Baada ya kusakamwa: EOTF wazinduka.

Mabbyjr

Member
Aug 19, 2007
29
1
Wananchi wengi wamekuwa wakihoji kulikoni EOTF (Ile NGO iliyo chini ya Mama Mkapa). Tangu Fisadi Mkapa amalize kipindi chake cha uongozi na kuanza kusakamwa na balaa la UFISADI, hii taasisi ilikuwa kimya kupita kiasi. Watu walianza kujiuliza kama na yenyewe itakuwa imemaliza kipindi chake cha kuwa active na Social activities baada ya Mkapa kumaliza kipindi chake. Hata hapa JF watu wamekuwa wakielekeza maswali kwa huo Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote lakini hakuna hata kiongozi mmoja kutoka mfuko alijitokeza kuzungumzia hilo. Hivyo mie nilihisi labda huo Mfuko umehamishiwa kwenye Miradi ya Fisadi Mkapa /Mr. Clean (Mawazoni)/ ambayo hataki kuizungumzia.

Sasa OETF imezinduka na kuja na hili hapa chini.....


Mfuko wa fursa sawa kwa wote - EOTF kwa kushirikiana na ustawi wa jamii umefungua kituo cha kusaidia watoto yatima kupata elimu kutokana na watoto hao kukosa fursa hiyo muhimu.

Akiongea na ITV katika kituo hicho kilichopo Ilala jijini, kaimu mkurugenzi mtendaji wa EOTF Bwana Steven Emmanuel amesema kuwa mbali na kuanzisha kituo hicho taasisi hiyo imejiwekea utaratibu wa kila ijumaa kufanya kazi mbalimbali za kijumuiya.

Kwa upande wake meneja mradi wa EOTF amesema kuwa wao kama taasisi inayojihusisha na masuala ya kusaidia makundi ya aina mbalimbali katika jamii wamehamasika kuanzisha mradi wa yatima kutokana na kundi hilo kutopewa uzito zaidi katika miradi iliyotangulia.

Source: ITV
 
MIRADI YA FIRST LADIES....
Naipenda Tanzania kwa ubunifu ktk sekta ya ugugunaji fedha za umma.....
 
atleast they are doin something for the community!!!

Noooo! Mtaalam...They are pretending that they are doing something for the community, but in reality they are the one who benefit the most and not the community.
 
bubu dats why i said "SOMETHING"!!!!!i hope we ol know the meaning ya hilo neno!!
 
Taasisi hii ilipashwa ibadili jina na kujiita fursa sawa kwa wachache.Mfuko huu umewahi kutoa fursa yo yote huko Tunduru,kibondo na pembezoni kwingine achia mbali Kilimanjaro na Dsm,nisaidieni jamani wenye data,nisije nikawalaumu bure.

Kuna watu mikoani wamekosa fursa jamani,achani mchezo.
 
Back
Top Bottom