Awamu nne, yupi bora?

Haiwezekani! Tanzania ni nchi maarufu sana Afrika. Na umaarufu huo hautokani na jina la nchi kuwa zuri, bali utendaji wa marais wake pamoja na timu yake.

Hivi sasa ni miaka zaidi ya 40 toka tupate uhuru, Tanzania bado ni kioo na mfano kwa Afrika licha ya umasikini wetu. Kwani umasikini ni bahari ya Afrika nzima.

Kwahiyo sikubaliani nawe pale unaposema hayupo bado. Basi angalau ungesema ni yupi aliyekuwa afadhali, maana hata katika wajinga kuna kiongozi ambaye anaonekana kuwa mzuri kuliko wengine.


Nahisi bora ungewauliza hao wanaowaona umaarufu wa Tanzania kwa walio nje ya nchi kuwa kigezo cha ubora ama kwa sisi tunaotaka maendeleo iwe kipimo "tunasema Hayupo"
 
Chaguaenin wenyewe
1. Aliyeleta mshikamano na kuua ukabila na kuleta ujamaa
2. Aliyeuza mbuga za wanyama kwa waarabu na kuruhusu uchumi holela
3. Aliyeuza machimbo ya madini na ardhi kwa bei chee
4. Umeme wa IPTL unawaka lini jamani Uuuwwiiiiiiiiiiiiii!! Uuuwwiiii



Mkuu naomba nikuengezee nukta katika hoja zako
1. ............... na kuviza demokrasia na baadae kuiacha nchi katika njaa na uduni wa kila hali
2. ..............ingawa yeye alifungua milango ya demokrasia na kutufanya tuwe na mipango ya kujinasua na njaa na uduni mwengine.
 
Chaguo langu la kwanza ni nyerere kwa sababu zifuatazo:
1 Elimu yetu ilikuwa bora,
2 Madawa yalikuwa yanapatikana mahospitalini,
3 Kulikuwa na mshikamano wa taifa
4. Aliweza kufuta kutojua kusoma na kuandika
5 Wakati anapata uongozi palikuwa kuna wasomi wacheche sana alipigania watu wasome angalau wapatikane wasomi wa kuendesha ofisi na mambo mengine
6 kulikuwa na maendeleo ya viwanda: kusindika vyakuka, nguo nk

ukiangalia yote hayo kwa kipindi chake cha urais alikumbana na matatizo mengi kuliko mafanikio, fikiria vita vya idd amini vilimaliza pesa kiasi gani?
pia alitufundisha kujitegemea.

hebu angalia sasa hivi hivi tulivyogeuziwa vibao kila kitu ni kuomba msaada, angalia raisi wetu wa sasa anavyokata mbuga kuomba misaada, kila sehemu watu wanaomba misaada. hebu fikiria hiyo misaada itatupeleka wapi? wakati anayetoa nae bado anatafuta. angalia china wanavyoendela.

Una maana kuwa hayo mazuri yalikuwepo wakati Nyerere akijiuzulu?
Kwa fikira zangu kwa vile msingi ulikuwa mzuri basi tungekuwa mbele kimaendeleo na sio kufilisika kiasi cha kumfanya Rais wa nchi aamuwe "kungatuka"
Ninachofikiri mimi ni kuwa hayo mambo unayoyataja yalikufa wakati wa Nyerere na hivyo aliefuatia alibidi aanzishe misingi mipya ambayo Maraias wengine wawili waliofuata wanayaendeleza.
 
Haiwezekani! Tanzania ni nchi maarufu sana Afrika. Na umaarufu huo hautokani na jina la nchi kuwa zuri, bali utendaji wa marais wake pamoja na timu yake.

Hivi sasa ni miaka zaidi ya 40 toka tupate uhuru, Tanzania bado ni kioo na mfano kwa Afrika licha ya umasikini wetu. Kwani umasikini ni bahari ya Afrika nzima.

Kwahiyo sikubaliani nawe pale unaposema hayupo bado. Basi angalau ungesema ni yupi aliyekuwa afadhali, maana hata katika wajinga kuna kiongozi ambaye anaonekana kuwa mzuri kuliko wengine.

