Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Habari zilizothibitishwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Ngeleja zinasema kuwa tatizo la umeme lililoikumba nchi muda mfupi uliopita linatokana na matatizo ya kiufndi kwenye gridi ya taifa na juhudi zinaendelea wakati huu kuhakikisha kuwa hali inatengemaa kabla ya kupambazuka.
Akizungumza nami muda mfupi uliopita Waziri Ngeleja amesema kuwa matatizo kama haya huwa yanaweza kutokea na kwa vile ni ya kiufundi zaidi basi yanahitaji umakini wa hali ya juu kuyatatua na amewahakikishia wananchi kuwa juhudi zote zinafanywa ili kurejesha hali katika hali ya kawaida.
"Siyo tatizo la sehemu sehemu tu, ni tatizo la system nzima ya gridi yetu na mafundi wetu wako kazini sasa hivi kurejesha hali katika hali ya kawaida" amesema Bw. Ngeleja.
Wakati huo huo nilitumia muda huo kumpa pongezi kwa jinsi alivyosimamia suala la Kakobe na Nguzo za umeme na hatimaye kuifanya serikali ichukue msimamo badala ya kuyumbishwa kirahisi. Nilimhakikishia kuwa Watanzania wanataka kuona serikali yao inachukua maamuzi badala ya vikao visivyoisha hasa kwenye mambo ambayo uamuzi unahitajika haraka.
Akizungumza nami muda mfupi uliopita Waziri Ngeleja amesema kuwa matatizo kama haya huwa yanaweza kutokea na kwa vile ni ya kiufundi zaidi basi yanahitaji umakini wa hali ya juu kuyatatua na amewahakikishia wananchi kuwa juhudi zote zinafanywa ili kurejesha hali katika hali ya kawaida.
"Siyo tatizo la sehemu sehemu tu, ni tatizo la system nzima ya gridi yetu na mafundi wetu wako kazini sasa hivi kurejesha hali katika hali ya kawaida" amesema Bw. Ngeleja.
Wakati huo huo nilitumia muda huo kumpa pongezi kwa jinsi alivyosimamia suala la Kakobe na Nguzo za umeme na hatimaye kuifanya serikali ichukue msimamo badala ya kuyumbishwa kirahisi. Nilimhakikishia kuwa Watanzania wanataka kuona serikali yao inachukua maamuzi badala ya vikao visivyoisha hasa kwenye mambo ambayo uamuzi unahitajika haraka.