Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,063
- 22,755
Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Peter Pinda jana alizindua kampeni ya kupiga kura kuwabaini wanaojihusisha na mauaji ya Albino na Vikongwe kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Zoezi hilo la kampeni ya upigaji kura litaigharimu kila kanda inayojumuisha mikoa mitatu Sh206 milioni ambazo zitatumika kwa ya ajili ya usafiri na uhamasishaji. Hapa naona kwa mbali watu wanaanza kujipanga mkao wa kula.
Inaniwia taabu kuamini kuwa serikali na vyombo vyake vya dola imeshindwa kupambana na wauaji hawa na sasa itajikita katika kupiga ramli. Bila shaka hiyo orodha itakapopatikana, kama kawaida atakabidhiwa mkuu wa kaya !! Mauaji ya Albino sasa yaelekea yataingizwa kwenye siasa maanake haiingii akili vyombo vya upelelezi vinavyolipwa na hela za walipa kodi vinashughulikia nini !!
Zoezi hilo la kampeni ya upigaji kura litaigharimu kila kanda inayojumuisha mikoa mitatu Sh206 milioni ambazo zitatumika kwa ya ajili ya usafiri na uhamasishaji. Hapa naona kwa mbali watu wanaanza kujipanga mkao wa kula.
Inaniwia taabu kuamini kuwa serikali na vyombo vyake vya dola imeshindwa kupambana na wauaji hawa na sasa itajikita katika kupiga ramli. Bila shaka hiyo orodha itakapopatikana, kama kawaida atakabidhiwa mkuu wa kaya !! Mauaji ya Albino sasa yaelekea yataingizwa kwenye siasa maanake haiingii akili vyombo vya upelelezi vinavyolipwa na hela za walipa kodi vinashughulikia nini !!