MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Kuhusu hali ya kifedha ya Shirika la Ndege la Taifa la ATC, Mataka alisema, lina hali mbaya kwani anaondoka na kuliacha likiwa halina hata ndege moja inayofanya safari zake.
Kwa mtaji huu mimi naona ni bora ATC ivunje nchi tujue hatuna national carrier. Kwa hali ilivyo sasa sioni sababu ya kuwepo kwa shirika hili kwa sababu zifuatazo:
1. Hatuna ndege hata moja. Unakuaje na shirika la ndege bila kuwa na ndege? Hii ni sawa na kuwa na duka bila bidhaa.
2. Rasilimali za nchi zinakwenda bure. Kama shirika halina ndege ina maana hakuna biashara ya maana. Kwa maana hiyo wafanyakazi wanalipwa pesa za bure.
3. Shirika linaonyesha udhaifu wa serikali kwa kukubali shirika la ndege lihujumiwe kwa makusudi. Serikali me dhihirisha kwamba haina nia ya kuendeleza hili shirika kwa hiyo ni bora waache kutudanganya na wavunje shirika tujue moja.