Baada ya Ziara za Mawaziri mikoani je CCM na Serikali wamepata nini?

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Nimepata simu muda mfupi toka kwa Mzee mmoja mida hii na katika maongezi yetu kasema ziara za mawaziri wa JK katika kuelezea bajeti waliishia kuongea na madiwani kwa mikutano ya ndani maana wananchi walikuwa wakiwazomea kila kona ya Nchi . Je kwa wana CCM na wachambuzi wa mambo ya siasa na hasa wa serikali ya JK mna la kutueleza ? Is there anything achievement?
 
lunyungu,
kwanini mmenitolea option ya kupost new thread ktk profile yangu?au kwasababu mie ni kada mpinzani?
 
Hayo kuzomea ni staili imeingia mjini,itapita kama mishono ya nguo ,CCM wa kweli hatishiki na zomea zomea,hizo ni hasira tu lakini upendo wao uko pale pale CCM ndio Baba,hasira zina mida na halafu hutulia na mambo yakarudi kama zamani wanajua walokole hawa wa upinzani ni wapakazaji ,hucharuka halafu mwisho hurejea CCM.
 
Mwiba
Sitaki kuamini kwamba uko kilaza wa digrii hii . Yaani hujaelewa nilicho kiandika hadi unajibu kitu ambacho hakina nafasi wala hukuulizwa ? Narudia tena kuuliza .Je kuna mafanikio yeyote yaliyo patikana baada ya ziara hizo za mawaziri? Na landa niongeze moja mnaweza kutueleza kiais kimetumika na Faida ambayo Taifa limepata baada ya mizunguko hiyo ?

Uliyo kosa access ya kuweka new topic nasema itakuwa ni technical error halafu mimi si Admn.Ila najua ombi ama swali lako litakuwa limefika mahala husika .
 
Mkombozi weka hapa hapa ama weka kwenye mada ya Mbowe maana ni habari za mtu huyo huyo.Itakuwa vyema ukaendeleza pale pale
 
Tathmini yangu ni kuwa; ziara zimewapanua wananchi kidemokrasia. Mfano sasa wamefahamu kuhoji juu ya ahadi za viongozi si kosa na ni jukumu la Viongozi waliowachagua kuwajulisha mustakabali wa maendeleo yao. Wananchi kujitambua kulianza kuonekana katika ziara ya lowassa MWZ. Natumaini sote tunakumbuka maswali motomoto juu ya ajila na ahadi ya maisha bora kwa Wadanganyika. Na la kufumbua macho zaidi ni ujasiri wa mtoto kumhoji Waziri Mkuu. Natarajia kama ni tathmini ziara imetoa wigo wa kukomaza demokrasia.
 
Hayo kuzomea ni staili imeingia mjini,itapita kama mishono ya nguo ,CCM wa kweli hatishiki na zomea zomea,hizo ni hasira tu lakini upendo wao uko pale pale CCM ndio Baba,hasira zina mida na halafu hutulia na mambo yakarudi kama zamani wanajua walokole hawa wa upinzani ni wapakazaji ,hucharuka halafu mwisho hurejea CCM.

....hongera sana Mwiba, i hope you are making your papa CCM proud of your garbage.

you are an idiot.
 
ntareyehirungu
Junior Member
-----------------------------------------------------------------

Tathmini yangu ni kuwa; ziara zimewapanua wananchi kidemokrasia. Mfano sasa wamefahamu kuhoji juu ya ahadi za viongozi si kosa na ni jukumu la Viongozi waliowachagua kuwajulisha mustakabali wa maendeleo yao. Wananchi kujitambua kulianza kuonekana katika ziara ya lowassa MWZ. Natumaini sote tunakumbuka maswali motomoto juu ya ajila na ahadi ya maisha bora kwa Wadanganyika. Na la kufumbua macho zaidi ni ujasiri wa mtoto kumhoji Waziri Mkuu. Natarajia kama ni tathmini ziara imetoa wigo wa kukomaza demokrasia.


Ninasema siku zote kuwa we are making, a big progress ndani ya hii forum, kila siku kunakuja vichwa vingi vikali ambavyo vinaweza kuchambua ishus, I mean what else can you ask for?

Mkuu hapo juu, heshima zangu zote mbele, keep it up!
 
Back
Top Bottom