Rutunga M
JF-Expert Member
- Mar 16, 2009
- 1,769
- 1,382
Wakuu
mwanamuzi Ambwene Yesaya (AY) usiku wa kuamkia jana alinusurika kifo kufuatia mashabiki kuvamia katika guest alikokuwa amefikia katika wilaya ya karagwe mkoani kagera wakishinikza kurudishiwa fedha zao walizotozwa kama kiingilio na kisha kutoonekana ukumbini.
Full tukio ni hivi.
AY aliletwa na mwanamama Dina ili ashiriki katika onesho la mavazi liloandaliwa na kampuni ya Dina Fashion ya jijini Dar na alitakiwa kufanya maonesho mawili katika miji ya Bukoba na Karagwe kwa malipo ambayo hayajajulikana.
Hata hivyo inadaiwa kuwa baada ya kufanya onesho pale ukumbi la Linas Club Mjini Bukoba alilipwa ujira nusu na kuahidiwa kuwa angelipwa fedha zilizosalia baada ya kufika Karagwe lakini waandaaji walishindwa kufanya hivyo.
Kutokana na hilo AY aligoma kutoka hoteli alikokuwa amefikia ili aende kupanda jukwaani hali iliyowafanya mashabiki kulalama na kuamua kumfuata hotelini hapo na kwa lengo la kumdhuru kabla ya kukolewa na polisi.
Baada ya hapo, polisi walimchukua AY, waandaaji na baadhi ya washiriki wa mavazi waliokuwa wametoka Bukoba na kuwasweka LUPANGO katika kituo cha Polisi Karagwe ambapo walilala hadi jana asubuhi.
Taarifa za hivi punde ni kuwa AY na waandaaji wa shindano hilo ameachiwa baada ya kuelewana lakini mashabiki WAMETAPELIWA.
SASA SIJUI ALAUMIWE, AY, DINA FASHION AU MASHABIKI ? Kazi kwenu
mwanamuzi Ambwene Yesaya (AY) usiku wa kuamkia jana alinusurika kifo kufuatia mashabiki kuvamia katika guest alikokuwa amefikia katika wilaya ya karagwe mkoani kagera wakishinikza kurudishiwa fedha zao walizotozwa kama kiingilio na kisha kutoonekana ukumbini.
Full tukio ni hivi.
AY aliletwa na mwanamama Dina ili ashiriki katika onesho la mavazi liloandaliwa na kampuni ya Dina Fashion ya jijini Dar na alitakiwa kufanya maonesho mawili katika miji ya Bukoba na Karagwe kwa malipo ambayo hayajajulikana.
Hata hivyo inadaiwa kuwa baada ya kufanya onesho pale ukumbi la Linas Club Mjini Bukoba alilipwa ujira nusu na kuahidiwa kuwa angelipwa fedha zilizosalia baada ya kufika Karagwe lakini waandaaji walishindwa kufanya hivyo.
Kutokana na hilo AY aligoma kutoka hoteli alikokuwa amefikia ili aende kupanda jukwaani hali iliyowafanya mashabiki kulalama na kuamua kumfuata hotelini hapo na kwa lengo la kumdhuru kabla ya kukolewa na polisi.
Baada ya hapo, polisi walimchukua AY, waandaaji na baadhi ya washiriki wa mavazi waliokuwa wametoka Bukoba na kuwasweka LUPANGO katika kituo cha Polisi Karagwe ambapo walilala hadi jana asubuhi.
Taarifa za hivi punde ni kuwa AY na waandaaji wa shindano hilo ameachiwa baada ya kuelewana lakini mashabiki WAMETAPELIWA.
SASA SIJUI ALAUMIWE, AY, DINA FASHION AU MASHABIKI ? Kazi kwenu