Baadhi ya Lecturers wa Mzumbe wana degree Feki - VC wao naye FEKI

FD,

Acha bwana, acha, acha kabisa. Wewe huitaji kujirudisha chini kiasi hicho. Of course ninajuwa unamtupie Mkandara vijembe hapa. Usikate tamaa wacha tuendelee kulalamika pengine tutafanikiwa siku moja pamoja na ugumu alioueleza kwa kina Mlalahoi. Nami pia ninauona ugumu huo. Lakini huyu waziri naye mbona alikuja na nguvu za soda akatutia matumaini sasa mbona naye ameingia mitini. Au na yeye anaogopa kutajiwa yake. Inavyoonekana ni kuwa kila mmoja anazinduka kujuwa kuwa yumo mwenye nyumba ya vioo kwa hivyo hastahili kuwatupia wengine mawe. Nadhani hili ndilo linalotukwamisha. Tungetegemea vyuo vyetu vya serkali viwe msimamo wa mbele kutetea hadhi ya elimu kwa hivyo Cs na VCs wao wangwekwa kwenye jopo la kutathmini shahada lakini ----- lo, lo, lo utamuweka Warioba humo utegemee ajiumbuwe kuwa PhD za PWU ni feki -- mama yangu weeee, ngumu hii.

By the way, si mmeona ya Magufuli, yeye anaongelea viwanja, wajameni wanafukuta na mauzo ya nyumba kwa nduguye Musa. Eh Walume, uraisi wa Tanzania NI KASI (kajob) BABANGU!

fikiraduni said:
Mlalahoi,

Na mimi nimetuma hela jana, baada ya wiki kama nne nitakuwa Dr.!
Kwasababu serikali yetu imeruhusu, basi na mimi nimeingia humo.

Tena naomba muache kutujadili, nikishaupata u dr basi narudi bongo, ajira serikalini. Upo hapo?

FD
If you cant beat them join them!
 
Mkandara,

heshima yako, nafurahi kusoma maandishi yako na kuwa angalau sasa unakubali kuwa shahada tulizokuwa tunajadili tangu BCS ni feki.

FD
Nakuhakikishia tar 3 Novemba 2006, nitakupa heshima yako ya "Dr", ahahahah
tena nitakuomba unisimamie tasnifu yangu..............ahahaha

Mwl.Moshi & Mlalahoi
Good points Bros, endelezeni shule, sincerely, najifunza mengi toka kwenu
 
fikiraduni said:
Mlalahoi,

Na mimi nimetuma hela jana, baada ya wiki kama nne nitakuwa Dr.!
Kwasababu serikali yetu imeruhusu, basi na mimi nimeingia humo.

Tena naomba muache kutujadili, nikishaupata u dr basi narudi bongo, ajira serikalini. Upo hapo?

FD
If you cant beat them join them!

Hongera sana
 
Jizalendo,

Nilikuwa nachokoza POINTS kutoka kwa mzee Mkandara. Nimefurahishwa na kukubali kwake na kuelezea ugumu wa kuzikabili na vilevile hapo hapo kusema sio FEKI. yupo sahihi kwa pande zote. Ametazama kote na kuelezea ubaya na uzuri.

Tumekubaliana kuwa hizi degree kuziita FEKI ni sawa na Kutoziita FEKI pia ni sawa. Ndio maana nami ninachukua Phd.

Mlalahoi,

Unapoteza muda kusomea Phd kwa miaka mingi. Kama upo serikalini na mawaziri wako wanazo kwanini upate taabu?;-)

Asante

FD
 
fikiraduni said:
Jizalendo,

Nilikuwa nachokoza POINTS kutoka kwa mzee Mkandara. Nimefurahishwa na kukubali kwake na kuelezea ugumu wa kuzikabili na vilevile hapo hapo kusema sio FEKI. yupo sahihi kwa pande zote. Ametazama kote na kuelezea ubaya na uzuri.

Tumekubaliana kuwa hizi degree kuziita FEKI ni sawa na Kutoziita FEKI pia ni sawa. Ndio maana nami ninachukua Phd.

Mlalahoi,

Unapoteza muda kusomea Phd kwa miaka mingi. Kama upo serikalini na mawaziri wako wanazo kwanini upate taabu?;-)

Asante

FD

Mheshimiwa FD,

Mwenye highest qualification kwenye ukoo wetu ana certificate of attendance baada ya kuhudhuria indoor short-course ya siku 3.Hii mission ya PhD ni more than personal,ni ya ukoo wetu mzima,na wamenishikia bango.Njia za mkato zipo lakini mie ni muumini wa falsafa ya no gain without pain.
 
Fikiraduni,

Unapofikia maamuzi ya kufanya kitu mshikaji siwezi kukushika shati!... mimi mwenyewe mbabaishaji tu ktk maisha. Ukinifunulia channel mshikaji siiachi umemwona Michuziline sii mwenzetu tena. baadhi ya waandishi watabaki wakipiga kelele na kuimba kuhusu mshikaji lakini ndio kisha punch sio!.. halafu kikubwa michuzi anajua utangazaji wa picha, anafahamu tamu ya Mdanganyika na nini akiweke kuliko waandishi kibao wenye hayo madigrii yenu. Kwa hiyo hata ukisema unataka kuuza unga nitakuunga mkono maadam unafahamu unacho kifanya.
Tatizo la wengi hapa ni lugha nayoitumia.
Toka bcstimes niliwambia vipo vyeti navyovikubali kama FEKI, ambavyo hutolewa na baadhi ya shule ama watu bila mhusika kufuzu masomo...Hivi vyeti sina kabisa maneno kwani hata ktk mtandao kuna watu kibao wanaviuza.
lakini Mnaposema eti PWU ama COU wanatoa vyeti FEKI mshikaji inabidi uje na ushahidi wa kutosha! Na kibaya mnachukulia jina la chuo kama sababu ya elimu kuwa FEKI na wengine mnachukulia muda wa mafunzo!.
No mshikaji vipo vyuo unaweza kupata elimu nzuri kwa malipo madogo kabisa.. UDSM zamani ilikuwa bureee! Je, huko Ulaya wangeikataa digree ya UDSM kwa sababu ni bure?..Pia wapo maprofesa waliosoma Bulgaria na Urusi ktk vyuo visivyotambulika na body hizi hasa wakati wa vita baridi.
Haya tukiangalia swala la Muda.
Hapo zamani Vyuo vingi vya Ulaya vinaweka muda mrefu wa masomo kwa sababu moja kubwa LUGHA. Kwa hiyo digrii nyingi ilikuwa miaka mitano. Miaka miwili ya mwanzo huchuliwa kama miaka ya kujifunza lugha kisha mitatu ya ELIMU husika.
Siku hizi mshikaji, ELIMU nyingi zimekwisha tafsirika kwa lugha na pia tunachagua wenyewe chuo kulingana na lugha. Maswala ya kutupwa Uturuki mara Bulgaria hayapo tena kwa hiyo watu wanaweza kabisa kumaliza digrii kwa muda mfupi. Na binafsi naamini kizazi hiki mnafahamu mambo mengi mapema sana kuliko sisi. Mfano mzuri ni huyu kijana Mushi anavyotupeleka puta wazee wazima hali hana hata umri wa miaka ishirini (navyosikia).
Enzi zetu miaka kumi nyuma kama hukujifunza Java miaka miwili huwezi kabisa kutupa hadithi hii yaani haiwezekani kabisa ukaunda tovuti!
Leo hii ni swala la siku tu tena huna haja ya kwenda darasani! maadam uwe software umemaliza kazi na kuna vijana kibao nawafahamu wanachezea PC kwa kujifunza wenyewe nyumbani. Shule ama darasa ni software zinazowaongoza na hawana hata lecturer zaidi ya hiyo disc. Na mshikaji wanafanya wavitu kishenzi, siwezi kusema elimu yao ni FEKI eti kwa sababu hawakwenda Chuo fulani cha mafunzo ya PC.
Anyway, sikubali UFEKI kwa tafsiri ya baadhi ya hawa wasomi wetu wanapo vichambua baadhi ya vyuo kwa sababu tu havitambuliwi na body fulani za Ulaya hali nchi yetu haina mkataba na body yeyote kati ya hizo nyingi za Ulaya.
Mwisho, Fikiraduni unafahamu fika kwamba vijana wetu kibao wamekwenda hizi University za community ambazo hazitambiliki. Ukitazama swala la ada zake nakuhakikishia kati ya wanafunzi 100 only 10% wamekwenda vyuo vinavyotambuliwa na accredition body alizozitaja Dr. Asaad. Huwezi kusoma vyuo hivyo kwa mwaka chini ya dollar 12,000 bila malazi na sidhani kama kuna Watanzania wengi wamesoma vyuo hivi hapa Marekani.
Je, Wabongo wote 90% waliosoma Marekani elimu yao ni FEKI?
 
