Elections 2010 Ati hii (Picha) imekaaje?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
katika pita pita zangu nimeaona niiposti hii:

38967_411141341155_687191155_5323021_3318516_n.jpg
 
squeezed vertically. is not 1:1 scale of the actual face. It is computer edited not actual image.
 
Tuombe iwe kweli Mwanakijiji, nitakuwa na furaha ya hali ya juu kama hili hili litatokea (itafanana kabisa na ushindi wa Obama ile November, 2008) ingawaje najua kazi iliyo mbele ya Dr Slaa ni ngumu mno, lakini inawezekana kabisa. Hivi wale CCM UK waliichangia CCM, je, hapa ukumbini kama kuna watu tunataka kumchangia Dr Slaa tunaruhusiwa kufanya hivyo au "sheria za uchaguzi Tanzania" hazituruhusu?
 
Kukipiku Chama Cha CCM inataka kazi tena kazi yenyewe iwe nzito sana, sio mchezo jamani kusema ukweli CCM imeota mizizi ndani ya Serikali. Kuking'owa CCM itachukuwa muda mrefu sana itabidi vyama vya upinzani viwe kitu kimoja Viungane pasipo na kuungana hakuna chama chochote cha Upinzani kinachoweza kukishinda CCM. mimi naombea Dr Slaa awe Rais wetu wa Mwaka 2010 Mungu amsaidie Ameen.
 
Kukipiku Chama Cha CCM inataka kazi tena kazi yenyewe iwe nzito sana, sio mchezo jamani kusema ukweli CCM imeota mizizi ndani ya Serikali. Kuking'owa CCM itachukuwa muda mrefu sana itabidi vyama vya upinzani viwe kitu kimoja Viungane pasipo na kuungana hakuna chama chochote cha Upinzani kinachoweza kukishinda CCM. mimi naombea Dr Slaa awe Rais wetu wa Mwaka 2010 Mungu amsaidie Ameen.

Mkuu hili la Wapinzani kuungana wengi tungependa sana litokee lakini kama tunavyojua kwamba katika baadhi ya vyama kuna mamluki ambao kazi yao kubwa ni kuudhoofisha upinzani hivyo sijui kama hili la kuungana litafanikiwa. Na kama unavyosema CCM mizizi yake imetambaa nchi nzima na ndiyo maana Dr Slaa kumshinda Kikwete ni kazi kubwa mno hasa ukitilia maanani CCM inaweza kutumia mbinu mbali mbali na vyombo vya dola ili kujihakikishia ushindi.
 
Kuing'oa CCM ni kazi nzito ni kweli. Lakini kwa hakika watu wakiamka hakuna lisilowezekana pamoja na mtandao mkubwa CCM iliyo nao. Hebu fikirini kwa mfano mwaka 1995 kama si Mwl. Nyerere unadhani Mrema asingeunyaka Urais wa TZ? CCM ilikuwepo kama jana na leo lakini upepo ulivuma kinamna kabisa. Wamshukuru Kambarage. Hakika mwaka ule CCM ilikuwa imepoteza kiti cha Urais. Ikabidi mzee wa kifimbo kuingilia kati baada ya kuona CCM inazamishwa. Nasema: CCM inaweza kung'olewa kama wananchi wakipata mwamko wa kutosha.
 
Kuing'oa CCM ni kazi nzito ni kweli. Lakini kwa hakika watu wakiamka hakuna lisilowezekana pamoja na mtandao mkubwa CCM iliyo nao. Hebu fikirini kwa mfano mwaka 1995 kama si Mwl. Nyerere unadhani Mrema asingeunyaka Urais wa TZ? CCM ilikuwepo kama jana na leo lakini upepo ulivuma kinamna kabisa. Wamshukuru Kambarage. Hakika mwaka ule CCM ilikuwa imepoteza kiti cha Urais. Ikabidi mzee wa kifimbo kuingilia kati baada ya kuona CCM inazamishwa. Nasema: CCM inaweza kung'olewa kama wananchi wakipata mwamko wa kutosha.
Itachukuwa Muda tena Muda mrefu sana. Ukiangalia kwa undani bado wananchi wamelala tena usingizi mzito. Unajuwa CCM inafanya kampeni zake kwa walala hoi kuwapa vitu vya anasa kwa mfano kuwapa pombe, kuwasaidia matatizo madogo madogo na vivutio vingi vidogo vidogo ambavyo havina mpango wowote ule.Ukiangalia kwa makini wanachi bado wapo usingizini tena huo usingizi ni mzito sana itabidi waamke wananchi wenyewe waone ukweli wa mambo kuwa Chama cha CCM hakina mpango wowote.Ndio tunaweza kusema kuwa hapo Wanachi watakapo amka kutoka usingizini ndipo ukifanyika Uchaguzi vyama vya upinzani vyaweza kukishinda CCM. Bila ya hivyo Nchi itazidi kudidimia ikiongozwa na Chama cha CCM, na umasikini utazidi itafika nchi yetu kuwa kama Zimbabwe. Itafika wakati pesa ya hapo kwetu itakuwa kama ni karatasi kwa lugha ya kizungu wanaita (Toilet Paper) Pesa ya hapo kwetu itakuwa haina thamani kabisa tuamkeni Wanachi tuwachaguwe Viongozi wanaopenda Maendeleo ya Wanachi na Walala hoi Masikini Asanteni.
 
Kukipiku Chama Cha CCM inataka kazi tena kazi yenyewe iwe nzito sana, sio mchezo jamani kusema ukweli CCM imeota mizizi ndani ya Serikali. Kuking'owa CCM itachukuwa muda mrefu sana itabidi vyama vya upinzani viwe kitu kimoja Viungane pasipo na kuungana hakuna chama chochote cha Upinzani kinachoweza kukishinda CCM. mimi naombea Dr Slaa awe Rais wetu wa Mwaka 2010 Mungu amsaidie Ameen.

Much as I would like Dr. Slaa to lead this country, It will be extremely difficult to dislodge the incumbent CCm President as long as the current constitution is in place!! I believe what should have been done by the opposition in order to reclaim this country from the fisadi clutches, was to mobilze the citizenry to demand a constitutional change prior to holding the general elections in October!! Holding these eletions under a single-party oriented constitution does not give a chance for the opposition parties to win and hence effect the desired changes!! Good luck Dr. Slaa, it is not impossible for you to win the presidency but all the same it will not be easy should it happen!
 
Tuombe iwe kweli Mwanakijiji, nitakuwa na furaha ya hali ya juu kama hili hili litatokea (itafanana kabisa na ushindi wa Obama ile November, 2008) ingawaje najua kazi iliyo mbele ya Dr Slaa ni ngumu mno, lakini inawezekana kabisa. Hivi wale CCM UK waliichangia CCM, je, hapa ukumbini kama kuna watu tunataka kumchangia Dr Slaa tunaruhusiwa kufanya hivyo au "sheria za uchaguzi Tanzania" hazituruhusu?
Bubu,
Tunaruhusiwa kuchangia. Kuna kikundi kimeanzishwa cha Friends of Slaa (FOS) nikipata taarifa zaidi nitakuPM
 
Mh mbona naona km kuna mkono wa Chama Cha Mafisadi... Ingawa ni nzuri kwa Dr Slaa kugombea but nadhani kazi aliyonayo ni ngumu mno!!!!! Isije ikawa ni mapandikizi ya CCM yenye mpango wa kuzorotesha bunge lijalo coz km Dr SLaa atakosa urais, na ubunge ndiyo hivyo tena... Asubiri 2015 kuingia tena mjengoni..Ohoooo... mapambano yatakuwa yamezoroteshwa kwa kiasi kikubwa!!!!
 
Bubu,
Tunaruhusiwa kuchangia. Kuna kikundi kimeanzishwa cha Friends of Slaa (FOS) nikipata taarifa zaidi nitakuPM


Kwa Obama yalianza hivi hivi na dunia haikuamini yaliyotokea.

Hapa kwenye hili njamvi kunqa mwanaJF mmoja keshasema Dr. anaenda kumchachafya JK kwenye mdahalo wa viongozi wanaowania uraisi.
 
I believe in Dr. SLAA; OBAMA hata mie sikuamini tangu mwanzo; ila iliwezekana; kumbukeni ujumbe wa slaa ni rahisi sana kueleweka ndio naamini hii mieze miwili ya kampeni tosha kabisa dr kuwa rahisi; nyine subirini mtaona; ujumbe wake rahisi sana kwa watz; JK kwishney; believe or not na hawataamini CCM dk za mwisho

Changia CHADEMA kwa SMS

Chadema kwenda 15710; muda ndio huu jamani fanyeni hara hara muda unakwenda pls do it now
 
Nadhani hapa Mwanakijiji ana maanisha kwamba hii picha ina toa ujumbe gani kwa wapiga kura. Kusema ukweli sijaipenda picha. Kama mtu mmoja alivyo sema hapa kwamba picha iko squeezed. Background hawa kuchagua nzuri na Dr. Slaa yuko dressed to casual. In short it is too simplistic. Maybe Chadema ilitaka itoe ujumbe kwamba mgombea wao na chama chao ni cha watu wa hali ya kawaida but kwa upande wangu hiyo picha haimuonyeshi Dr. Slaa kama mgombea uraisi. Hata slogan wanayo itumia hapo haivutii. The public relations and media people at chadema better step their game up.

Kwa kuwa siyo viuri kukosoa bila kutoa pendekezo mi ninge shauri picha ionyeshe Dr. Slaa aki hutubia maelfu ya watu kuonyesha mvuto na uhamasishaji. Pia slogan iseme kitu kama " Ukombozi wa Watanzania." Anyway sija pata muda sana wa kuthink about it but ingekua mimi nime pewa hiyo kazi nauhakika ninge toka na kitu kizuri zaidi.
 
Nilitaka sana Dr.Slaa aendelee na ubunge maana mchango wake bungeni kwa upande wa upinzani ni muhimu sana. lkn kumngoe JK :nono: itakuwa ngumu!
 
Kukipiku Chama Cha CCM inataka kazi tena kazi yenyewe iwe nzito sana, sio mchezo jamani kusema ukweli CCM imeota mizizi ndani ya Serikali. Kuking'owa CCM itachukuwa muda mrefu sana itabidi vyama vya upinzani viwe kitu kimoja Viungane pasipo na kuungana hakuna chama chochote cha Upinzani kinachoweza kukishinda CCM. mimi naombea Dr Slaa awe Rais wetu wa Mwaka 2010 Mungu amsaidie Ameen.

Chadema iungane na TLP ?
 
na hili nalo tuliweke kwenye vichwa vyetu

WANAOPIGA KURA NI WENGINE NA WANAOCHAGUA NI WENGINE,

WANANCHI HATA TUKIMPIGIA KURA DR SLAA lAKINI TUME ISIYO HURU YA UCHAGUZI WATAMCHAGUA jK, HAPA CHA MUHIMU TUNGESISITIZA TUME HURU YA UCHAGUZI KWANZA WAKATI SLAA ANARUDI BUNGENI KUJENGA NA KUIMARISHA CV YAKE NZURI YA KIUTENDAJI NA 2015 NDIO ANGEINGIA KWENYE HUU MPAMBANO AKIWA NA MPINZANI MPYA EDDO LOWASA, AMBAYE BY THAT TIME ATAKUWA AMESHAFIFIA SANA PAMOJA NA KAMPENI ZA KINA TIDO
 
Back
Top Bottom