Attention Bodi Ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Kwa Wanafuzi(HESLB)


Kuna vijana wako China wananieleza kuwa hawakuwa radhi kabisa kwenda huko kusoma ila walilazimishwa na wizara husika ili kumantain diplomatic relationship,

sasa kumbe masharti ni kuwa ukichaguliwa China means lazima uende huko bila kujali umechaguliwa sehemu gani.

Kuna ambao walipata UDSM,Mzmbe n.k,wahusika wa scholarships pale wizara ya elimu ya juu wanapitia lists za vyuo vyote,wakikuona tu huko unakuwa deleted na kukupeleka unakostahiki kwa mujibu wa taratibu zao.

Naweza kusema kuna matatizo mengi yanayomfanya mtu aone bora KUBINJUKA out kuliko kuendelea kusoma bongo;kwa mfano
(a)supplementary za ajabu/discontinuation
(b)matokeo si mazuri sana kiasi cha kutokuwa na uhakika wa kutopata chuo/mkopo
(c)kutoeleweka kwa bodi ya mkopo;mara itatoa 60% tu,mara vile.....wabaki mtu wa hali zetu za kimaskini kuyumbayumba.....hivyo kuongeza instabilty katika masomo.
(d)sometimes mazingira ya baaadhi ya courses(kama vile Computer) katika vyuo vyetu hayajatulia,nakumbuka mwaka 2005 vijana wengi sana waliikimbia hii kozi pale mlimani na kwenda India

Critique, Pole sana kwa misconstrued interpretation of my comments. Hata hivyo I was playing sarcasm of some of the reasons vijana wengine huzitumia kama basis ya wao kwenda kusoma nje.

Pia nawapa pole hao vijana ambao kwa mujibu wako walilazimishwa kwenda kusoma China. We need to look into this claim as well. Japokuwa ni vigumu kuamini hilo maana hata mwaka 1996 wakati serikali ilipoleta mkataba kwa wanafunzi wa elimu ya juu, kulikuwepo na forms joint admissions board ambazo zilimtaka mwanafunzi aliechaguliwa zaidi ya vyuop viwili avijaze ili kuonyesha anataka kwenda wapi. Na uzuri wa hizo forms, zilikuwa zina include other East African universities as well.

Mara nyingi sisi wajazaji wa hizi forms tunadharau vipengele muhimu kama hizo. Na pia tabia ya procrastination ambayo imejikita miongoni mwetu husababisha wengi to fall into prey katika mikono ya administrators of these higher education offices. Watu wanaitwa kwenye orientation hawaendi kisa wanaogopa kuonekana wenye mshawsha wa shule. They come two weeks late, chuo imeshapitisha majina ya walio-report. Inaonekana mtu hajaripoti on time, they expect mtu ameenda kwingineko. Na taarfia kama hizi hufikia wizara husika mapema sana wakati wa orientation period. Sasa ikitokea bahati huyo mtu kachaguliwa China, basi wizara husika inamlazimu kwenda huko. I can take this scenario maana ilishawatokea kwa watu wawili ninaowafahamu na mmoja ilibidi aende India mwingine alienda Algeria. It does not sink in easily kuwa mtu unalazimishwa kwenda kusoma China kisa diplomatic ties, let us not justify some claims wakati kuna mechanisms zimewekwa kwa kusuluhisha matatizo kama hayo. Wapo wazazi wanawalazimisha watoto kwenda kusomea nje, mmoja wapo ni ndugu yangu wa karibu, alienda kusoma Urusi, maisha yakamshinda akarudi. Kama ushahidi upo wa watu kulazimishwa basi iwekwe bayana kama issues zingine humu JF tuone kama wahusika hawataadhibiwa.

Kuhusu kufeli, hilo lipo sehemu zote duniani na humu limezungumziwa mno na different influences zimetajwa hadi zile ambazo zipo personal. Swali je hakuna anayefaulu katika vyuo hivi? Kwa nini mtu ukimbie kusoma sehemu moja kwa sababu ya kufeli wakati hujasomea hapo ukajua kiini cha kufeli? Kuna somo moja la CT200 enzi hizo naona kwa sasa ina course code nyingine, wanafunzi walikuwa wanaiogopa hilo somo kama umande. wengi tulitishiwa kuwa tutafeli na hatutafaulu hilo somo. Wapo waliofeli na tupo tulio faulu. Tulipofika mwaka wa tatu tulifundishwa somo la education evaluation and measurements ndipo nikagundua wengi waliofeli ule mtihani walishindwa kwa sababu maswali mengi yalihusiana na application of theory.

