Atupwa selo kwa kumnyooshea mkono rais

Kubwajinga

JF-Expert Member
Jan 23, 2008
2,194
297
Huu upuuzi wa polisi/ askari kanzu kunyanyasa wananchi unahitaji ukemewe na JK mwenyewe kwani ni kinyume kabisa na demokrasia. Ina maana Joe the Plumber wa USA itabidi aswekwe ndani Obama akishinda uraisi??


Atupwa selo kwa kumnyooshea mkono rais
Na Festo Polea, Mwananchi 10/20/2008

MLEMAVU wa mkono, Issaya Boniface Keraryo amekamatwa na polisi kwa ajili ya mahojiano baada ya kuibuka alikokaa na kusogea mbele ya halaiki kisha kusimama na kunyoosha mkono kuelekea juu kama mtu anayeashiria kutaka kuuliza swali huku akielekeza macho yake kwa Rais Jakaya Kikwete.

Mlemavu huyo alinyoosha mkono kwa muda wa dakika kama tatu na kulazimika askari kanzu waliokuwepo eneo hilo kumsogelea kwa lengo la kumtaka aeleze anachotaka kuuliza, ili kiwasilishwe meza kuu.

Baada ya kusogezwa pembeni askari kanzu hao walizidi kumsogelea na kumpeleka ndani ya jengo la Ukumbi wa Karimjee kisha kumuacha kwa muda hadi Rais na msafara wake walipoondoka ndipo askari hao walipomchukua na kuelekea naye Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano.

Akizungumza na Mwananchi, mlemavu huyo baada ya kuachiliwa na askari kanzu hao alisema alinyoosha mkono kwa lengo la kumtaka, Rais Kikwete kumtafutia wafadhili wa kumsaidia matatizo yake yanayomkabili.

"Nilitaka kumwambia Rais anisaidie kupata wafadhili kwani hali yangu ya afya hairuhusu kufanya kazi za kupata kipato na nyumba ninayoishi nitafukuzwa Ijumaa kwa kuwa sina fedha za kulipia pango," alisema Issaya na kuongeza

"Hata hivyo Rais Kikwete kipindi alipokuwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa nilipata nafasi ya kukutana naye na aliniahidi kunitafutia wafadhili wa kunisaidia matatizo yangu, lakini hadi leo hakuna mafanikio yoyote," alisema Issaya na kutaka kusaidiwa na waandishi.

Mlemavu huyo kabla hajasimama na kuelekea mbele ya adhira, muda mrefu alikuwa amekaa pembeni jjirani na walipokuwa waandishi wa habari, akionekana akinyoosha mkono na kisha kuushusha bila kujulikana alikuwa na maana gani.

Baada ya muda kupita na kuona kuwa rais amemaliza hotuba yake na kitakachofuatia ni kuondoka bila kutoa dukuduku lake, akalazimika kusogea mbele ya watu na kunyoosha mkono kwa muda wa dakika kama tatu na kufanya watu kumshangaa kwa dakika hizo tatu hadi alipotolewa na askari hao.
 
KJ, hii hali ni ya kawaida kwa Tanzania. Nafanya mawasiliano na Mwananchi Communications niweze kupata maelezo ya kina kuhusiana na hili. Kama tatizo lake ni kama ninavyoona hapa:

“Nilitaka kumwambia Rais anisaidie kupata wafadhili kwani hali yangu ya afya hairuhusu kufanya kazi za kupata kipato na nyumba ninayoishi nitafukuzwa Ijumaa kwa kuwa sina fedha za kulipia pango,” alisema Issaya na kuongeza

Basi naweza kuangalia namna ya kutafuta msaada kwa mtu huyu. Binadamu yeyote ni kilema, tofauti zetu ni aina gani ya ulemavu tulio nao.
 
KJ, hii hali ni ya kawaida kwa Tanzania. Nafanya mawasiliano na Mwananchi Communications niweze kupata maelezo ya kina kuhusiana na hili. Kama tatizo lake ni kama ninavyoona hapa:


Basi naweza kuangalia namna ya kutafuta msaada kwa mtu huyu. Binadamu yeyote ni kilema, tofauti zetu ni aina gani ya ulemavu tulio nao.

Muhimu zaidi ni kuwa je JK ana taarifa za yaliyomfika huyu mwananchi au zilimfikia na hana mpango naye?
 
Muhimu zaidi ni kuwa je JK ana taarifa za yaliyomfika huyu mwananchi au zilimfikia na hana mpango naye?
..Sidhani kama JK anafahamu kilichomtokea huyo mlemavu. Tatizo la jamaa wa intelligency nadhani wanafanya kazi kwa kukariri mambo fulani badala ya kutumia na akili zao wakati mwingine. Kwa mtazamo wangu ningewaona waungwana sana kama wangemsaidia huyo mlemevu kusogea mbele hadi alipokuwa JK ili aweze kuwasilisha alichokuwa nacho. au JK amewapig amkwara kuwa sitaki kuona kwenye mikutano watu wananyoosha mikono kwa ajili ya kuuliza maswali.....
 
Sijapenda jinsi stori ilivyokuwa over exaggrated! Kutupwa selo ni kukaa rumande, ila kuitwa kwa ajili ya mahojiano na polisi ni jambo la kawaida katika utendaji kazi wa walizni wa viongozi katika matukio kama hayo. Kwani muda wote huwezi kujua nani ni nani na ana nia gani hasa!
 
Sometimes watanzania siasa zinatuzidi sana, kama JK angemuintertain huyu kilema basi tujue kuwa angakuwa anawindwa na vilema kila aendapo na kila mtu ana matatizo yake,hilo tusilipinge. Ila cha muhimu hapa si kumtazama kilema mmoja ni kwa serikali ya JK kuweka sera maalum za kuwainua watu kama hawa. Hilo la kuwekwa ndani sidhani kama ni kweli, kuingia kituo cha polisi na kuhojiwa ni tofauti na kuwekwa ndani (under arrest).
 
Sometimes watanzania siasa zinatuzidi sana, kama JK angemuintertain huyu kilema basi tujue kuwa angakuwa anawindwa na vilema kila aendapo na kila mtu ana matatizo yake,hilo tusilipinge. Ila cha muhimu hapa si kumtazama kilema mmoja ni kwa serikali ya JK kuweka sera maalum za kuwainua watu kama hawa. Hilo la kuwekwa ndani sidhani kama ni kweli, kuingia kituo cha polisi na kuhojiwa ni tofauti na kuwekwa ndani (under arrest).
Hofsede,
Rais ni wetu wote na kila mtu kwa kuwa alimchagua kivyake ana haki ya kupeleka matatizo yake kwake regardless.

Hivi wewe unadhani kura alipigiwa na mtu mmoja mmoja au kundi la watu kwa pamoja?

Sikiliza, ukiwa na mtoto nyumbani akakuletea shida yake ya daftari ya shule au set ya shule basi utamfukuza na kusema ahhhhhhh mpaka mlete shida zenu familia nzima?

Kilema yule yeye ndiye anajua shida yake na kusaidiwa ni shurti wa si ombi maana aliahidiwa maisha bora. Sasa ana shida hajui kesho atalala wapi na kaona mahali pa kufikisha shida yake, sasa ndio afanyeje?

Niliwahi kuona mtu mmoja anaomba ukuu wa wilaya kwa Mwinyi akiwa rais kwenye mkutano wa hadhara na baada ya siku kidogo tu akapewa.

Huo ndio mtindo wa Ki-tz
 
wanajaribu kukwepa what happened mbeya isitokee tena. ukionekana unakimbelembele unachukuliwa mapema na kuifadhiwa.
 
wanajaribu kukwepa what happened mbeya isitokee tena. ukionekana unakimbelembele unachukuliwa mapema na kuifadhiwa.

I somehow agree with you but it was a very wrong move.

Lakini kama kweli JK hafahamu kuhusu yaliyotokea, nalo ni jambo la kushangaza sana na hao wasaidizi wake wanatakiwa wawajiike. Huyu mlemavu alikuwa na haki ya kusikilizwa hata kama isingekuwa rahisi kupatiwa msaada papo kwa papo.
 
Yani ukinyoosha mkono juu ni kuvunja sheria ama kuhatarisha usalama?
Hao walinzi wanajuwa kazi yao kweli? Tena baada ya kuona ni kilema bado akapelekwa lupango? Ama kweli Hasira hasara.
 
Muhimu zaidi ni kuwa je JK ana taarifa za yaliyomfika huyu mwananchi au zilimfikia na hana mpango naye?

Nadhani kwa sasa Mh. Rais hamuhitaji labda muda mfupi kabla ya uchaguzi 2010 atakuwa na uwezo wa kuona acha mkono bali kidole kitakachonyoshwa juu bila kuinua sana mkono wako.
 
Kama alishawahi kumuahidi huko nyuma,,lazima amsaidie maana alishamuahidi.....bwana ahadi..
 
Forget about ahadi...Alikamatwa kwasababu ya kunyoosha mkono juu kwa nia ya kuuliza swali. Kama lilikuwa ni eneo ambalo ulinzi ulikuwa kamili...Then kumkamata kilema huyo na kumsweka lupango ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
 
..Sidhani kama JK anafahamu kilichomtokea huyo mlemavu. Tatizo la jamaa wa intelligency nadhani wanafanya kazi kwa kukariri mambo fulani badala ya kutumia na akili zao wakati mwingine. Kwa mtazamo wangu ningewaona waungwana sana kama wangemsaidia huyo mlemevu kusogea mbele hadi alipokuwa JK ili aweze kuwasilisha alichokuwa nacho. au JK amewapig amkwara kuwa sitaki kuona kwenye mikutano watu wananyoosha mikono kwa ajili ya kuuliza maswali.....



.watu wa intelligence kwa sasa wanayo haki ya kumtilia shaka kila anayetaka kumsogelea rais....hata kama ni kwa mbali walimweka mahali pa usalama kwa kuwa hawakujua alitaka kuropoka nini....afteral je kama angeamua kumrushia maneno mabaya ...au kumrushia mayai viza..au hata kumdaka miguu i kama yule wa mwanza....

ulinzi wa rais utakuwa umeimarishwa kadiri maadui wake wanavyoongezeka.....
 
PM.. tatizo ni kuanza kuwa na maadui wa kufikirika... siku si nyingi kuna mtu atapigwa risasi kwenye mikutano ya Rais kwa sababu ya kulinda usalama wa Rais kumbe mtu wa watu alikuwa anachomoa wallet tu. Na kwa kadiri anavyozidi kuwa muoga ndivyo hatua dhidi ya wale wanaohisiwa kuwa ni maadui zitakapoanza kuchukuliwa kwa nguvu zaidi na kwa ukali.
 
Kama ameitwa kwa mahojiano tatizo ni lipi?but tukijua kuwa amechukuliwa hatua ambazo si sahihi kwa kutaka kuuliza swali hapo ndo tatizo lilipo.Maana yawezekana kumhoji huko kukawa njia ya kumfikishia Mheshimiwa ujumbe.
 
Forget about ahadi...Alikamatwa kwasababu ya kunyoosha mkono juu kwa nia ya kuuliza swali. Kama lilikuwa ni eneo ambalo ulinzi ulikuwa kamili...Then kumkamata kilema huyo na kumsweka lupango ni ukiukwaji wa haki za binadamu.


Ingekua Leo mngepaza sauti Kali kwa JPM.

Hapa kazi tu
 
Back
Top Bottom