Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
ATCL kwaendelea kufuka moshi Send to a friend Wednesday, 23 February 2011 19:46 0diggsdigg
Gedius Rwiza
WAFANYAKAZI wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wametishia kugoma wakishinikiza uongozi wao kuondolewa na kwamba, hawamtaki Mkurugenzi wa shirika hilo, David Mattaka.
Mwananchi ilishuhudia mabishano makali kati ya uongozi wa ATCL na wafanyakazi hao, ambayo nusura yasababishe mkutano baina yao kuvunjika, baada ya wafanyakazi kutaka wanahabari waingie mkutanoni huku uongozi ukipinga na kuwatoa nje. Hatutaki mkutano wetu uwe na waandishi wa habari kama vipi tunavunja mkutano, waambie watoke nje haraka sana, alisikika akiamrisha kiongozi wa shirika hilo.
Baada ya mabishano makali na kuonekana mkutano unataka kuvunjika kwa ajili ya waandishi, waliamua kuondoka na mkutano uliendelea kama kawaida.
Hata hivyo, chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa, mada kubwa iliyojadiliwa ni kutaka kufahamu taarifa zilizotoka kwa Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu, kwani kuna baadhi ya wafanyakazi waliotumwa kwa waziri kuona kama menejimenti iliyopo itaondolewa na ikibidi shirika liundwe upya.
Kilieleza kuwa hivi sasa wafanyakazi wako tayari shirika liundwe upya, lakini wanahofia ajira zao huenda zisiendelezwe kutokana na menejimenti iliyopo ndio maana wanamtaka Mattaka kuondoka mara moja.
Kilisema aliwahi kuondolewa kutokana na shirika hilo kuonekana linadorora na baadaye alirudishwa. Tunashangaa ni kwanini mkurugenzi alirudishwa maana tangu aliporudi hakuna maendeleo yoyote, bali shirika linaendelea kudidimia siku hadi siku, kilieleza chanzo chetu.
Kilieleza kuwa kama hali itaendelea ilivyo sasa wataandamana hadi kwa Waziri Nundu kueleza kilio chao na kwamba, wanakosa maslahi yao ya msingi kutokana na menejimenti mbovu. Hata hivyo, jitihada za kuzungumza na Mattaka hazikufanikiwa baada ya mwandishi wa habari hizi kuzuiliwa kuingia ofisini kwake.
Gedius Rwiza
WAFANYAKAZI wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wametishia kugoma wakishinikiza uongozi wao kuondolewa na kwamba, hawamtaki Mkurugenzi wa shirika hilo, David Mattaka.
Mwananchi ilishuhudia mabishano makali kati ya uongozi wa ATCL na wafanyakazi hao, ambayo nusura yasababishe mkutano baina yao kuvunjika, baada ya wafanyakazi kutaka wanahabari waingie mkutanoni huku uongozi ukipinga na kuwatoa nje. Hatutaki mkutano wetu uwe na waandishi wa habari kama vipi tunavunja mkutano, waambie watoke nje haraka sana, alisikika akiamrisha kiongozi wa shirika hilo.
Baada ya mabishano makali na kuonekana mkutano unataka kuvunjika kwa ajili ya waandishi, waliamua kuondoka na mkutano uliendelea kama kawaida.
Hata hivyo, chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa, mada kubwa iliyojadiliwa ni kutaka kufahamu taarifa zilizotoka kwa Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu, kwani kuna baadhi ya wafanyakazi waliotumwa kwa waziri kuona kama menejimenti iliyopo itaondolewa na ikibidi shirika liundwe upya.
Kilieleza kuwa hivi sasa wafanyakazi wako tayari shirika liundwe upya, lakini wanahofia ajira zao huenda zisiendelezwe kutokana na menejimenti iliyopo ndio maana wanamtaka Mattaka kuondoka mara moja.
Kilisema aliwahi kuondolewa kutokana na shirika hilo kuonekana linadorora na baadaye alirudishwa. Tunashangaa ni kwanini mkurugenzi alirudishwa maana tangu aliporudi hakuna maendeleo yoyote, bali shirika linaendelea kudidimia siku hadi siku, kilieleza chanzo chetu.
Kilieleza kuwa kama hali itaendelea ilivyo sasa wataandamana hadi kwa Waziri Nundu kueleza kilio chao na kwamba, wanakosa maslahi yao ya msingi kutokana na menejimenti mbovu. Hata hivyo, jitihada za kuzungumza na Mattaka hazikufanikiwa baada ya mwandishi wa habari hizi kuzuiliwa kuingia ofisini kwake.