Wenye kuelewa Bloom's taxonomy, watakubaliana na mimi. elimu yetu kuanzia sekondari kwenda chini na baadhi ya course za chuo (kutokana na udhaifu wa walimu wengine) imejikita katika ku-test "knowledge". Knowledge is the lowest level katika blooms taxonomy. Mwalimu ukitunga swali la "application" au "synthesis" wanafunzi wengi wanafeli somo ile mbaya na wanabaki kudai umetunga mtihani wa kukomoa. When in actual sense that is a level at least a student in a college should be able to attain. Sipendi kuingia katika mjadala wa supplementaries wala kufeli kwa wanafunzi.
blooms_taxonomy.gif


Ila hao ndugu waliokwama huko Urusi au mahali popote duniani, kama walipewa scholarship za serikali kwenda huko na walikuwa wamechaguliwa kuingia katika chuo chochote Tanzania, THEY HAD A CHOICE! Wakumbuke if you make a choice you should be prepared for its consequence, let there be any. Kama wapo walioenda kwa sababu ndipo walipochaguliwa kwenda kusoma, wakumbuke maisha ni magumu popote maana hata UDSM wapo wanaolala na njaa but where there is a will there is a way.

Marekani pia shule ni ngumu na pengine ni ngumu kuliko jinsi watu wanavyofikiri. Scholarship ukiipata ni lumpsum humo humo ujitegemee pamoja na kulipia mahitaji yote ya shule na bado ununue vitabu maana ni lazima kama unataka kufaulu somo. Hawana makengeza ya kwamba unasubiri hela itumwe, wao wamekupa tarehe, wanategemea utafuta tarehe zao. Ukishindwa its none of their business. Bongo wanafunzi wanapewa hela za book allowance ambayo wameibatiza jina la "Simu allowance" halafu huyo akipata supplementary anasema ameonewa? Certain aspects just do not sit right.
 
tatizo Lenu Mnafanyiwa Hivyo Lakini Wakija Keshokutwa Na Vijokofia Mnakuwa Wa Kwanza Kuwasupport, Wanawaona Mazoba Ndio Maana
Si Ndo Nyie Nasikia Mmefungua Tawi La Ccm? Ccm=serikali Vipi Sasa?
Poleni Lakini Komaeni Ndio Maisha Ya Tanzania Na Watanzania Wake, Siye Wenzenu Tushajiamulia Kuwasusia Hamna Noma
Kama Wamefungua Tawi Is Wamwandikie Makamba
 
Heshima mbele Bimkubwa...
nimekuelewa vema.
Sijui twafanyaje kuthibitisha hiyo claim kuwa hao vijana walilazimishwa,ila nakumbuka siku huyo kijana anaongea na mzee Rajabu pale wizarani kwamba abaki asome computer science pale UDSM mimi pia nilikuwepo,Mzee Rajabu akamwambia " mimi nilikuwepo katika selection board na nimekufuta"...kipindi hicho kabla majina ya waliochaguliwa hayajatangazwa.Kijana akawa hana namna zaidi ya kwenda China kusoma,the goodpart ni kwamba wao hawana matatizo kama yanayowakumba hao Russia...I guess
 
Swali langu bado halijajibiwa kwa kweli, hivi katika Tanzania (elimu ya juu) na serikalini hakuna Mtanzania mwenye uwezo wa kufikiria suluhisho la matatizo ya elimu ya juu na kulifanyia kazi? Tuombe wazungu waje kutusaidia kufikiria?
 
Hivi inakuwaje mtu unakubaliwa kusoma IFM/ UDSM/ MZUMBE etc halafu unaacha kumaliza na masomo hapo unakubali kwenda Urusi?
Huo ni uamuzi mkuu hao wengine walipata nafasi vyuo vya home la huko Russia wakachagua Urusi,Kosa lao lipi???
 
Bimkubwa taratibu kidogo......
Kuna vijana wako China wananieleza kuwa hawakuwa radhi kabisa kwenda huko kusoma ila walilazimishwa na wizara husika ili kumantain diplomatic relationship,hao vijana kwa sababu ya hofu ya kukosa vyuo walilazimika kujaribu sehemu nyingi ikiwemo vyuo vyetu kule Tz,sasa kumbe masharti ni kuwa ukichaguliwa China means lazima uende huko bila kujali umechaguliwa sehemu gani.

Kuna ambao walipata UDSM,Mzmbe n.k,wahusika wa scholarships pale wizara ya elimu ya juu wanapitia lists za vyuo vyote,wakikuona tu huko unakuwa deleted na kukupeleka unakostahiki kwa mujibu wa taratibu zao.

Nakumbuka kuna kijana alitamani kulia akiwaomba wambakishe Bongo,lakini akajibiwa anaweza kubaki bila kujiunga na masomo kwa sababu tayari kashafutwa.

Naweza kusema kuna matatizo mengi yanayomfanya mtu aone bora KUBINJUKA out kuliko kuendelea kusoma bongo;kwa mfano
(a)supplementary za ajabu/discontinuation
(b)matokeo si mazuri sana kiasi cha kutokuwa na uhakika wa kutopata chuo/mkopo
(c)kutoeleweka kwa bodi ya mkopo;mara itatoa 60% tu,mara vile.....wabaki mtu wa hali zetu za kimaskini kuyumbayumba.....hivyo kuongeza instabilty katika masomo.
(d)sometimes mazingira ya baaadhi ya courses(kama vile Computer) katika vyuo vyetu hayajatulia,nakumbuka mwaka 2005 vijana wengi sana waliikimbia hii kozi pale mlimani na kwenda India
Mkuu wewe unaelewa na kujua kinachoendelea wengine hapa wamejawa an wivu an jazba kwa wabongo wenzentu........najua mambo haya yalishanikuta najua kinachoendelea.....wengine wanafikiri vijana wamefata kupanda ndege......hoja hafifu sana.Asante sana bwana Critique
 
Heshima mbele Bimkubwa...
nimekuelewa vema.
Sijui twafanyaje kuthibitisha hiyo claim kuwa hao vijana walilazimishwa,ila nakumbuka siku huyo kijana anaongea na mzee Rajabu pale wizarani kwamba abaki asome computer science pale UDSM mimi pia nilikuwepo,Mzee Rajabu akamwambia " mimi nilikuwepo katika selection board na nimekufuta"...kipindi hicho kabla majina ya waliochaguliwa hayajatangazwa.Kijana akawa hana namna zaidi ya kwenda China kusoma,the goodpart ni kwamba wao hawana matatizo kama yanayowakumba hao Russia...I guess


Hapo Rajab alitumia ubabe ambao haustahili na nadhani alitaka kumnyamazisha kijana wa watu akimwambia yeye ndio amemfuta jina. which in real sense is against the choice of the applicant.

Hii ndio tabia inayoumiza wengi sana katika elimu. Utaratibu upo na unaeleweka sema wengi hawafahamu hilo wanaona bora wakamhonge fulani au watumie mlango wa nyuma matokeo yake unaumia. You spend years nursing a would inflicted by one person. Ila iweje mtu aende kufuatilia majina ambayo hayajatangazwa? Pia kama huyo mtu alituma application mwenyewe ya kwenda China sidhani kama alikuwa na choice mpaka hapo. Je aliomba pia kujiunga na Chuo chochote hapo na akawa amepewa admission? Maana sioni sababu ya mtu kuumia roho na kuhangaika kwenda kuomba upewe nafasi chuo cha nyumbani wizarani. Mara zote admission za vyuo inatolewa vyuoni na siyo wizarani. Pale ambapo joint admissions board inakutana ni wiki moja baada ya vyuo kufunguliwa.

Mimi nadhani huyo kijana alikuwa hana admission ya chuo cha nyumbani na alitaka kubadilisha vyuo wizarani ambapo ni kitu kigumu kufanyika. Angekuwa na admission tayari wala hakuwa na haja kwenda wizarani, angetuma tu barua wizarani kusema haendi tena na wala hahitaji kutaja chuo anachoenda kusomea. Pole zake kwa kweli.
 
Bimkubwa

Nakubaliana na critique
Siku hizi hawafanyi kama enzi zile ,yani tusema TSJ wakianza toa selection yao na jina lako likawemo,uwezekano wa wewe kuchaguliwa UDSM ni mdgogo sana 0.00001%

Sema uzuri unakua selection mara nyingi udsm nzio inaanza kutoa ,hivyo jina lako kupatikana vyuo vingine vya ndani ni kidogo sana unless ktk kuapply uliongeza ama kupunguza jina.

Na ukipata huko nje kama umepata ndani mara nyingi vya ndani wanafuta.
Hata hivyo hiyo ni moja ya sababu lakini MAJUU nayo pia ni sababu kwani kuna watu wanaacha udsm,mzumbe na kwingine wakiwa tayari mwaka wa pili ama wanaingia mwaka wa tatu na kuingia MAJUU.
 
Imetolewa mara ya mwisho: 20.08.2008 0122 EAT
•
Tanzania ya mwisho udahili elimu ya juu

Habari Zinazoshabihiana
• Tatizo Chuo Kikuu ni Mukandala - TAHLISO 25.04.2008 [Soma]
• Sakata la ada, mikopo elimu ya juu... Wasomi watangaza mgomo nchi nzima 27.07.2008 [Soma]
• Sitta ateua wajumbe Baraza la Mitihani 17.10.2007 [Soma]

Na Joseph Lugendo

WAZIRI Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema Tanzania
ni nchi ya kwanza kwa kuwa na kiwango cha chini zaidi
cha udahili wa wanafunzi wa elimu ya juu, katika eneo la
Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Bw. Pinda alisema hayo bungeni juzi wakati akifungua warsha fupi ya uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Elimu iliyofanyika katika ukumbi wa zamani wa Bunge wa Pius Msekwa.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Bw. Pinda alitoa
takwimu za utafiti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wa
mwaka juzi ambazo zinaonesha kuwa Tanzania ina asilimia
0.27 ya wanafunzi wenye sifa wanaojiunga na elimu ya
juu kati ya nchi saba zilizofanyiwa utafiti huo.

Kwa mujibu wa utafiti huo, nchi inayoongoza katika
kundi hilo kwa kuwa na udahili wa juu wa wanafunzi
katika elimu ya juu, ni Afrika Kusini ambayo ina asilimia
9.11 ikifuatiwa na Kenya yenye asilimia 1.47.

Nchi ya tatu kwa mujibu wa utafiti huo ni Uganda yenye
asilimia 1.23 ikifuatiwa na Lesotho yenye asilimia 0.98 na
Msumbiji asilimia 0.33 huku Tanzania 'ikishika mkia'.

Waziri Mkuu alisema Serikali ilishaanza kuongeza juhudi kutafuta mapato endelevu kwa ajili ya kugharimia sekta ya elimu hususan ya juu ambapo mwaka 1998 iliunda kikundi kazi kilichokuwa chini ya iliyokuwa Wizara ya Sayansi Tekinolojia na Elimu ya Juu, ambayo ilifanya utafiti na kupendekeza kuanzishwa kwa Mfuko wa Elimu kisheria.

Vyanzo vya mapato ya Mfuko huo ni bajeti ya Serikali, michango ya hiyari kutoka kwa wadau mbalimbali, michango kwa njia ya zawadi, vitega uchumi na vyanzo vingine vyovyote vitakavyobuniwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania inayosimamia Mfuko huo kisheria.

Huku akitumia usemi wa 'safari ni hatua na mpanda ngazi huanzia chini', Bw. Pinda alisema mafanikio yameshaonekana katika shule za msingi, ambapo mwaka huu asilimia 100 ya wenye umri wa kuanza shule walidahiliwa.

Alisema sasa wanakabiliana na changamoto ya shule za sekondari za kata zinazokabiliwa na ongezeko kubwa la wanaojiunga shule hizo na kwamba kasi iliyopo inaonesha kuwa dhamira ya kuboresha elimu kwa ujumla, itatimia.
 
Slaa hana nafasi katika uteuzi huo.mwenye dhanmana ni Rais mwenyewe na sio mtu yeyote mwingine

Ni kweli fisadi jr. mwenye dhamana ni raisi peke yake hata dhamana ya kuwabembeleza wezi wa pesa zetu za BOT badala ya kuwawajibisha anayo yeye!!!
 