You are comparing presidents of different era, roles, developments, people etc.

Nyerere aliweka misingi mibovu, from structural engineering standponts makes all other sequel structural components to be weka, and not reliable.

Akina Mwinyi, JK, MKapa, wameshindwa kurudi nyumna na kuiweka sawa misingi mibovu ya Nyerere nao wakawa wanaelea tu,

Ni aibu Zawadi kufikiria nchi hii imeshwahi kuwa na rais;unless kama haujui matatizo ya Tanzania na watanzania

so hakuna
'zidumu fikra sahihi za mweyekiti wa chama'
 
Duhhhh

kweli watanzania hatuna shukurani.....

Hakuna rais kama mwinyi na hatutakuja kumpata rais kama mwinyi...

Kwanza hakutaka kuwa rais..
Halafu alikuta nchi mbovu kupita maelezo

sukari kwa foleni,ukikutwa na sabuni za zambia tu unakamatwa kwa uhujumu uchumi,,,,
nchi nzima watu wanavaa matambara yanayofanana,,,,,
na kandambili za matairi

vitongoji kama sinza na mbezi beach havikuwepo......kulikuwa mashamba tu.

Duh pamoja na yote hayo alitukanwa kuliko rais yeyote yule....yaani,
 
Duhhhh

kweli watanzania hatuna shukurani.....

Hakuna rais kama mwinyi na hatutakuja kumpata rais kama mwinyi...

Kwanza hakutaka kuwa rais..
Halafu alikuta nchi mbovu kupita maelezo

sukari kwa foleni,ukikutwa na sabuni za zambia tu unakamatwa kwa uhujumu uchumi,,,,
nchi nzima watu wanavaa matambara yanayofanana,,,,,
na kandambili za matairi

vitongoji kama sinza na mbezi beach havikuwepo......kulikuwa mashamba tu.

Duh pamoja na yote hayo alitukanwa kuliko rais yeyote yule....yaani,
Usisahau pia huyu ndiye alikuwa rais wa kwanza kuanzisha biashara Ikulu.
Mkewe alituletea sisi walevi bia za Stella Artois, na majenereta, huku bwana mkubwa akipokea vibahasha vilivyojazana na vijisenti kutoka kwa mashemeji zake Wahindi.
 
usisahau pia huyu ndiye alikuwa rais wa kwanza kuanzisha biashara ikulu.
Mkewe alituletea sisi walevi bia za stella artois, na majenereta, huku bwana mkubwa akipokea vibahasha vilivyojazana na vijisenti kutoka kwa mashemeji zake wahindi.

hizo zote redio mbao tu.hakuna kilichothibitishwa.....

Kwani mkewe akikuuzia majenereta.....bila kuzuia mwingine kuuza majenereta

wewe unaumia wapi?

Mwinyi aliwasitiri watanzania kwa mengi...
Enzi zake hata udiwani watu walikuwa hawagombei kwa sababu watu walikuwa hawana njaa.
 
pia gundueni hamna binadam 100 clean, hata huyo mnaemsifu sana Obama, bado anaongoza wanajeshi Afghanstan na bado anatamani resources Africa...............hamna rais ambaye JF mnamtaka atatokea dunia hii hakuna, hata akiwa dr slaa atakua namapunguvu chungu nzima...Zuma na kupendwa kwake SA anaipata fresh sasa maandamano chungunzima kule SA
 
Hivi sasa ni miaka zaidi ya 40 toka tupate uhuru, Tanzania bado ni kioo na mfano kwa Afrika licha ya umasikini wetu. Kwani umasikini ni bahari ya Afrika nzima.

Kama nchi ni maskini miaka 40 baada ya uhuru, haiwezi kuwa kioo na Mfano Afrika. Hatuchagui viongozi kutupa umaskini, Umaskini umeletwa na uongozi mbovu iliopo asante kwa kujibu mwenyewe suali lako.
 
Tanzania imeshatawaliwa na marais wanne tofauti, maarufu kwa jina la awamu nne. Akianza J.K. Nyerere, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Che Mkapa na J.K. Mrisho.

Kwanza, kabla sijaendelea tuangalie muujiza mkubwa kabisa uliojitokeza kati ya awamu ya kwanza na ya nne. Angalia kwa makini majina hayo, J.K yanalingana. Na hii si bahati mbaya, bali iltabiriwa na Kinjeketile mwaka 1903 kabla ya kuanza vita vya maji maji. Lakini nini maana ya kushabihiana huko. Hili ni swali ninalowaachia wasomaji.

Kwa bahati nzuri mimi nimepata sababu moja wanayoshabihiana, nayo ni kupata umaarufu sana kwa watu wa ndani na nje. Pili kushika madaraka wakiwa vijana. Uchumi je? Sitii pua yangu huu ni uwanja wenu.

Ali Hassan Mwinyi na Mkapa. Hawa nao wana sifa moja inayoshabihiana, kuwa ni maraisi waliopata urais bila wananchi kuwadhania kuwa wangekuwemo katika jopo la wagombea Urais. Ya mwisho lakini si ndogo, wote huacha mouth touch.

Lakini yote tisa kumi, yupi ni mbora kuliko wote kama rais wa nchi? Tupe data zako za kina na toa ushadi tosha. Ni hoja makini tu ndizo zitazohesabiwa.

Mi nadhani Majina ya Nyerere na Kikwete hayafanani kwa sababu nyerere ni Julius Kambarage Nyerere yaani J.K.N na Kikwete ni Jakaya Mrisho Kikwete yaani J.M.K sasa u J.K. uko wapi? Naomba mnifafanulie! Ladda ingelikuwa ni Jakaya Kikwete Mrisho labda U J.K. ungeleta maana!
 
Sidhani kama kuna sababu yeyote ya kung'ang'ania kuwaweka katika mzani hawa jamaa waliopata kuishi ndani ya ikulu yetu....

La muhimu, wao na washauri wao, na watendaji wao wametuleta mpaka hapa tulipo - je tunaridhika na tulipofikia? Kama haturidhiki, tukae na kufikiri tufanye nini ili tufike kule tulinakokusudi kufika.

Kujadili watu kunaweza kuwa bora iwapo tu, tutachukua mema yao na kujenga juu yake na yale maovu yao tusiyaige bali tuyaondoe kabisa katika jamii yetu!!!

Tusimame watanzania tulete mabadiliko..

Napatikana (facebook: mtanzania halisi, pia nina forum: chini ya mti:chiniyamti.ning.com)

Karibuni...
 
Zawadi;

Sidhani kama umekuwa fair kulinganisha zama tofauti bila kuweka vigezo sawia!! Pia naamini kiongozi bora ni yule achukuaye maamuzi na kusimama nayo hata kama yanaweza yasimpe sifa kwani ndio uongozi wenyewe, sticking to the strategy until proven fruitless... so far in Tanzania we have had only one president who could do that, Huyo ni Nyerere, period!!!

  • Mkapa alijaribu lakini alizungukwa na awapendao na hata baada ya kujua alimezea [its not good]
  • Mwinyi --- sina la kusema
  • JK --- sikumbuki lini amesimama upande mmoja wa shilingi, kila siku anaplay safe kama mzani [he is libra anyway]
Sioni tatizo kulinganisha marais wa zama tofauti. Ninasababu ya kusema hivi, tena sababu nzito sana. Ninafikiri wote mtakubaliana.

Sababu kubwa na nzito, ni kwa vile barabara ya kutoka Tripoli (Libya) mpaka Johanesburg (A. Kusini) haijengwi katika ERA moja. Cha msingi ni kuanza ujenzi wa barabara hiyo. Tunaweza tukaunganisha kwanza kati ya nchi hadi nchi mpaka zikaja ungana Kampala. Na hii inaweza kuchukua rais baada ya raisi, awamu baada ya awamu na ERA baada ya ERA.

Basi maendeleo ya nchi nayo huenda katika nyayo hizo hizo, sekta baada ya sekta na kadhalika. Kwa hiyo la msingi katika mnyororo huo ni kuangalia ni nani katika ERA yake alifanya vizuri zaidi na kulisukuma gurudumu la maendeleo lenye msingi imara. Na hiki ndio kigezo muhimu katika kulinganisha hao maraisi.

