Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,479
- 30,144
Tumemsikia Rais wetu akilihutubia Taifa mwisho wa mwezi, kupitia vyombo vya habari vya Televisheni na redio, katika utaratibu aliojiwekea yeye mwenyewe. Baada ya kumsikiliza, tulivyomuelewa ni kama vile anaona hakuna makosa yoyote ya polisi katika mauaji ya raia wasio na hatia, katika matukio mbalimbali yaliyotokea siku za karibuni, hususani katika mikutano ya kisiasa. Akahalalisha matumizi hayo kwa madai kuwa Jeshi la polisi linatimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria za nchi yetu. Kutokana na maelezo ya Rais, sasa ndiyo tumepata jawabu, kwa nini Kamanda Kamuhanda alitamba kwenye vyombo vya habari kuwa hawezi kujiuzulu kutokana na tukio la kuuawa kwa mwandishi wa habari Daudi Mwangosi. Tumepata tafsiri pia kuwa ingawa 'OPERESHENI UA MWANGOSI' iliratibiwa na kuongozwa na Kamuhanda, lakini katika hali halisi, operesheni hiyo, ilikuwa na baraka zote za mkuu wa nchi!! Na ndiyo maana pamoja na wananchi wengi, baada ya kuziona zile picha za mauaji ya Mwangosi, walihoji sana, kwanini kamanda Kamuhanda na wenzake akina Shilogile, Chagonja na Mwema, wasiwajibike kwa matokeo hayo. Lakini wakuu hao wa polisi, walitulia kimya kabisa, na hadi kufikia hizo tambo za huyo Kamuhanda, ambaye anaeleza wazi kuwa yeye hawezi kujiuzulu ng'o!! Kwa maana hiyo kwa mazingira hayo, sioni hata maana ya pesa za walipa kodi kutumika ovyo kwa kuunda Tume za uchunguzi za akina IGP na Mwema, ambazo matokeo yake yanajulikana wazi kuwa yatawasafisha wauaji!! kwa kuwa ni dhahiri Tume hizo haziwezi kutoa taarifa kinyume na matamshi yaliyotolewa na mkuu wa nchi kuwa mauaji hayo yalibidi, kwa kuwa Jeshi la polisi lilikuwa linatekeleza wajibu wake wa kisheria!! Baada ya kufanya tathmini hiyo, nadhani ni wajibu wetu watanzania kuangalia what is the next step. Kwa maoni yangu kwa kuwa picha za mauaji, hasa katika tukio la Mwangosi zipo, na kwa kuwa ipo wazi kuwa hata huyo corporal Simion, aliyeburuzwa mahakamani ni geresha tu ya watawala, ambapo hatimaye hata yeye naye ataachiwa huru. Sasa naamini ni wajibu wa wanasheria wetu wazalendo,pamoja na wanaharakati na wenye uzalendo wa hali ya juu, kuziangalia sheria zetu, kama kutakuwa na uwezekano wa masuala haya ya mauaji wa makusudi wa raia wasio na hatia, kuweza kuyafikisha kwenye mahakama ya kimataifa ya the Hague. Nasema hivyo kwa kuwa kwa ushahidi usio na shaka yoyote, kwa sasa mtuhumiwa namba moja wa mauaji ya raia wasio na hatia ni yeye mwenyewe Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete. Kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa, hakuna uwezekano wowote wa Rais wetu, kumburuza mahakamani,wakati huu ambapo yupo madarakani, na hata hapo atakapoachia madaraka na kumkabidhi Rais wa awamu ya tano!! Kwa maana hiyo wadau mliobobea kwenye sheria, na wadau wengine wanaharakati, tuchangie mada hii, tuangalie namna gani tunaweza kuwafikisha wauaji wa raia wasio na hatia kwenye vyombo vya sheria, ambapo kwenye sheria za nchi yetu, zinawapa ulinzi wa hali ya juu kabisa, pamoja na Katiba hiyo hiyo kutamka wazi kuwa wananchi wote wapo sawa mbele ya sheria!!!