Gudboy
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 867
- 77
MWANAMKE Mwanaidi Majid anasakwa na jeshi la polisi kwa kitendo chake cha kumuua mume wake kwa kumchoma na kisu baada ya kumfumania.
Mwanaume huyo aliyeuawa alifahamika kwa jina la Jophrey ama kwa jina maarufu 'Chochorii Chochoraa' aliuawa baada ya mzazi mwenzake kumchoma na kisu kwa kile kilichodaiwa kuwa alimfumania akiwa na mwanamke mwingine.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea jana kwenye majira ya saa 4 asubuhi, huko katika Mtaa wa Mukendo wilayani Musoma mkoani Mara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Liberatus Barow, amesema kuwa marehemu huyo ambaye ni mcheza shoo maarufu mjini humo aliuawa na mzazi mwenzake huyo baada ya kumkuta akiwa na msichana mwingine kwenye bahati nasibu.
Amesema mtuhumiwa Mwanaid, alipomkuta mzazi mwenzake huyo akiwa na msichana huyo ndipo alipomvaa mwanamume huyo na kuanza kupigana naye ambapo baada ya muda mfupi alichomoa kisu kisha kumchoma nacho tumboni.
Kamanda Barow amesema, jeshi lake linaendelea kumsaka mwanamke huyo ambaye alitoweka baada ya tukio.
source: nifahamishe.com
Na Mwandishi Wetu. Musoma
Mwanaume huyo aliyeuawa alifahamika kwa jina la Jophrey ama kwa jina maarufu 'Chochorii Chochoraa' aliuawa baada ya mzazi mwenzake kumchoma na kisu kwa kile kilichodaiwa kuwa alimfumania akiwa na mwanamke mwingine.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea jana kwenye majira ya saa 4 asubuhi, huko katika Mtaa wa Mukendo wilayani Musoma mkoani Mara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Liberatus Barow, amesema kuwa marehemu huyo ambaye ni mcheza shoo maarufu mjini humo aliuawa na mzazi mwenzake huyo baada ya kumkuta akiwa na msichana mwingine kwenye bahati nasibu.
Amesema mtuhumiwa Mwanaid, alipomkuta mzazi mwenzake huyo akiwa na msichana huyo ndipo alipomvaa mwanamume huyo na kuanza kupigana naye ambapo baada ya muda mfupi alichomoa kisu kisha kumchoma nacho tumboni.
Kamanda Barow amesema, jeshi lake linaendelea kumsaka mwanamke huyo ambaye alitoweka baada ya tukio.
source: nifahamishe.com
Na Mwandishi Wetu. Musoma