ATM za NMB ni kero tupu

Gudboy

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
867
77
Jana nilikua pale mlimani city sasa nilikua nataka kununua kitu fulani lakini nilikua na upungufu wa pesa, sasa kwa sababu eneo hilo lina ATM nikaamua kwenda kwenye hii bank ya makabweli lakini nilipofika pale nikakuta hazifanyi kazi zote ni kwa sababu ilikua saa 12 tayari, haka kautaratibu kao ka kuzifanya out of service ni kawaida yao na hurudisha kwenye service saa 12.30 lakini jana hadi saa moja hazikua zikifanya kazi, hii ilisababisha nikose huduma niliyoitaka kwa kuwa hata maduka hufungwa saa 1. Nimesikitika sana na naomba wahakikishe huduma ni nzuri kwenye eneo hilo maana kulikua na wateja wengi sana waliokuwa wakisubiri huduma
 
Back
Top Bottom