Mkandara,
Tumekubaliana. Kuna kitu kimoja ambacho hata mimi nimekiona. Wengi wanajali sana formal education, wakati sio sahihi.

Mfano, miaka ishirini iliyopita na sasa hivi ni tofauti kabisa. Kuwa na access na internet ni somo kabisa na unatakiwa upewe maksi fulani, maana unajifunza mengi mno!, humu kujadiliana tu na kuchangia mawazo kwa mtu kama MLALAHOI anapata points za Phd yake!

Masomo ya kusoma maandiko na mawazo ya mtu mwingine kisha useme ndio umeelimika sio dili. Unaweza kuvumbua au hata kujisomea vitabu visivyo rasmi na ikawa upo fresh.

Kitu kingine ni experience. Mtu mwenye masters na experience ya miaka kumi kazini au kwenye taaluma na hizi internet zetu huwezi kuniambia akiandika na kupeleka kazi yake asipewe Phd!!. Nakataa kwasababu huwezi kumlinganisha huyu mtu na kijana aliyeunganisha vyote vitatu bachelor to Phd. Huyu wa mwisho atakuwa amekariri maoni au maandiko ya wengine, wakati mwenye experience ya miaka kumi na masters na Phd ya COU ya wiki nne atakuwa yupo DEEP zaidi na masula husika.

Kwa hilo Mkandara tupo pamoja. Life ni Life, itafute iwezekanavyo, BTW kwanini tunasoma? degree moja haitoshi kweli? inatosha tunachotafuta ni sifa au mkate wa kila siku.

Nikishamaliza Phd yangu nitawataarifu.

FD
 
HIVI WE ASSAAD UNAWAFANYA WENYE MAMLAKA ZA UTEUZI NCHI HII NI WAJINGA KIASI WEWE KUWEPO HAPO ACCOUNTING DEPARTMENT UDSM UKAONA UNA AKILI KUPITA RAIS MSTAAFU WA JAMHURI YA MUUNGANO?

INAJULIKANA TOKA ZAMANI KWAMBA UDSM WAKISHIRIKIANA NA IFM HAWAITAKI MZUMBE NA WANGEKUWA NA UWEZO WANGEIFUTA. TUANGALIE VIGENZO VICHACHE
1. ILI USHINDE CONSULTANCY YA SERIKALI LAZIMA UANDIKE PROPOSAL YA MAANA YENYE USHINDANI. MZUMBE IMEFANYA CONSULTANCIES NYINGI SAN ZA SERIKALI NA KWA BAHATI NZURI NI KWAMBA HAO UDSM, IFM, CBE, TIA NAO HUWA WANAOMBA NA WANAKOSA MZUMBE WANASHINDA SASA IWAJE MALALAMIKO YAJE HAPA?

2. KUNA SOMO MOJA LINAITWA 'STRATEGIC MANAGEMENT' AMBALO HUFUNDISHWA UNDERGARDUATE NA POSTGRADUATE PIA KATIKA MOJA YA TECHNIQUE ZA KUWIN BUSINESS NI KUWEZA KUWATAMBUA WASHINDANI WAKO SASA UDSM WAMEGUNDUA KWAMBA WAO SI 'THE LEADING UNIVERSITY' TENA BALI NI MZUMBE WANACHOAMUA NI KUCHAFUA JINA LA MZUMBE.

3. TANZANIA KUNA MABARAZ MAWILI YA PROFESSIONALS AMBAYO NI NBAA NA NBMM KWA MIAKA KADHAA SASA WANAFUNZI HUFANYA MITIHANI YA MABARAZA HAYA. PAMOJA NA KWAMBA WENGI HUSHINDWA REKODI ILIYOPO INAONYESHA MZUMBE WANAONGOZA KWA KUFAULU MITIHANI ILE. KAMA HUAMINI KAWAULIZE IFM.
4. KATIKA SOKO LA AJIRA VILE VILE MZUMBE WANAONGOZA. IKIWA KAZI ZINAOMBWA NA WATU WANAITWA KWENYE USAILI NA KILA KITU KINAENDESHWA KATIKA MISINGI YA UWAZI NA HAKI IWEJE MZUMBE WASHINDE KILA MARA. NENDA KATAFUTE DATA LAPF, CRDB, HAZINA, BP, ERNEST N' YOUNG, PWC, KPMG, NMB, NA SERIKALINI. NI MAJUNGU TU KWAMBA UDSM HAMTAKI GRADUATES KUTOKA MZUMBE.

5. INTAKE YA FIRST YEAR MZUMBE KWA MFANO MWAKA HUU IMECHUKUA DIVISHENI ONE TU NA KWA UCHCHE SANA HAWAFIKI 15 DIVISHENI TU NA NI KWA PROGRAM MOJA YA B.SC(POM) SASA HAPO UDSM HADI DIVISHENI THREE KIBAO WAMECHUKULIWA KWA NINI MSIENDELEZE MAJUNGU.

6. KWAMBA WAHADHIRI WA MZUMBE WANA Ph.D ZA PWU SASA Ph.D YA PWU UTAIFANANISHA NA HIYO YA UDSM ACHENI USHAMBA WA KITAALUMA!

7. UNASHANGAA NINI KUONA MTU AMEPATA Ph.D KWA HARAKA KWANI HUJUI KAMA PETER MSOLLA ALIPATA Ph.D KABLA TYA MASTERS? TAFUTA DATA.

8. SAWA UDSM KUNA MAPROFESSOR NA MADAKTARI TUJIULIZE BASI HAO NG'OMBE, MBUZI, KELELE ZA KUKU, NYUMBANI KAMA GEREJI YAMETOKA WAPI? KWA MAANA TUNAJUA PROFESSOR AFANYE KAZI ILE ALIYOAJIRIWA NA MWAJIRI WAKE SASA KUWA NA VYOTE HIVYO SI AWEZA KUWA LECTURE RUM MARA APIGIWA SIMU NG'OMBE AMEANGUKA HUKU NA DAWA HAMNA MATOKEO NI KUACHA LECTURE NA KUKIMBILIA NG'OMBE NYUMBANI AU PORINI MAKONGO AU KOKOTE?

9. UKITAKA KUJUA KAMA MZUMBE IS THE BEST KAWAULIZE WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA PALE UDSM WANAOSOME SHERIA NA UHASIBU PAMOJA NA UTAWALA KWAMBA WANGEJISIKIAJE KAMA WANGEPATA UDAHILI MZUMBE?
NENDA UKAPATE JIBU. TENA WEWE ASSAAD WAULIZE SI UPO HAPO HAPO?

10. WACHANGIA HOJA KARIBUNI KWENYE MJADARA. LAKINI NAWAPA ANGALIZO HUYU ASSAAD AMEWEZA KUKOPI CV's ZA WAHADHIRI MZUMBE KUTOKA KATIKA PROSPECTUS AMBAYO NI PUBLIC DOCUMENT INGEKUWA WALE JAMAA WANA HOFU NA ELIMU YAO WASINGEYAANDIKA HAYO. NENDENI MZUMBE MKAJIONEE MAMBO BADALA YA KUKAA TU NA KUSIKILIZA NINI NANI ANASEMA NINI.

11. HALAFU ANYESIFIA ETI MTU KASOMA ALIPORUDI KAKATALIWA KWAMBA Ph.D YAKE FEKI HAPA NI KUVUKA VIWANGO VYA JUU VYA UVUNJAJI WA HAKI ZA BINADAMU.
 
najribu tu kueleza umma kwamba UDSM na MZUMBE zote ni universities lakini kuna kitu kimoja hakieleweki upande mmoja kwamba kama ulikuwepo si kila siku ni wewe tu. watu wa UDSM lazima waikubali mzumbe na huu mtindo wao wa kukataa graduate wa mzumbe katika employment vacancies zao ndio utakaowamaliza.
pale mzumbe staff ni kutoka vyuo vyote hadi TUMAINI wa UDSM ndo wamejaa na wanaisuka mzumbe kwa kushirikiana na wakongwe wa pale hii inaleta maan . UDSM ushamba wa kitaaluma utawaghlimu zaidi na zaidi.
 
Falesy

Usichanganye watu.
Hamna mtu anayesema wahitimu wa UDSM ni bora kuliko wa Mzumbe au vice versa, kinachozungumzwa hapa ni wakufunzi wa vyuo husika na nyadhifa zao.

Tunataka mtu akiwa na PhD basi iwe ni PhD inayofahamika ilipatikanaje na kutoka chuo gani.
Ukijaribu kuangalia wengi wa wenye PhD hapo Mzumbe wamezipata kutoka chuo kimoja na kwa wakati mmoja na chuo chenyewe ni Online. Naomba unitajie chuo kimoja tu chenye hadhi duniani kinachotoa PhD online tena hata bila kuwa na thesis.

Kwa sababu wewe upo Mzumbe au una uelewa wa mzumbe, tupatie title za thesis za hao PhD holder wa PWU. Nimepita maktaba kuu ya Serikali (ambayo kisheria ina nakala za kila thesis) lakini sijafanikiwa kupata copy. mzumbe wenyewe hawa kwenye Maktaba yao. Mimi nakupa laki mbili (200000) utuletee angalau thesis mbili tu.

Swala lingine ni watu kusema wamepata Masters kutoka Mzumbe miaka ambayo ilikuwa bado siyo University na ilikuwa haijapewa mamlaka ya kutoa Master hata degree bali walikuwa wanatoa Diploma na Advanced Diploma.

Mengine yote uliyosema siyo relevant na subject tunayozungumzia.

BTW: Tanzania huhitaji kuwa mjuvi kuteuliwa au kupewa wadhifa, cha muhimu ni politics na connections.
 
Aljazeera

Juhudi kubwa unayoifanya kumuelimisha huyu bwana ni uungwana tosha sana, hiyo h/w uliyompa najua hawezi kuifanya (ajabu kaona mabaraza mawili tu ya professionals in Tanzania!!!), muulize swali moja tu, kwanini alienda/ali-join Mzumbe?, i dont believe that was his/her best choice..................Agreed kuna best products toka Mzumbe, however, watu kama Falesy, Nungwi et al ..................mmmhhh, Mungu saidia.
 
Falesy,

Ndugu yako Nungwi alikuja na moto. AKASHUKA. AKAPOA.MWISHO AKAKIMBIA.
Sina haja ya kulinganisha wanafunzi kwasababu ulichosema ukikigeuza ndio ukweli. Huwezi kulinganisha chuo kikuu chenye miaka mitano na chenye miaka 30!!!. man you must be kidding!. Anyway sihitaji kwenda deep nahofia na wewe utakimbia kama Nungwi. Angalia walivyokujibu hapo juu. Mmoja wapo ni product ya UDSM mwingine ni product ya chuo kimoja Canada (Aljazeera na Mkuu Ogah) kisha linganisha na uandishi wako na majibu yako (Mzumbe product) utaelewa the difference kati ya waliofundishwa na maProfesa wa kweli na ma daktari wa COU!.

Hilo la ajira tumeshaliongelea na ni kweli mzumbe wamejaa serikalini tu! sehemu nyingine UMEONGOPA!. Hilo lina explain kupata tenda serikalini! Accountant General ni Mzumbe, Auditor General ni Mzumbe, what do you expect!?!. Tumeongelea divisions pia. Hakuna mtu duniani atakaye penda kusoma advanced diploma kama anaweza kusomea DEGREE. Nenda Venezuela kawaambie una BBA kisha Ogah aseme ana Bcomm. Watakuuliza BBA ndio nini? Ila Bcomm wataelewa mara moja.

Soma mada toka mwanzo kisha weka maoni, jazba ni the last thing. Nilikuona kule kwenye udini, kasome nilichowaandikia.

Na wala hakuna aliebeza Mzumbe product, soma mada inahusu nini.

Inferiority complex isikutawale!

Thanx

FD
 
Yaani mshkaji unabeza Chuo kikuu cha 13 kwa UBORA AFRICA?!!?

ahahahahahaha
Wamemaintain standards (like hawana PHD FEKI) ndio maana ni ya 13, out of vyuo 11 vya South Africa na chuo kimoja Misri hakuna chuo chochote Africa kinachofikia standards za UDSM!!!. Kama unapinga na hili sihitaji hata kujadiliana tena na wewe kuhusu hii mada.

FD
 
Duh!
Mac,

Ni vizuri kuchangia lakini ni vizuri kuchangia pia kwa kuangalia mada inasemaje. Mwenzio akitoka nje ya mada unatakiwa kumrudisha, na wewe ukiendelea kuchangia nje ya mada ndio kwaanza mnakuwa sawa na wa kwanza.

Kama hukuelewa mada inahusu nini uliza tutakukumbusha.

FD
 
Another interesting article in relation to "authenticity" of PWU degrees!

November 16, 2004 at 10:07PM MST
Investigators: Degrees for Sale

Increase your earning power with some cash and a click of the mouse. It may be that easy.
People around the country walk away with diplomas from online schools in a matter of months. And some of them earn more money because of it.
But the degrees they hold may not be worth the paper they're printed on. And you may be picking up the tab.
The Investigators on Eyewitness News 4 show you Degrees for Sale.
(Online commercial: ) "Hi, and welcome to Pacific Western University. You no longer need to sit in a classroom to learn and earn a bachelor, masters or doctorate degree in order to grow and earn more as a professional."
This is an online ad for Pacific Western University. But it may not tell the whole story.
Pacific Western is one of seven schools labeled as a diploma mill by federal investigators at the U.S. General Accounting Office.
Their report was used in a senate investigation this year.
Many online schools are perfectly legitimate. But diploma mills issue degrees sometimes without requiring any student academic work or based solely on "life experience."
The government's investigation found that federal employees had obtained degrees from the online schools, like Pacific Western , with the U.S. government picking up the tab.
"As long as you have a computer and an internet connection you can be a university." Education author John Bear is a former consultant to the FBI task force that cracked down on diploma mills.
"The internet is the fondest, wildest dream of the diploma mills operators come true. Most importantly, they can maintain the fiction that they are a real place," says Bear.
So the investigators set out to find Pacific Western University. We pay a visit to its "campus" located in Los Angeles. We don't find students, classrooms or professors. Only a small office with two receptionists and a man who introduces himself as the dean.
We're handed a small registration packet that boasts successful graduates and high standing faculty. And we're told all course work takes place online.
So we ask how fast we can get a degree to teach in Arizona.
"Often our courses don't meet what the state requires in Arizona."
It won't meet the credentialing requirements for Arizona, this program. But wait a minute.
The Investigators found educators who are teaching right here in Tucson and some of them made more money because of degrees from Pacific Western University.
Dr. David G. Iadevaia teaches at the Pima Community College east campus. Where he's been on the payroll for more than ten years.
While he holds an accredited degree from the University of Rhode Island, he also has a PhD from Pacific Western University.
Pima tells The Investigators the PhD put Iadevaia in to a higher salary bracket. Earning him an extra $32,000 since 1992.
We also talked to PCC about Dr. David R. Bishop, a faculty member at the downtown campus.
While holding credible degrees from two accredited schools, St. Louis University and Loyola University, Bishop also holds a PhD from Pacific Western University.
Because of that PhD, Pima says he's been paid an extra $13,000 since 1997.
We tried interviewing both men about their PhD's, but neither was interested in going on camera. Both say they feel misled by Pacific Western University. And thought the university was a credible school.
Pima Community College conducted their own internal audit of faculty members last July about the same time we began our investigation. They discovered both those professors were using degrees from unaccredited schools.and so revoked their PhD standing, and reduced their salaries.
But PCC is not going to ask the professors to reimburse taxpayers or face any disciplinary action.
The Investigators wanted to know why. PCC authorities say it was the school's responsibility to check these credentials.
Our education expert, John Bear, says human resource departments around the country aren't doing their homework.
Patty Weiss: "What I'm astonished at, is the number of employers who don't check."
John Bear: "Isn't that amazing? That they don't for such an important thing?"
We wanted to know why it took so long for PCC to notice these questionable degrees.
They would only provide a statement, saying the college places a great deal of value on the credentials of its faculty. Adding, that the college has now strengthened the process to assess credentials before hiring and also conducts periodic audits.
And if you have a story for The Investigators, call our hotline at (520) 624-KVOA.
http://www.kvoa.com/global/story.asp?s=2578367&ClientType=Print/
 
Bandugu,
je, mmeweza kupitia hizi digrii na kuona uzito wa elimu aliyotoa Mwl. Julius Kambarage Nyerere chini ya Ujamaa?...Ebu tazameni elimu za hao wote mnaowazungumzia kabla ya hiyo PWU mtaona tamu ya Nyerere.
Wasomi wote hao wameanza vizuri sana chini ya Ujamaa lakini wameshindwa kupata digrii toka shule za maana baada ya Ujamaa kisha!.
Baada ya Ujamaa hata jangwa linazidi kusogea kusini mwa bara letu kwa kasi ya ajabu ndivyo elimu inavyopotea. Tumekata miti bila kupanda kwa tamaa ya fedha, leo tunamtukana Mungu kwa kutushushia balaa la jangwa!...sawa na elimu tumeivua wenyewe.
UDSM, IFM na Mzumbe vilikuwa vyuo baabu kubwa na wala hapakuwa na mjadala wa kipi zaidi kwani kila kimoja kilikuwa na ubora wa elimu yake ktk major fulani. Leo hii sintashangaa nikiambiwa kuna vijana wanamaliza UDSM, IFM au Mzumbe makabuntas!.. Lecturer wote wana miradi nje ya Kufundisha wengine wafanya biashara tena basi biashara hizo zimesajiliwa kisheria sasa kweli hapa kuna elimu imebaki?
 
Mzumbe University inaaibisha. Nakumbuka kuwa muda mfupi kabla sijaondoka Tanzania mwaka 1995, Chuo cha Ardhi kiliunganisha na UDSM. Wakati huo Vice Chancellor Luhanga alisema kuwa walimu wengi waliopo Ardhi Institute wanauwezo wa kutosha kufundisha watoto mambo yaliyoko vitabuni; lakini hawana nguvu ya kitaaluma ya kuweza kuchambua mambo mapya. Hivyo akatoa taarifa kuwa angependa wote waendelee na vibarua isipokuwa wathibitishe kuwa wanao ubavu kwa kusomea Ph.P. Nakumbuka kuwa aliyekuwa mkuu wa Chuo cha Ardhi wakati huo alikuwa profesa mmoja feki ambaye ilibidi avuliwe madaraka hayo na kutelemshwa kuwa Senior Lecturer. Walimu wengine wote walirudi kupitia tanuru upya na wengi wao walijipatia Ph.D zinazotambulika ingawa sielewi lililotokea kwa wale walioshindwa kupata legitimate Ph.D's.

Nadhania kuwa wakati Mzumbe inapandishwa kuwa Chuo Kikuu, ilitakiwa serikali ichague mtu ambaye ni academically credible kuongoza chuo hicho. Ni dhahiri kuwa mtu huyu angeweza kuweka standarad mpya. Lakini kitendo cha kumwacha Mr. Waryoba kama Vice Chancellor wakati yeye mwenyewe ni feki ilikuwa ni kosa kubwa sana. Najua kuwa kuna mwalimu Propser alishindwa kupata Ph.D Norway akaamua kununua Ph.D ya Commonwealth University na sasa hivi ni Lecturer hapo Mzumbe. Inaelekea hakuna mtu aliyemuuliza kulikoni ulikuwa Norway lakini unakuja na digrii kutoka visiwa vya Carribean.

Kuhus ubora wa wanafunzi nadhani kuwa swala hili huwa linakuwa overbloiw. Ninajua leverage ambayo wanafunzi wa mzumbe wamekuwa wakipta kutoka Serikalini kwa muda mrefu. Wakati Chuo hicho kinaanzihswa miaka ya 60 kilikuwa Chuo cha kusomesha kozi fupi fupi wafanya kazi wa serikali ambao hawakuwa na elimu ya kutosha katika taaluma ya fedha na uongozi. Watu hao baadaye walikuja kuchukua madaraka ya uongozi serikalini na kuacha trail ya kuwapendelea wanafunzi wanaotoka Mzumbe katika ajira, hasa kwa vile walitaka na wao wajiweke katika level ya University. Trail hii imeendelea huenda hadi leo hii; nafahamu kuwa wakati mimi ninasoma pale UDSM miaka ya themanini, jamaa wengi walioshindwa kuendela na masomo (disco) pale UDSM walihamia Mzumbe ambao walifaulu kupata advanced diploma zao na leo hii wana madaraka makubwa kwenye Idara mbali mbali za serikali. Je unadhani kuwa hawa jamaa watatoa maoni gani kuhusu kulinganisha wanafunzi wa Dar na wale wa Mzumbe? Ni dhahiri watasema Mzumbe ni bora; hii nidyo leverage ambayo ipo Mzumbe kwa muda merfu.

Baada ya hapo, bila kujali kuwa wanafunzi wakoje, kinachotakiwa ni kujenga nazingira mazuri ya kitaaluma kwa kuhakikisha kuwa chuo kina walimu wenye uwezo wa kutoa hoja kimataifa wakasikilizwa. Mimi sasa hivi nafindisha chuo kimoja ambacho kutokana na wingi wa wanafunzi, huwa tuna kodi walimu wanaoitwa "adjuncts" na vile vile tuna "full time lecturers". Ni watu wenye uwezo wa kufundisha mambo yaliyoko vitabuni na wanatusaidia sana katika kutayarisha undergraduates wetu. Lakini watu hawa hawahesabiki kama sehemu ya waalimu wa chuo, ingawa wana Ph.D nzuri tu zinazotambulika. Kwenye process ya accreditation hatuwahushi kabisa.

Ninachotaka kusema ni kuwa inelekea kuwa Mzumbe sasa hivi inafundishwa na watu wa level ya "adjuncts" or "full time lectures;" hakuna full time academics. Ingawa watu hawa wanaweza kufundisha undergraduate mambo ya kitabuni sawasawa, hawawajengi wanafunzi ngazi kuthink beyond the book, na hiyo ni sumu kwa taifa.
 
Wandugu, kwa majibu haya naogopa kwamba huyu Falsey hatarudi tena kwenye hii mada. Akirudi basi ana roho ngumu!
 
KICHUGUU na wenzako mbona fikira zenu ndogo?
DR.Warioba anaweka kampus Mbeya na Dsm, na muda mrefu sana ana program nzuri ya kusomesha walimu nje nani hafamu? na ni utaratibu wa kudumu, UDSM hakuna utaratibu huo hadi itokee commonwealth ndio mtu asome, Mzumbe haiishi kwa kubahatisha ina mipango mizuri ya kueleweka.
mfano mzuri huyo Dr.Assad wenu tunampambanisha na kijana mdogo sana Nyamsogoro ambaye amemaliza Mzumbe na alikuja na division one akaokota na cpa na akaenda UK nako akavunja rekodi na wanafunzi wote wanaokula dozi yake watakupa sifa zake hafanani kabisa na DR.wenu Assad(mbabaishaji) na ndio maana anapata muda wa kujadili Mzumbe wamekula nini, au DR.Warioba briefcase yake nyeusi, kifupi ana muda wa kuchezea,
na kama DR.Assad MJUAJI basi sasa bosi wake ni DR.Nchimbi(mzumbe product) najua yeye ni bodi member wa NSSF sasa kama anataka kuhoji uwezo wa wana mzumbe anatakuwa na mheshimiwa nchimbi tena dr.Nchimbi ana masters 2 na Phd. ndio maana JK akaona umuhimu wa DR. Nchimbi kwenda wizara ya kazi.
mimi nawaomba nyote kwa pamoja(Udsm) shughulikieni madawati kwanza kabla ya kuijadili Mzumbe,tumeona kwenye magazeti hivi karibuni wanafunzi wamekaa chini bila hata mkeka au jamvi wanakula lecture, uchoro huo huukuti MZUMBE UNIVERSITY, ndio maana hata uzushi waliouleta akina FIKIRADUNI kuwa ni chuo cha 13 hauingii akilini. chuo hakina vitabu,madawati nk kitawezaje kufanya vizuri?
DR.Warioba anakuiteni mkachukue madawati maana UDSM haina tofauti na shule za msingi za mbagara charambe watoto wanasoma chini, kweli UDSM wanafunzi wanasoma chini wataweza kuja kushindana na Mzumbe? jibu hapana ndio maana ajira zote Mzumbe inakomba, na huwezi kuona mwanafunzi wa Mzumbe anahangaika kutafuta CPA ni wale wa Udsm ndio inawachukua hadi miaka 8 sababu uwezo mdogo.
kama DR.Warioba hana sifa angeweza kuleta mijuiza hii ya ajabu? nadhani kama kuna WaTanzania wa kupewa Nobel basi ni mheshimiwa DR.Warioba (kiona mbali),
sasa hivi Mzumbe kuna kozi ya aina yake Bachelor of Accounting &Finance kwa mtaji huu soko la ajira tutazidi kukomba kila mwaka.
Mzumbeee oyeeeee, UDSM- Ziii!!!!.
hakimbii mtu hapa. uko FD?
 
Back
Top Bottom