Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Mchungaji mmoja alikuwa akihubiri kanisani mara akamuona mama mmoja akilia kwa uchungu sana.Mchungaji akajua yule mama amechomwa na mahubiri yake,akazidi kuongeza dozi ya neno.Baada ya mahubiri mchungaji akamuita yule mama ashuhudie ni kipi kilichomfanya alie wakati wa mahubiri.Yule mama huku akiendelea kulia akasema;yaani mchungaji kila nikiziona hizo ndevu zako namkumbuka mbuzi wangu beberu aliyeibiwa,napata uchungu mno mpaka naishia kulia tu,ni hayo tu baba mchungaji.