Augustine Lyatonga Mrema: Mpiganaji!

Ninauhakika Mrema bado ana nafasi ya pekee sana. Katika Project X mojawapo ya mambo tunayoangalia ni nani atampinga JK mwakani kwa ufanisi mkubwa. Huyu tutamtengeneza na mojawapo ya majina matatu tunayoyaangalia ni la Mrema.
mimi naamini kwamba kuna njia moja tu ya kuitoa ccm madarakani na hii inaweza kutokea kama vyama vya upinzani vyote vitaungana kusimamisha mgombea mmoja tu na viongozi wengine wakubwa wote waliobakia kwenye upinzani wakagombea ubunge kwenye majimbo yao husika.na hili litawezekana kama pia watakuwa wakali sana na tume ya uchaguzi hili ufanyike kwa haki sio kama miaka iliopita.
wananchi tuko tayari kwa mabadiriko kwani enough is enough with ccm na hakuna anayependa kutaabika wakati utajiri wa nchi yetu tunauona hivi hivi unaliwa na wachache.tatizo kubwa ni wao wapinzani kwani wameshindwa kutufanya tuamini kwamba wako tayari kutuongoza kwani wao wenyewe wanashindwa kujiongoza kwenye vyama vyao.
Kama wapinzani kweli wana uchungu na nchii hii basi waweke tofauti zao pembeni na wakubaliane kuweka mgombea mmoja na wakubwa waliobaki waingie bungeni.kwa njia naamini kama hawatofanikiwa mwakani basi 2015 nchi itakuwa yao.
swala la wapinzani kugawanyika sasa hivi ni wanaisaida ccm sana kwani mgawanyiko wao unagawanya kura pia na mwisho wa siku ccm ndio anaishia kuwa na kura nyingi kuliko wao.hakuna sababu yakusimamisha wagombea wa ubunge wa 4 au 5 kutoka upinzani kwenye jimbo moja,kwani hii inasaidia ccm zaidi.
kazi kwenu wapinzani kama kweli mnaipenda hii nchi na mnataka kutuletea maendeleo wananchi basi inabidi mjiunge mapema mno hili sisi wananchi tujue msimamo wenu huko vipi.
 
Last edited:
mimi naamini kabisa mrema alikosea kutoka ccm kwa wakati ule.
nia yake ya kutaka kuleta mabadiliko na kuwa kiongozi wa TZ ilikuwa nzuri, lakini njia ya jinsi ya kufika huko(kuwa kiongozi wa TZ) ndio ilikuwa mbaya.

saa ingine kama unataka kufika kileleni cha kazi yako/siasa au mambo mengine lazima utii amri za wakubwa wako hata kama ukubaliani nao.

kwa wakati ule mrema alikuwa kwenye nafasi nzuri sana na kama angebaki ccm, si mkapa wala kikwete wangeweza kusimama na mrema. sasa hivi tungekuwa tunamuongelea mrema kama x-president, na kama angekuwa rais 1995 basi angeweza kupambana na mafisadi/ufisadi wote....

hali kama ya mrema imejitokeza hivi karibuni kwa zitto (ingawa motive za zitto kugombea hazijulikani), lakini zitto alichokifanya amewasikiliza wazee wa chadema kwa ajili anajua time yake itafika. zito anachotakiwa kufanya ni kucheza vizuri na kuakikisha vitu vilivyompatia umaarufu anaviendeleza, kwa ajili katika wanasiasa TZ ambao ni +/- 5 ya umri wake yeye ndiye maarufu

je mrema angebaki ccm na kutii ya wakubwa wake sasa hivi tungekuwa tuna mwita X-president????
 
yaani mimi nauthamini mchango wake kwa nchi hii sana na pia he is a leader of his sort ambae tungependa kuwa nae mwenye uwezo wa kuamua jambo na kulitolea ufumbuzi linapojiri we need strong leaders jamani . waafrica wanatakiwa kutishwa tishwa. na ni mpambanaji sana bwana.

kuwahi kazini, sungusungu, vituo vya polisi kujengwa jirani na raia, majambazi kurudisha silaha, kujitoa CCM, kupambana na ccm BILA kumwogopa mwenye CCM muda huo! this was man and still is!!.... I am ranking him 3rd katika historia ya mashujaa wa taifa hili baada ya uhuru!

Nyerere
Sokoine
Mrema
 
Mkuu mbele ya mwenye chama chake enzi hizo (Mwalimu), Mrema asingekubaliwa kugombea urais

Ni kweli mkuu, wale wanaomlaumu Mrema eti alikimbilia kule mara alikurupuka ni kama washabiki tu wa mpira wa miguu ambao wanaouona mpira zaidi wakiwa nje ya uwanja,ndo ukweli huo,ukiwaingiza uwanjani ni utumbo tu,dizaini za washabiki ambao hata chandimu hawakucheza lakini shuhudia wanavyoujua mpira na ku critisize wakiwa nje ya uwanja ama watazamaji...Yote aliyofanya Mrema ni sawa tu,aliyafanya kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla,wananchi ndio hawakumwelewa na wanasiasa walitumia ufinyu huo wa ulewa wa wananchi kwa manufaa yao....Ukitizama kwa undani utangunduwa kuwa vichaa ni wananchi waliompinga na ambao bado hawakubali kuwa ilikuwa ni ukichaa kumpinga mpiganaji wa kweli.
 
- Ni kweli in the absense of mashujaa kama lilivyo taifa letu, Mrema ni shujaa,

- Lakini si nimesikia kwamba wana usalama wa taifa wa serikali ya CCM, kama alivyokuwa Mrema huwa hawastaafu, wala kutoka mpaka mwisho wa maisha yao au kuna exception kwa Mrema?

Respect.

FMEs!
 
Pia kama tungekuwa na Mrema madarakani, ujambazi ungepungua sana Tanzania. Jamaa alijua kuzitumia "siku saba"

Hatutaweza kupata maendeleo mpaka pale viongozi wetu watakapoweza ku level na wananchi. Kwa maana kwamba watambue hali halisi na ku act accordingly badala ya kujigeuza na kujifanya tofauti kabisa na wananchi....Kwamba wawe in touch instead of out of touch. Mambo aliyokuwa akiyafanya Mrema yalipekea kuambiwa kuwa ni kwasababu ya kutokusoma nk,na kwasababu yalikuwa ni nje ya utashi wa kisomi na siasa uchwara za kikabila,ikawa rahisi kwake kuwa branded "kichaa" na huku ukiangalia kiundani,uelewa mdogo wa wananchi uliosababishwa na ufinyu wa elimu ndo silaha kubwa ya ccm na mafisadi wake. Mrema clearly leveled with THE PEOPLE na he was amongst them.....In reality,he was the right one for our generation.Siasa zetu zilitufanya tuwaone viongozi wetu kama ndugu zetu,hata mwalimu alisema waitwe ndugu..Na kwa ufahamu wetu,tukasema ni ndugu hawa na usomi wao walioupata kwa jasho letu watatusaidia.

Waliosoma ubepari tafsiri yake ikawa ni ubinafsi,hakuna undugu,undugu ni kwenye maandishi tu lakini utendaji ni ubinafsi,hawaku level na wananchi na taizo hilo bado lipo....Hapo classes za walio wasomi na wasio wasomi ambao ni watawaliwa na watu wa kudanganywa zikawa created. Wananchi bado hawaelewi kuwa inawezekana kuwa hold accountable hao ndugu..Ni mentality mbaya sana inayotu cost hadi sasa kwasababu mwalimu alikuwa akiwaamisha tu hata kama wakifanya kosa gani,mradi tu waliitikia kauli mbiu za zidumu fikra sahihi na kwamba hawa ni ndugu...Tuko karibu na viongozi kuliko wao walivyo karibu na sisi,at least kifikra na kimatarajio kwasababu kila mwananchi akienda kupiga kura pale penye kuidondosha kwenye sanduku yuko peke yake,ni kama ahadi anajiwekea na ndugu huyo anayemchagua,lakini wakati wa vote tallying, ajenda yao hiyo haina nguvu na wakati wa kuuliza huwezi kuuliza mwenyewe kama ilivyo wakati wa kudondosha kura yako peke yako kwenye sanduku, na mabadiliko ni lazima mobilization...ani sasa hata yule aliyeko nyuma yako amabye hujui alimpigia nani kura awe consulted.

Ni mkorogo lakini kwa kifupi Lyatonga was a honest and a decent man who leveld with his people. Aliyashughulikia matatizo jinsi yalivyo na si kufanya usanii kwa kutumia usomi na mambo ya protokali.

This man is a honorable man beyond all the dirty politics.....Alikuwa na nia ya ukweli na halisi ya kumsaidia mtanzania....Tanzania kama familia,tulifanya makosa kumpuuzia ndugu yetu Mrema,mwalimu na yeye kama baba,alifanya makosa yaliyo icost familiy yetu na ambayo bado yanaendelea kui cost,kama kweli mwalimu aliamua kuwa siasa za vyama hazina nguvu zaidi ya siasa za maslahi ya Taifa kwasababu ukoloni ulishaondoka,basi angeondoa ubinafsi na kuhakikisha kuwa Taifa linaongozwa kwa misingi ya uzalendo wa kweli....Mwalimu kama binadamu alifanya kosa.

