSU NCHI IPITIWE NA TUME/JOPO LA WATAALAMU ALAFU IPELEKWE BUNGENI KABLA YA KUSAINIWA NA RAISI.

UWEPO WA MABUNGE MAWILI


(I) BUNGE LA UWAKILISHI
Hili ni bunge ambalo litatokana na kuchaguliwa kutoka kila wilaya ,na mbunge atakua mwenyekiti wa hamashauri husikahivyo basi kila wilaya itakuana mbunge mmoja .hii itasaidia kupunguza idadi kubwa ya wabunge , kuondoa mgongano wa madaraka kati ya mbunge na mkiti wa halmashauri, pia kuwa kiungo kati ya serikali kuu na serikali ya mitaa.yaani halmashuri.kwa mfano kwa sasa tungekua na wabunge133.Nafasi ya mkuu wa wilaya isiwepo majukumu yake yachukuliwe na mkurugenzi wa wilaya.
(11)BUNGE LA WANANCHI
Hili ni bunge litakalotokana na kila mwananchi kuwa na nafasi ya kushiriki ,kuchangia ,kupanga , na kuamua masuala ya kitaifa litakua na m/kiti na katibu wake hili ndilo litakua msingi wa maamuzina ushauri kwenye bunge la uwakilishi ,kila mtanzania atapata fursa ya kushiriki na kusema chochote atakachoona kinafaa ili kuimarisha taifa.linaweza likawa linafanyika kwamwaka mara tatu kwa mwaka kujadili mustakabali wa taifa,

BARAZA LA MAWAZIRI

baraza la mawaziri liwe ni chombo cha kiutendaji ,hivyo basi liundwe na wataalamu waliobobea ambao watakua ni watumishi wa wa umma nawatawajibika kwa bunge kwa utendaji wao.na watakua wanapewa malengo endapo watashindwa kufanikisha malengo hayo watatolewa kwenye nafasi zao ili kuondoa siasa zisizotekelezeka,

USIMAMIZI WA FEDHA

Usimamizi wa fedha uwe chini ya CAG na HAZINA, hazina watatakiwa kupeleka fedha zote kwakuingiza kwenye akaunti zinazohusikakama ni miradi,vijiji, shule,halmashauri au taasisi kupitia akaunti zao mkurugenzi wa wilaya atakua ni msimamizi tu hii ni kuondoa ubadhirifu wa fedha za umma.la msingi ni kuimarisha taasisi hizi.

UWEPO WA TUME HURU YA UCHAGUZI

Tume ya uchaguzi huru isiyofungamana na upande wowote,pia iwe na mamlaka ya kushitaki au kushitakiwa na mtu yeyote kikundi au taasisi yeyote,chama.

IAINISHE VIPAUMBELE VYA TAIFA

Katiba mpya inatakiwa kuainisha vipaumbele vya taifa,ili kila kiongozi au utawala utakaochukua madaraka ujikite kutekeleza vipaumbele hivyo.kwa upande wangu napendekeza teknolojia ndio kiwe kipaumbele namba moja.

 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom