ATC ivunjwe!

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Kuhusu hali ya kifedha ya Shirika la Ndege la Taifa la ATC, Mataka alisema, lina hali mbaya kwani anaondoka na kuliacha likiwa halina hata ndege moja inayofanya safari zake.

Kwa mtaji huu mimi naona ni bora ATC ivunje nchi tujue hatuna national carrier. Kwa hali ilivyo sasa sioni sababu ya kuwepo kwa shirika hili kwa sababu zifuatazo:

1. Hatuna ndege hata moja. Unakuaje na shirika la ndege bila kuwa na ndege? Hii ni sawa na kuwa na duka bila bidhaa.

2. Rasilimali za nchi zinakwenda bure. Kama shirika halina ndege ina maana hakuna biashara ya maana. Kwa maana hiyo wafanyakazi wanalipwa pesa za bure.

3. Shirika linaonyesha udhaifu wa serikali kwa kukubali shirika la ndege lihujumiwe kwa makusudi. Serikali me dhihirisha kwamba haina nia ya kuendeleza hili shirika kwa hiyo ni bora waache kutudanganya na wavunje shirika tujue moja.
 
Kwa mtaji huu mimi naona ni bora ATC ivunje nchi tujue hatuna national carrier. Kwa hali ilivyo sasa sioni sababu ya kuwepo kwa shirika hili kwa sababu zifuatazo:

1. Hatuna ndege hata moja. Unakuaje na shirika la ndege bila kuwa na ndege? Hii ni sawa na kuwa na duka bila bidhaa.

2. Rasilimali za nchi zinakwenda bure. Kama shirika halina ndege ina maana hakuna biashara ya maana. Kwa maana hiyo wafanyakazi wanalipwa pesa za bure.

3. Shirika linaonyesha udhaifu wa serikali kwa kukubali shirika la ndege lihujumiwe kwa makusudi. Serikali me dhihirisha kwamba haina nia ya kuendeleza hili shirika kwa hiyo ni bora waache kutudanganya na wavunje shirika tujue moja.
Mimi nashauri kifanyike kitu kama tulivyofanya CRDB. kwa kuuza hisa kwa wananchi kiasi fulani hapo tutapata mtaji mzuri na shirika tutakuwa tunalimiliki wenyewe. Haya ndio yangu. Nawasilisha.
 
Ivunjwe! Utavunja nini wakati unachota kukivunja hakipo? You must be kidding!

Nikisema ivunjwe namaanisha rasmi mkuu maana hicho unacho sema hakipo bado kina wafanya kazi na kina tugharimu watanzania.
 
ni kweli livunjwe kwani kama huna ndege sasa unafanya nini,lengo la kuwa na shirika la ndege ni nini? hii ni aibu sana,
ok sasa huo mshahara unawalipa kwa kufanya kazi gani? usafilishi abiria,usafirishi mizigo,huna lolote haina maana kuwa na shilika mfu bora life tu
 
Muulizeni Kikwete inakuwaje Kagame wa juzi juzi tu ameweza yeye wa miaka 50 ameshindwa?
 
Swali linatakiwa liende kwa Mkapa na Kikwete, tuwaulize
1. Kwanini ATC haina hata ndege moja?
2. Tuwaelimishe kabisa kwa kuwaambia uamuzi wenu wa kuiuza ATC na imekufa kwa matunda ya maamuzi yenu upo wazi kabisa!
 
Nikisema ivunjwe namaanisha rasmi mkuu maana hicho unacho sema hakipo bado kina wafanya kazi na kina tugharimu watanzania.

muuu hata kuvunja kutagharimu.

kuvunjwa ni kweli inatakiiwa ivunjwe kisiasa maana kiuchumi na kistrategic ishavunjika.

its time wahusika waweke effort na nguvu zao zote kwenye reli kwa miaka 15 or20 yrs ijayo

kwa hali tuliyonayo , strategically kiuchumi hata ajira reli ina umihumu mkubwa kuliko anga but priority zetu zimekuwa always wrong kuhusu reli vs anga.
 
Kama hakuna ndege ni ajabu, watakuwa wame privatise ndege na sio shirika!
 
Kuvunjwa mie naona ndiyo bora zaidi! Juzieti walienda kuanzisha MRADI ENDELEVU WA MAZINGIRA BUNGE PR SCHOOL kwa kupanda miti ikiwa ni sehemu ya Corporate Social Responsibility! Nilijiuliza maswali mengi kuwa hawa jamaa wanapata muda wa kwenda kupanda miti kwa kuwa hakuna shughuli nyingine YA MSINGI ya kufanya ofisini au ni CSP kiukweli??Baada ya hotuba ya Mataka nimepata uhakika kuwa kweli ofisini hakuna shughuli ingine (labda uhasibu kushughulikia mishahara) Sisis kama walipa kodi hawa waajiriwa wa ATC tunawalipa kwa shughuli gani wanayofanya??Vunja shirika..Serikali ikubali imeshindwa waache Private operators waendelee na biashara!!! Hata cha kuuza hakuna kama hata ndege moja hakuna!! Waati Majembe wauze furniture zao (kama bado zipo) walipe mafao mafanyakazi na jengo liuzwe na kutumika kupipia madeni yanayowakabili kama shirika!!!!! Mashirika mengine yalikufa na kuzikwa na tushayasahau; itakuwa ATC!!!!! So frustrating!!!!
 
Ni kweli kabisa. Fedha tunazo tumia kuhudumia mfu ni bora zingekwenda kwingine. Hata kama kuvunja itakua nayo ina gharama yake ni bora kwa sababu itakua gharama ya wakati mmoja kuliko hizi gharama za kila siku zisizo na maana. Inasikitisha jinsi nchi hii inavyoendeshwa kiswahili kila sekta. Yani tuna dharauliwa sana Watz.
 
Wakitaka National Carrier ni bora hata wakanunua hisa kidogo Precision - wakajivunia hiyo kama National Carrier. Ili mradi wasiingilie utawala/uendeshaji wake. Waachane kabisa na hii kitu inaitwa ATC
 
Back
Top Bottom