Hivyo basi ujambazi na matatizo ya kijinsia kama alivyosema Kwame very minor kwa watu wasomi,ila ukweli ndio matatizo tuliyonao ambayo wao kama wasomi hawaoni kama yana exist...Ni kama mwalimu tu na hotuba za nguvu ambazo kinadharia zinakubalika lakini kivitendo hazi level na hali halisi...Hadi tutakapowachagua viongozi wenye kuwa in touch na wananchi halisi,bado hata tatizo la ufisadi litaonekana kama chuki binafsi tu kama anavyo ainisha mkuu wetu wa nchi.
 
- Ni kweli in the absense of mashujaa kama lilivyo taifa letu, Mrema ni shujaa,

- Lakini si nimesikia kwamba wana usalama wa taifa wa serikali ya CCM, kama alivyokuwa Mrema huwa hawastaafu, wala kutoka mpaka mwisho wa maisha yao au kuna exception kwa Mrema?

Respect.

FMEs!

Mkuu FMES ushujaa uko determined kutokana na historia ya nchi ama jamii yenyewe,hatuwezi ku import shujaa,tutasoma historia yetu jinsi ilivyo na kubaini kuwa shujaa ni nani accordingly. Kama historia yetu hairuhusu kuwa na mashujaa basi hatuwezi kuwa nao,na kusema in a absence of mashujaa ni sawa na kufananisha ushujaa na kama kipaji flani ambacho kilitakiwa kiwe imported,that is impossible,kama tuna mashujaa base on our history tunao,na kama hatuna,basi hatuna,hatuwezi kusema this is a least shujaa kwasababu we lack the people with "Shujaa talents"
 
Mrema ni great leader.Na he is a legend to Tanzanians kama alivyo Mwalimu.Mrema kosa lake kubwa ni hakujua how capable mafisadi walivyo and to what extent they will go to destroy anything that was on their way.Yeye aliamini kuwa kuna democracy ya kweli.Uchaguzi wa 1995 alishinda clearly. Every move ambayo alifanya Mrema ilikuwa kwa maslahi ya wananchi.From the day alivyoondoka ccm he was very popular kuzidi rais mwenyewe.hata pale 1997 alienda kugombea temeke akashinda ubunge.ni Mrema pekee amegombea majimbo tofauti na akashinda.watu wa temeke walijua cv yake and wat he can do for them.lakini mgogoro ulivyozidi Nccr aliachia ubunge na kujiunga na Tlp.How many people wanaweza kufanya hivyo.wakina seleli na mwakyembe sio wapinzani wa kweli.sio lazima wahame ccm but wawe wanaweka kila kitu hadharani na sio ku edit the truth eti for the benefit of the country. Tatizo wako afraid ku loose benefit zao na wadhifa kitu ambacho Mrema Hakujali. Kwangu binafsi mashujaa wa Tanzania ni Mrema na Sokoine.Mwalimu alikuwa na ukabila fulani. As a leader their is no room for that. Kwa sasa hakuna upinzani wa kweli na Ccm wata excel kwenye uchaguzi ujao despite ufisadi wao. Huko chadema ni mafisadi na undugu umejaa.na ni chama pekee kwa sasa chenye nguvu na uwezo waku make a difference. But sorry kuwa dissapoint.ITS NGO. To conclude Mrema made a difference to this country. He is a great man and a great leader kama Sokoine au Mandela.
 
Ametajwa mara nyingi kuwa ni pandikizi la ccm upinzani na kuwa atarudi tu ccm. Miaka imepita na majaribu mengi amepitia lakini hajapiga magoti kwa ccm. Kati ya wapiganaji wote huyu ndiye shujaa wangu. Natumaini historia itamhukumu vyema na kwa haki.
huyo bado ni CCM tu kama alivyo kuwa marando,akimaliza kazi ya kuua vyama atarudi CCM.NCCR ni kama haipo kwa ajili ya yeye na wenzie,sasa TLP inachechemea chini ya uongozi wake.
Lini na WAPI alirudisha hiyo KADI YA CCM?
 
