Azimio la Arusha liko wapi jamani? walaaniwe walioliua!

MNYISANZU

JF-Expert Member
Oct 21, 2011
7,048
1,102
Hakuna kipindi kama hiki ktk historia ya Tanzania ambapo "AZIMIO LA ARUSHA" lilikuwa linahitajika sana!. Kwa sasa Azimio la Arusha lilikuwa linahitajika katika kutumika kama mwarobaini wa kudhibiti ufisadi uliotamalaki kila mahali [ rejea nyongeza ya posho za wabunge, mishahara na posho wanazolipana maofisa wa ngazi za juu BOT, TRA,NSSF na mashirika/taasisi zingine za umma]. Kushuka kwa uwajibikaji miongoni mwa viongozi na watumishi wa ngazi za juu, kupuuzwa kwa professions zingine kama madaktari,walimu,polisi,etc ni kielelezo kingine kinachoonyesha kuwa Azimio la Arusha lilkuwa bado relevant na linahitajika. Kila siku huwa najiuliza ni akina nani haswa walioliuwa hili Azimio? na kwanini hawakulifanyia marekebisho tu pale panapohitajika kufanya hivyo? . Mwisho kabisa walaaniwe wale wote ambao kwa namna moja au nyingine walishiriki kuliua hili Azimio.
 
Huoni kama lile Azimio ndio lililopelekea watu wa nchi hii wakafikia hapa tulipo?
 
Huoni kama lile Azimio ndio lililopelekea watu wa nchi hii wakafikia hapa tulipo?
Azimio hili lilkuwa limecontain rules mbalimbali ambazo zilikuwa ni mwiba kwa mafisadi na ufisadi. Kama lilikuwa na weakness zake kwa nini hawakulifanyia ammendments tu ili liendane na wakati na mazingira
na badala yake wakaliua? Mbona hao ni mabingwa wa kuitia viraka katiba?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom