Augustino Mrema: Behind the Scene

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,963
10,460
Mnyonge Mnyongeni, lakini haki yake mpeni.

Katika kikao cha saba cha bunge lilohitimishwa jana, kamati yake ya Hesabu za serikali a mitaa ilitoa ripoti moja nzuri sana juu ya ubadhirifu mkubwa ulioonekana katika serikali za mitaa.

Kamati yake, tofauti na kamati nyingine za bunge, ilithubutu kutaja kwa majina na mahali walipo wahusika wa ubadhirifu wa mali za halmashauri na kutoa mapendekezo mazuri sana ya hatua za kuchukua dhidi ya wahalifu hao na namna ya kuzuia wizi huo kwa siku zijazo.

Mheshimiwa huyu aliongea kwa uchungu sana namna anavyoumizwa na wizi huu, huku huduma za kijamii zikizorota kwa kukosa pesa.

Behind the Scene (vibwagizo)
  • Mrema ni mtu pekee ambaye amewahi kupewa cheo kisichotambulika katika katiba ya nchi (Naibu waziri Mkuu), enzi za mzee Ruksa. Enzi hizo pia alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani na utendaji wake ulijulikana sana.
  • Ni mtu pekee ambaye amekuwa mbunge katika majimbo mawili tofauti. Alikuwa mbunge wa Jimbo la Temeke mkoani Dar Es Salaam mnamo mwaka 1996 baada ya mahakama kutengua ubunge wa Ally Kihiyo, ambaye alighushi elimu yake katika wasifu wake, na kwa sasa Mrema ni mbunge wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro
  • Ni mtu pekee ambaye amekuwa mwenyekiti wa vyama viwili tofauti vya kisiasa kwa nyakati fofauti na amegombea uraisi kupitia vyama hivi viwili tofauti. Alikuwa Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Mnamo mwaka 1995 enzi hizo Mabere Marando akiwa katibu mkuu na aligombea ubunge mwaka huo. Alihama NCCR na kuhamia TLP ambako alimpindua Leo Lwekamwa na kumtimua Thomas Ngawaiya aliyemkuta hapo, na amegombea uraisi mara mbili kwa tiketi ya chama hiki.
  • Ni mmoja wa wabunge waliokunywa 'Kikombe' cha Babu Ambilikile Mwasapile wa Loliondo

Mwenye vibwagizo zaidi aongezee.

Nawasilisha
 
amewahi kuwa mbunge wa moshi vijijini, Temeke na sasa Vunjo ..... na amewahi kujiuzulu katika nyadhifa yake katika dhana ya uwajibikaji

ingawa kwa sasa uwezo wake upo katika stage ya "standstill"
 
Ni waziri pekee aliyehamua kuweka rehani uwazi wake kwa kukiuka kanuni ya collective responsibility huku akijua wazi kitakachofuata....

Nendeni mkajifunze kiswahili upya jamani lol, hamua=amua, hacha=acha, hogopa=ogopa.......mko wengi na mnakera sana.
 
mwalimu mwenyewe hajui kiswahili mwanafunzi atajua kweli
nashukuru umemfundisha hapa hapa jf.

Nendeni mkajifunze kiswahili upya jamani lol, hamua=amua, hacha=acha, hogopa=ogopa.......mko wengi na mnakera sana.
 
Ni mtu pekee aliyeweka mapipa ya lami kule kilema akiwa na lengo la kujenga barabara
japo hakufanikiwa baada ya serikali kumtimua unaibu waziri, hivyo mshiko ukawa kidogo.
 
Ni mtu pekee aliyeweka mapipa ya lami kule kilema akiwa na lengo la kujenga barabara
japo hakufanikiwa baada ya serikali kumtimua unaibu waziri, hivyo mshiko ukawa kidogo.

mkuu mamdenyi inaelekea tumetoka sehemu moja, mbonyi mbee
 
amewahi kuwa mbunge wa moshi vijijini, Temeke na sasa Vunjo ..... na amewahi kujiuzulu katika nyadhifa yake katika dhana ya uwajibikaji

ingawa kwa sasa uwezo wake upo katika stage ya "standstill"

LAT hapo kwenye red sikumbuki alipatakujiuzulu wadhifa gani.

Kwenye blue umepiga chini ya mkanda kabisa na maumivu yake huwa makali sana.
 
Chama chake ni chama pekee kinachotumia Jogoo kama alama ya Bendera yao. Na ni Mwaenyekiti pekee wa chama aliyeacha kumpigia kampeni mgombea wake wa urais 2010 na kumpigia ****** ili magamba yasimsumbue.
 
LAT hapo kwenye red sikumbuki alipatakujiuzulu wadhifa gani.

Kwenye blue umepiga chini ya mkanda kabisa na maumivu yake huwa makali sana.

mkuu
Augastine Mrema aliwahi kuwa afisa usalama katika wizaraya mambo ya ndani wakati huo Mzee Ali Hasan Mwinyi alikuwa waziri wa mambo ya ndani .... miaka ya 1980's kulitokea mauaji ya watu waliosadikika ni wachawi huko mwanza/shinyanga na Mwinyi kama waziri na Mrema walijiuzulu kupisha uchunguzi na uwajibikaji
 
Back
Top Bottom