Natofautiana na wengi humu. Mrema ushujaa wake uko wapi zaidi ya kujitoa CCM? Si huyu kwa sababu ya kupenda ukubwa ndiye aliyeharibu kila alipoenda? Huyu ndiye aliyekuwa tumaini kubwa la wanaotaka mabadiliko lakini akaichezea cooni hiyo turufu. Hapana, mimi sijaona bado ushujaa wake.

Amandla.......
 
Natofautiana na wengi humu. Mrema ushujaa wake uko wapi zaidi ya kujitoa CCM? Si huyu kwa sababu ya kupenda ukubwa ndiye aliyeharibu kila alipoenda? Huyu ndiye aliyekuwa tumaini kubwa la wanaotaka mabadiliko lakini akaichezea cooni hiyo turufu. Hapana, mimi sijaona bado ushujaa wake.

Amandla.......

Fundi,hatuwezi kwenda nje ya matukio ya kisiasa ama historia ya nchi yetu kumpata shujaa wa wakati huo...Kutokana na historia ya siasa zetu kubaki ccm inawezekana ndio ushujaa kwako. Tatizo siyo kupenda ukubwa,bali the urge to be the leader and to inspire the people....Kazi aliyoianza ilitakiwa aimalize na wafuasi wa kazi zake ni mtaji wa kisiasa uliokuwa ukimezewa mate na wanasiasa wa pande zote za upinzani na ccm...Kama kubaki ccm ni maslahi na kujitoa ndani ya ccm ni kinyume chake kama historia inavyojidhihirisha,je huo si ushujaa?Ulaji ndio umekuwa tatizo sugu hata kwa wale wanao attempt kuwa mashujaa wa wananchi,lakini wewe unadespise matendo ya kuacha ulaji kama tamaa ya madaraka,what the heck?
Uwezo wa kuyashugulikia mambo mengi huendena na authority aliyonayo kiongozi huyo,the more authority the better scope for dealing with the so issues,Unasema alikuwa anapenda ukubwa,sasa ulitaka awe katibu kata ili kuushughulikia ufisadi wa Taifa?Wapenda mabadiliko gani hao na walifanya nini kwenye vita hiyo ya ufisadi wakati wa sakata la Mrema?
 
Labda nitakuwa na upungufu wa misamihati lakini nadhani Mrema alikuwa na Guts. Neno shujaa ni lazima liambatane na busara, strategies za kushinda au kufikisha ujumbe vitu ambavyo viko kwenye short supply tukimzungumzia ndugu Mrema.

Kushiriki kwa Mrema katika uchaguzi wa 1995 bila kuwa na mabadiliko ya kihalali ya kikatiba kumeisaidia sana CCM.

Kulikuwa na watu waliotaka katiba yenye kuruhusu wagombea huru na nchi wahisani zilikuwa zinatoa shinikizo kwa serikali kubadilisha. Lakini ghafla akatokea mtu maarufu aliyetaka kugombea kwa kupitia chama. Hivyo agenda zote za mabadiliko ya kikatiba zikawekwa kapuni.

Baada ya kushindwa ndio anagundua kuwa katiba ndio yenye kuwapa advantage CCM. Lakini alitakiwa kuyaona hayo kabla yenye kushiriki kwenye uchaguzi wa 1995.
 
Ametajwa mara nyingi kuwa ni pandikizi la ccm upinzani na kuwa atarudi tu ccm. Miaka imepita na majaribu mengi amepitia lakini hajapiga magoti kwa ccm. Kati ya wapiganaji wote huyu ndiye shujaa wangu. Natumaini historia itamhukumu vyema na kwa haki.
mkuu umenenaa..

Mrema bado anatofautiana sana na wanaojiita wapiganaji wa ufisadi(mwakyembe, seleli, sendeka, kilango, kimaro, mengi, lembehi, nape nk) pamoja na wengine kuwa wasomi wa vyeti.

Mrema hakutaka kuikana nafsi yake kwa ajili ya ubionafsi wa mwili bali mara aliondoka CCM na kuacha vyeo vyoteee ambavyoo wapiganaji hawana na walicho nacho (ubunge) wanautamanii sanaa ndani ya CCM.

Si wapiganaji bali wapenda sifa rahisi kutoka kwa jamii isiyochambuaa kwa kina mwelekeoo wa mapambanoo ya kuleta mabadilikoo.
 
..sidhani kama Mrema alikuwa akiwa-treat wapinzani vizuri na kwa heshima.

..pia zilianza kuenea fununu kwamba Mrema naye anachukua kidogo-dogo toka kwa wafanyabiashara wakubwa.

..tena nakumbuka alikuwa na urafiki mkubwa na wahindi familia ya kina Bora mpaka kufikia kufungua mgahawa wao hapa mjini.

