Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Mvutano mwingine umeibuka CUF baada ya Maalim Seif na wabunge kuweka nguvu kubwa katika uchaguzi wa kata ya Vijibweni na kuambulia nafasi ya tatu.
Baadhi ya viongozi wa chama hicho wamesema kwamba madai ya Hamad Rashid kuhusu Katibu Mkuu Maalim Seif kushindwa kukiwezesha chama kujijenga kupata ushindi yamethibitika kufuatia chama hicho ambacho ndicho kilichokuwa kinashikilia kiti hicho cha udiwani kupoteza kiti hicho na kushindwa hata kushika nafasi ya pili.
Katia uchaguzi huo chama kikongwe CCM kilifanikiwa kutetea kura zake kikifuatiwa kwa karibu na CHADEMA huku CUF ikishika nafasi ya tatu.
Viongozi hao wanalalamikia nguvu kubwa ya fedha na wabunge pamoja na katibu mkuu Maalim Seif ambaye pia ni makamu wa pili wa Rais yeye mwenyewe kuongoza kampeni katika kata hiyo na kushindwa.
Viongozi hao wanadai kwamba Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Julius Mtariro alitoa taarifa zisizokuwa za kweli kuhusu nguvu ya chama hicho katika kata hiyo hali ambayo ilifanya chama hicho kitumie fedha nyingi bila mafanikio.
....ndiyohiyo
Baadhi ya viongozi wa chama hicho wamesema kwamba madai ya Hamad Rashid kuhusu Katibu Mkuu Maalim Seif kushindwa kukiwezesha chama kujijenga kupata ushindi yamethibitika kufuatia chama hicho ambacho ndicho kilichokuwa kinashikilia kiti hicho cha udiwani kupoteza kiti hicho na kushindwa hata kushika nafasi ya pili.
Katia uchaguzi huo chama kikongwe CCM kilifanikiwa kutetea kura zake kikifuatiwa kwa karibu na CHADEMA huku CUF ikishika nafasi ya tatu.
Viongozi hao wanalalamikia nguvu kubwa ya fedha na wabunge pamoja na katibu mkuu Maalim Seif ambaye pia ni makamu wa pili wa Rais yeye mwenyewe kuongoza kampeni katika kata hiyo na kushindwa.
Viongozi hao wanadai kwamba Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Julius Mtariro alitoa taarifa zisizokuwa za kweli kuhusu nguvu ya chama hicho katika kata hiyo hali ambayo ilifanya chama hicho kitumie fedha nyingi bila mafanikio.
....ndiyohiyo