Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wakati vumbi la posho mbili kwa kazi moja halijatua sasa limeibuka tena suala la watumishi wa serikali kulipwa pensheni mbili Serikalini na kwenye Chama! Taarifa za uhakika zinataja orodha ndefu ya viongozi wa CCM ambao tayari wamepokea pensheni katika Chama na wanasubiri, au tayari wamepokea pensheni serikalini! Kwa mujibu wa taarifa, mbunge wa Mlalo Hassan Ngwilizi tayari amelipwa pensheni kwa "kukitumikia chama" chake katika kipindi hicho hicho ambacho alilipwa pensheni ya Bunge! Ngwilizi alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM. Pia Mbunge wa Handeni Dkt Abdallah Kigoda ambaye amepokea Pensheni Bungeni na Serikalini! Mbali na Pensheni Dkt Kigoda na Ngwilizi walikuwa wakilipwa na CCM posho ya Tsh 40,000 kila siku ambazo walikuwa DSM kwa hoja kwamba kituo cha Ngwilizi na Kigoda kilikuwa ni Dodoma kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa CCM! Balozi wa TZ nchini Urusi Jaka Mwambi amelipwa TSh 16,320,000 zikiwa pensheni kwa kuitumikia CCM tr 28 Novemba 2007 kwa hundi # 062332 ya CRDB! Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Aggrey Mwanry alilipwa Tsh 3.7m/- kwa hundi #062333 ya CRDB ikiwa ni pensheni ya CCM huku akilipwa pensheni ya Bunge! Rostam Aziz amelipwa TSh 3,520,000 tr 10 Desemba 2007 kwa hundi #062331 ya CRDB ikiwa ni pensheni ya utumishi wa NEC, Fedha na Uchumi. Wengine waliolipwa pia pensheni na Bunge ni Salome Mbatia, Omar Ramadhan Mapuri! (Source: MwanaHALISI, Nov 4-10, 2009, uk. 2).