Ulinganishaji wa marais katika ERA tofauti upo pahala pote Duniani. Kwa mfano, Marekani huwambii lolote juu ya Abraham Linkoln. Maksi zake ni za juu kabisa. Halikadhalika katika Soka. Mpaka leo wataalam wa soka wanajaribu kuwalinganisha wachezaji tofauti na Pele. Na wengi wanakubali kuwa bado kiwango cha pele kilikuwa ni kikubwa sana.

Kwa hiyo nawatoa wasiwasi wale wote wanaodhani kuwa Julius ceasa hawezi kulinganishwa na Bush. Au ujenzi wa piramid, Misri hawawezi kulinganishwa na mjenzi wa Kitega uchumi TZ. Na kwa maana hiyo ni sawa kabisa kuwalinganisha marais wa awamu zote nne na tukampata mbora zaidi au mshindi.

Iangalieni Tanzania vizuri katika awamu zote nne na mtoe majibu makini ili tujifunze nayo.
 
Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamewahi kutoa majibu ya hili swala na naamini hayo majibu yalitoka mioyoni mwao. Kuna wakati ambapo jina Tanzania lilikuwa la heshima na la kujivunia na waliokuwapo enzi hizo ni mashahidi. Kuna wakati Tanzania ilitazamwa kwa macho ya husuda na majirani zake na msimamo wake kwa maswali mbali mbali uliheshimiwa. Hivi sasa jina Tanzania linahusishwa kwa namna fulani na nchi ya mataahira na ni aibu wakati mwingine kujitambulisha hivyo.
Tanzania imewahi kuwa Maraisi wa aina nne tofauti kabisa na wenye misimamo na uwezo tofauti kabisa.

1. Mwenye nguvu, mvuto na mpiganaji ambaye yuko tayari kuutetea msimamo wake kwa nguvu ya hoja - Uraisi aliupigania mwenyewe.
2. Yupo yupo na mpole asiyejua jukumu la kiongozi wa nchi wala heshima inayoendana nayo, kila kitu rukhsa - Uraisi aliukwaa kama ngekewa.
3. Asiye na mvuto lakini hutumia nguvu kutetea hoja na kusimamia malengo hata kama hayana manufaa kwa taifa - Uraisi alipakatwa.
4. Asiyejua kwa nini aliutaka Uraisi ni kama mtoto anayelilia wembe na akapewa ! Uraisi wake ni feki - anachezeshwa kama "puppet"
 
Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamewahi kutoa majibu ya hili swala na naamini hayo majibu yalitoka mioyoni mwao. Kuna wakati ambapo jina Tanzania lilikuwa la heshima na la kujivunia na waliokuwapo enzi hizo ni mashahidi. Kuna wakati Tanzania ilitazamwa kwa macho ya husuda na majirani zake na msimamo wake kwa maswali mbali mbali uliheshimiwa. Hivi sasa jina Tanzania linahusishwa kwa namna fulani na nchi ya mataahira na ni aibu wakati mwingine kujitambulisha hivyo.
Tanzania imewahi kuwa Maraisi wa aina nne tofauti kabisa na wenye misimamo na uwezo tofauti kabisa.

1. Mwenye nguvu, mvuto na mpiganaji ambaye yuko tayari kuutetea msimamo wake kwa nguvu ya hoja - Uraisi aliupigania mwenyewe.
2. Yupo yupo na mpole asiyejua jukumu la kiongozi wa nchi wala heshima inayoendana nayo, kila kitu rukhsa - Uraisi aliukwaa kama ngekewa.
3. Asiye na mvuto lakini hutumia nguvu kutetea hoja na kusimamia malengo hata kama hayana manufaa kwa taifa - Uraisi alipakatwa.
4. Asiyejua kwa nini aliutaka Uraisi ni kama mtoto anayelilia wembe na akapewa ! Uraisi wake ni feki - anachezeshwa kama "puppet"
Uchambuzi wako umekuwa wa kina sana na wenye hoja mahsusi. Lakini tukizichambua hizo hoja No1 hadi 4, zinaweza kuzaa hoja kubwa nyingine. Na kwa maana hiyo zinaweza kupata upinzani na kuungwa mkono kwa wkati mmoja.

