Hi JF, Serikali baada ya kupandisha bill ya umeme kwa 18% sasa nimeona wizara ya maliasili imetangaza kuchukua ushuru kwa watumiaji wa mkaa. Tangazo ambalo limetolewa kupitia star tv kuwa watakatisha ushuru kwa watumiaji wa mkaa wote hata kama ni wa kutumia nyumbani kama utakuwa hujakatia ushuru mkaa utataifishwa na mhusika kushtakiwa. Wameona wakiwakamua watumiaji wa umeme tu haitoshi sasa wanarudi hadi kwa walala hoi. Mi sìilewi hii serikali ya awamu ya nne inawatakia nini raia wa tz. Sasa wanataka hata kula tusile ili tufe na njaa. Bado kidogo watakatisha ushuru wa kuni za majumbani. Wanahakikisha wanatukamua hadi tukome. Mi ni mgen kama kunamahali nimekosea naomba nielekezwe. Naomba kuwasilisha.