Baada ya Mawaziri mafisadi kuwajibishwa anaefuata awe JK

Jan 16, 2007
721
176
Tofauti kati ya Rais wetu JK na viongozi wengi wa CCM,serikali na taasisi nyingine za serikali na umma wanatofautiana kwa majina matendo yao ni sawa ndiyo maana Rais JK alikua na kigugumizi kutoa maamuzi katika rushwa,ufujaji wa mali za umma na ufisadi.

Kwani kwa kufanya hivyo baada ya hapo tunahaki ya kuhoji uhalali wake kubakia katika kiti cha urais kwani ni yeye aliewateu na yeye ndiye amekua akiwalinda mbali na kelele nyingi za CHADEMA, wanaharakati na walalahoi .MH.RAIS NAWE UNAPASHWA KUJIPIMA NA KUTOA UAMUZI WA BUSARA KUACHIA NGAZI KABLA NAWE KUKULAZIMISHA KUFANYA HIVYO.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Mtoto akiwa mwizi siyo lazima na baba mzazi awe mwizi. Kuna mitoto mingine kama mikina maige na ngereja haisikii tusimuhukumu JK.
 
Unaupeuo mdogo wa mawazo. Rais sio nafasi ya ufundi cherehani au nafasi yoyote ile katika dunia, hivyo akimaliza miaka mitano wananchi hupiga tena kura kwa ridhaa yao. 2015 JK hatogombea tena atakuja mwingine kwa ridhaa ya wananchi. Acha kupotosha umma. tuna uhuru wa habari tusiiutumie vibaya.
 
Nani alisema baraza la mawaziri linavunjwa? Kinachokuja ni re-shuffle tu, wataotemwa hawazidi mawaziri watatu na manaibu waziri hawazidi watano, jumla wanane.
 
Unaupeuo mdogo wa mawazo. Rais sio nafasi ya ufundi cherehani au nafasi yoyote ile katika dunia, hivyo akimaliza miaka mitano wananchi hupiga tena kura kwa ridhaa yao. 2015 JK hatogombea tena atakuja mwingine kwa ridhaa ya wananchi. Acha kupotosha umma. tuna uhuru wa habari tusiiutumie vibaya.
Hili ndio tatizo la wabongo au wadanganyika wengi unyeupeo kama wako ya kua Rais hawezi kuwajibishwa.Nguvu ya umma inaweza kufanya awajibishwe.Madudu haya yote ambayo yamnafanyika ya ufisadi katika kila idara na taasisi za umma na serikali na ndani ya CCM "Kujivua gamba"Hakuna hatua anazozichukua mpaka kwa shinikizo la CHADEMA na baadhi ya wabunge wa CCM ambao wameisha ona ya kua nchi imemshinda.Hata hao wabunge wa CCM waliosinikiza wenzao watemwe badala ya kuchuakua hatua bado anaendelea kupata kigugumizi oh mara kuitisha kikao cha CC kupata ridhaa,je kwani alipowateua aliomba ridhaa na hao mawaziri mbali na haya yote wamegoma kujiuzulu wenyewe.Sababu kubwa ya kuwa na kiburi cha kufanya hivyo ni kwamba hawaoni tofauti kati wanayoyafanya wao na anayoyafanya yeye Mh.Rais JK na haya madudu wanayoyafanya watendaji wa chini yake ni kio cha Mh.Rais wetu JK.Sababu nyingine ambayo inamfanya kua na kigugumizi katika kutoa maamuzi ya kuwatimua viongozi wengi wabadhirifu(Mafisadi)Anaogopa wakifunguka na kuanza kusutana kwa kuna baadhi ya ufisadi ulipata baraka zake na swala lingine anaogopa baada ya kuwatimua baada ya shinikizo la vyama vya upinzani na baadhi ya wabunge wa CCM(Ambao najua wengi lakini wanaogopa vitisho)Wengi watahoji umakini wake na uwezo wake wa kutawala,ambapo nchi imepoteza rasilimali nyingi na wananchi kuendelea kuishi kwenye lindi la umasikini,hakuweza kuchukua hatua mpaka baada ya shinikizo.Inakua kana kwamba dereva wa gari amekaa kiti cha mbele haoni mashimo wala ajali vitu ambavyo wanaviona abiria waliokaa viti vya nyuma.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Back
Top Bottom