Hoja namba 2, Yupo yupo na mpole ambaye ni Mwinyi. Kumbuka ndiye aliyesimamia mabadiliko toka ujamaa mpaka ubepari. Utaifishaji ndio ilikuwa kazi kubwa mno. Na hapa si utaifishaji tu, bali kubadilisha vichwa (idiolojia ) ya watanzania 35 mil. idiolojia ikiwa pamoja na ueleo wa maneno kinyume nyume, badala ya Mnyonyaji tumwite Muwekezaji, Nyapara mpaka kiongozi au msimamizi n.k. Kazi hii si rahisi, na aliifanya akiwa na upinzani mkali wa wafuasi wa Nyerere. Waziri hatekelezi agizo lolote la rais mpaka akaulize Butiama.

Tunaweza tukamwita mpole, lakini kama angekuwa mkali sana na mwenye kushikilia misimamo yake, Tanzania ingeweza kuingia katika vita. Maana tamaa ya mzee kifimbo katika uongozi ilikuwa kubwa kuliko tulivyofikiria, hasa ukizingatia umaarufu wake nchini. Kuwa Mzee haambiliki alikuwa alikuwa akiongoza awmu ya 2 kwa distance control, sio siri kwa watanzania wote. Jaribu kuwa katika hali hiyo mwenyewe, kuwa wewe ni bosi lakini umbo tu mwendeshaji ni mwingine. Kwa upande wangu Mwinyi alikuwa smart sana, kutawala serikali na serikali ndani ya serikali na bado tukapata amani. Uwezo huo wanao wachache sana, na ni viongozi wale walioweka maslahi ya Taifa mbele ndio wanaweza kufanya hivyo japo ya kuwa na jeshi.

Namba 3, hutumia nguvu kutetea hoja na kusimamia malengo hata kama hayana manufaa kwa taifa - Uraisi alipakatwa. Hapa umepatia, na ninakuunga mkono. Tumpe nafasi ya ngapi,, fikiria kama tamaa yake ya kuendelea baada ya miaka 10 ingefanikiwa na akakaa miaka 20. Je nchi ingekuwa wapi? Piga picha hiyo, na utoe nafasi.

Namba 4, Asiyejua kwa nini aliutaka Uraisi ni kama mtoto anayelilia wembe na akapewa ! Uraisi wake ni feki - anachezeshwa kama "puppet. Sijui anachezeshwa au ndio mbinu za kisiasa hizo. Kuna mifano ya marais wengi, hutumia mbinu hizo na kufanya vizuri katika maendeleo. Aliposhindwa katika uchaguzi kiongozi wa chama cha KADIMA (Israel), alisema maneno yafuatayo: Kuna wanasiasa wanaoamini kuwa maneno na vitendo ni tofauti. Akimaanisha kuwa hawatatekeleza yale wanayoahidi. Na ni kweli, katika utawala wa Nitanyau Palestine imetulia kuliko alivyoahidi vita tu na HAMAS, na kwamba atakifuta chama hicho. Kitu ambacho hakijatokea.

Naona mchezo bado mgumu, watoa hoja wameogopa sana kutaja moja kwa moja jina la Rais aliyeshinda. Lakini maelezo ya kila mmoja yanaashira sana kuwa Nyerere yu karibu zaidi kushinda tuzo.
 
yaaani hata msemeje naweza nikapanga MAraisi bora wa tanzania kwa awamu zoote nne, unajua sisiwachache wenyebahati ya kuuudhulia awamu zoote nne tunaweza kusema with reasons
1. Nyerere
2. Mkapa
3. Mwinyi
4. huyu simtaji ila ni wamwisho anaharibu kila kitu hana chakujisifia mpaka sasa
sisemi kwa unafiki ila anahitaji abadilike zaidi
 
Back
Top Bottom