Kuna haja ya kufanya restructuring kwenye hiyo Bodi ya Mikopo! Otherwise ni uozo mtupu na nawaonea huruma sana wanafunzi wa Law School.....
 
hali sii swari tuangalie tunatakiwa kupewa nini na kwa kigezo gani. mkulima mTZ apewe awezeshwe aelimike aendele taifa.
 
hali sii swari tuangalie tunatakiwa kupewa nini na kwa kigezo gani. mkulima mTZ apewe awezeshwe aelimike aendele taifa.

Kweli mkuu!yan kwa staili hii miaka ijayo hatutopewa mikopo kabisa,hii serikali ya CCM inatunyanyasa...
 
Bodi ya mikopo hata ije na vigezo vya aina gani itakuwa ni vigumu kubadilika kama mambo ya msingi hayaguswi:

1. Wale waliosoma kwa mikopo kuna haja ya kuwekewa utaratibu warudishe. Ni rahisi bila hata hivyo vitambulisho vya taifa inawezekana. Kwa mfano ikiwekwa sheria/kanuni kwamba kila mwajiri wa Tanzania anaeajiri 'graduate' wa vyuo vikuu lazima afanye makato maalum kwa mfanyakazi huyo yatakayopelekwa TRA/MAMLAKA MPYA YA KUKUSANYA FEDHA HIZI ZA MALIPO YA MKOPO na mlipaji awe ametia saini kabisa kukubali kisheria kwamba analipa mkopo wake. Kiwe ni kiwango kidogo kinachoendana na mshahara wa mhusika.

2. Ikifanyika hivyo manake ni kuwa kutakuwa na hela toka kwa wananchi wenyewe waliowahi kuchukua mkopo, ambao watakuwa wanafadhili wanafunzi wengine. Kutakuwa na mzunguko maalum wa fedha zinazolipwa na kukopesha wanafunzi wengine. Hii ndio ilivyo kwa STUDENT LOANS COMPANY hapa Uingereza.

3. Nijuavyo ni kuwa tuna wanafunzi kidogo sana [tunahitaji vyuo vingi] ambao honestly ukiangalia kwa makini wangeweza kabisa kulipwa wote kwa asilimia mia moja bila kuathiri sekta nyingine. Kama tungekuwa tunazingatia kuwa hizi fedha ni mikopo sio misaada, niliwahi kuandika huko nyuma kuwa ukiangalia ni kama msaada kwa vile hamna utaratibu wa kurudisha. Kama wanafunzi japo elfu kumi waliowahi kupata mkopo wangekuwa wanarudisha kiasi cha shilingi elfu kumi tu kwa mwezi kila mmoja hii ingekuwa ni sawa na milioni mia moja kwa mwezi, bilioni moja nukta mbili kwa mwaka! Sasa hiki ni kiwango cha chini sana kuweka lakini tukiweka takwimu halisia ni kuwa tuna wanafunzi waliowahi kuchukua mkopo zaidi ya elfu kumi na wanaweza kulipa zaidi ya elfu kumi...

4. Kama shirika la mikopo ya wanafunzi lingefanya kazi kama mashirika ya NSSF,PSPF nk ingekuwa ni fursa nzuri kwao, wapewe mtaji kwa njia moja iweze kuwekeza na kuwakopesha wanafunzi kutoka matunda ya uwekezaji huo huku wakiendelea kukusanya malipo kwa upande mwingine.

5. Tukubali kwamba mambo ya mikopo yalipoanza hakukuwa na utaratibu mzuri wa kuchanganua nani alipwe nani asilipwe, nilipokuwa Dar miaka miwili iliyopita baadhi ya jamaa niliosoma nao Tambaza wakiwa wanafanya shahada ya pili walipewa mikopo! Kuna walakini katika mfumo huu.

6. Bado inawezekana kujipanga upya wakaweza kuanza vizuri in time for September. Vinginevyo tunaweza kuwa na vigezo vingiii lakini visisaidie...
Mawoni mazuri...naishauri bodi ya mikopo izingatie na laiti kama yakizingatiwa hakuna mwanafunzi atakayekosa mkopo.
 
Back
Top Bottom