..siamini kama Mrema ni mwana-demokrasia wa kweli. vilevile si mtu anayeshaurika. kuna masuala mengi sana alikuwa akishauriwa na Prof.Baregu lakini aliyapuuza na mwisho wake tunaujua.

..waanzilishi wa NCCR walichoshwa na tabia na vituko vya Mrema na zaidi suala la kutokushaurika na hicho ndicho chanzo cha mgogoro mkubwa ndani ya chama hicho.

NB:

..mkiona kama taifa tunaanza kumlilia mwanasiasa wa aina ya Mrema mjue tuna hali mbaya ya kusikitisha.
 
Labda nitakuwa na upungufu wa misamihati lakini nadhani Mrema alikuwa na Guts. Neno shujaa ni lazima liambatane na busara, strategies za kushinda au kufikisha ujumbe vitu ambavyo viko kwenye short supply tukimzungumzia ndugu Mrema.

Kushiriki kwa Mrema katika uchaguzi wa 1995 bila kuwa na mabadiliko ya kihalali ya kikatiba kumeisaidia sana CCM.

Kulikuwa na watu waliotaka katiba yenye kuruhusu wagombea huru na nchi wahisani zilikuwa zinatoa shinikizo kwa serikali kubadilisha. Lakini ghafla akatokea mtu maarufu aliyetaka kugombea kwa kupitia chama. Hivyo agenda zote za mabadiliko ya kikatiba zikawekwa kapuni.

Baada ya kushindwa ndio anagundua kuwa katiba ndio yenye kuwapa advantage CCM. Lakini alitakiwa kuyaona hayo kabla yenye kushiriki kwenye uchaguzi wa 1995.

Si kweli Zakumi,si kweli kwamba neno shujaa lazima liambatane na maneno hayo niliyo ya highlight...Once again ume categorize namna ya ushujaa unaotaka mtu flani awe nao bila kuzingatia historia halisi. Mkwawa ni shujaa,ali committ suicide,si kila mtu anaamini kuwa ku committ suicide ni ushujaa and so forth...Tujadili kama grat thinkers wa kweli na tuweke porojo pembeni. Kwa mtu kama Mrema alikuwa na mtaji wa kisiasa,na mtaji huo ni wafuasi,hata hao wenye kutaka mabadilko watayapata vipi kama hakuna wananchi wenye kusapoti?Mabadiliko ya katiba yatapatikana vipi kama huta wamobilize wananchi towards that agenda?Hao mnaodai walikuwa na agenda nzuri si kweli,wote walikuwa wakiwamezea mate wananchama kwani the more you have the better off you are.

Hilo la ushujaa ni pana, however thread heading inasema "Mpiganaji" we can discuss both,personally base on the real situation on the ground at the time,Mrema is still a hero,hiyo ni bila kutumia vigezo vyangu binafsi kama wewe ulivyofanya kwa kusema eti neno shujaa lazima liambatane na busara na winning strategies,ukweli ni kwamba si kweli kuwa kila shujaa huwa anatafuta ushindi. Kwa kufanya mambo amabayo si wengi wanaweza kuyafanya ama ku ya accomplish ni characteristic ya ushujaa,na hilo liko wazi miongozi mwa wanasiasa wetu....Hakuna anayethubutu kuutema ulaji by anymeans.

Kutaka kumsingle out Mrema kuwa aliyazuia mabadiliko ya katiba ni upotoshaji...Alifanya kazi yake lakini kikwazo ni wengi wetu,na bado pia hadi sasa kikwazo cha vita ya ufisadi ni wengi wetu.
 
Naamini angemvuta JK au Lowassa ili wagombee urais na yeye kuwa tayari kuwa PM, wangelikuwa na nafasi kubwa sana ya kushinda.

Kwa mantiki hiyo mrema hakufanya kosa kwani hao JK na Lowassa si tunaowaona sura zao halisi sasa? Kwa utendaji kazi wa mrema angefikia pale alipofikia marehemu Sokoine., yaani waziri mkuu kutokubaliana na rais.
Historia ya mrema ya upambanaji ni kubwa na inahitaji thread ya peke yake; nimefurahi huyu aliyejaribu kuuliza;ni kweli wakati mrema anatoka serikalini, wapiga kura wapya wa sasa hivi walikuwa watoto wadogo sana. Nikipata muda nitawaeleza kilichotokea - yapo mengi - akina patel na mashamba ya mkonge (ni patel wale wale wa sasa), Chavda nk. Kweli mrema was right!
 
Back
Top Bottom