Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Wakati naendelea kulumbana na FMES na Mzee Mwanakijiji kuhusu wajibu wa Wapiganaji, Vita ya Wapiganaji na ni nani anafaidika na Upiganaji, jina moja linakuja mukichwa na dhamira inaniambia kuwa hukukweli alikuwa ni mpiganaji.
Mrema pamoja na udhaifu wake wa kuchemka kwa nguvu ya soda, kuwa na elimu duni na kufanya mambo kwa pupa, Kitendo chake cha kutoka CCM ni kwa kuwa aliweka Utaifa na Utanzania mbele na si maslahi yake binafsi au ya chama.
Naomba mwenye kumbukumbu nzuri, atukumbushe ni kwa nini Mrema aliamua kuasi ndani ya Baraza la Mawaziri na hata kuamua kuachana na CCM na kuingia upinzani?
Nakumbuka tetesi ni kuwa alikataa kukubaliana na uamuzi wa Baraza la Mawaziri (collectively responsibility) kufumbia macho wizi wa fedha BOT ama kupitia mfuko wa EPA au CIS na aligangamaa kuwa ataanzisha uchunguzi na kupeleleza kilichotokea. Alipoambiwa alifumbie macho, akaghadhibika na kukataa kukaa upande mmoja na Baraza la Mawaziri na Serikali na hivyo kuasi na kulazimika kujivua/kuvuliwa uwaziri na mwishowe kujitoa CCM.
Mrema hakujali maslahi yake au kitakachotokea kwake baada ya kuondoka CCM (life after action), ingawa aliingiwa na pupa ya kutaka apewe uenyekiti wa CHADEMA na alipokataliwa, ndipo akaungana na Wana Usalama wenzake kina Mabere Marandu kule NCCR.
Ninachotaka kujengea hoja ni kitendo chake cha kukataa kukubali kufumbia macho uhalifu na uhujumu na kutii amri ya kuwajibika kwa jumla kuruhusu Uhujumu.
Je ni Watanzania wangapi na Wapiganaji wangapi ambao leo hii wako tayari kupoteza nafasi zaoza kazi na maslahi wakiwa katika mfumo wa Kiutawala na Kisiasa kwa kusimamia haki, utu na uwajibikaji ili kulinda maslahi ya Watanzania na Taifa?
Mrema pamoja na udhaifu wake wa kuchemka kwa nguvu ya soda, kuwa na elimu duni na kufanya mambo kwa pupa, Kitendo chake cha kutoka CCM ni kwa kuwa aliweka Utaifa na Utanzania mbele na si maslahi yake binafsi au ya chama.
Naomba mwenye kumbukumbu nzuri, atukumbushe ni kwa nini Mrema aliamua kuasi ndani ya Baraza la Mawaziri na hata kuamua kuachana na CCM na kuingia upinzani?
Nakumbuka tetesi ni kuwa alikataa kukubaliana na uamuzi wa Baraza la Mawaziri (collectively responsibility) kufumbia macho wizi wa fedha BOT ama kupitia mfuko wa EPA au CIS na aligangamaa kuwa ataanzisha uchunguzi na kupeleleza kilichotokea. Alipoambiwa alifumbie macho, akaghadhibika na kukataa kukaa upande mmoja na Baraza la Mawaziri na Serikali na hivyo kuasi na kulazimika kujivua/kuvuliwa uwaziri na mwishowe kujitoa CCM.
Mrema hakujali maslahi yake au kitakachotokea kwake baada ya kuondoka CCM (life after action), ingawa aliingiwa na pupa ya kutaka apewe uenyekiti wa CHADEMA na alipokataliwa, ndipo akaungana na Wana Usalama wenzake kina Mabere Marandu kule NCCR.
Ninachotaka kujengea hoja ni kitendo chake cha kukataa kukubali kufumbia macho uhalifu na uhujumu na kutii amri ya kuwajibika kwa jumla kuruhusu Uhujumu.
Je ni Watanzania wangapi na Wapiganaji wangapi ambao leo hii wako tayari kupoteza nafasi zaoza kazi na maslahi wakiwa katika mfumo wa Kiutawala na Kisiasa kwa kusimamia haki, utu na uwajibikaji ili kulinda maslahi ya Watanzania na Taifa?