Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Naomba kuuliza huyu Lameck Airo ndo mwenye Lacairo Hotel Mwanza Kirumba?
Mbunge wa sasa wa jimbo Rorya, Prof. Phillemon Sarungi.
Lameck Airo ametangaza nia ya kugombea ubunge ili kushindana na baba yake mdogo kupitia Chama Cha Mapindizi (CCM) katika jimbo la Rorya mkoani Mara.
Airo ambaye ni diwani wa kata ya Koryo (CCM) na kamanda wa vijana wa wilaya ya Rorya ni mtoto wa mdogo wake mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Prof. Phillemon Sarungi.
Ingawa hajatangaza nia, kuna kila dalili kwamba Sarungi ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 10, atatetea tena kiti chake.
Airo alitangaza uamuzi huo katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa jumuia ya wanawake wa chama hicho (UWT) ikiwa ni mara yake ya pili kutangaza nia hiyo.
Alisema kama mwana-CCM ni haki yake ya msingi kujitokeza kugombea ubunge katika jimbo hilo ili aweze kutoa mchango wake wa kuharakisha maendeleo.
Alisema kwa muda mrefu alikuwa mpiga debe mkubwa kwa mgombea wa CCM ambaye ni baba yake mkubwa, hivyo ni wakati wake sasa na yeye kupigiwa debe.
Akifungua mkutano huo, Airo ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliwataka wanawake wa chama hicho kuunganisha nguvu zao pamoja katika kuhakikisha chama hicho kinaibuka na ushindi wa kimbunga kwa nafasi za Udiwani, Ubunge na Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
Akitoa salamu za serikali za wilaya hiyo, mkuu wa wilaya ya Rorya, Kanali mstaafu Benedict Kitenga, alisema kuwa serikali ya wilaya yake inasikitishwa na mila za wakazi wa wilaya ya Rorya kuwakandamiza wanawake kwa kushindwa kuwapa nafasi za maamuzi hasa za kugombea uongozi.
Mimi nawaomba hali hii ninayoiona hapa kwetu ya kuwatenga wanawake kwa kushindwa kuwapa nafasi za maamuzi itasababisha tusifikie kauli yetu ya uwakilishi wa 50 kwa 50. Nawa ombeni tubadilike ili wanawake wawezeshwe na wakiwezeshwa wanaweza, alisema kanali Kitenga
CHANZO: NIPASHE
Atangaza kumvaa baba yake kwenye ubunge
Mbunge wa sasa wa jimbo Rorya, Prof. Phillemon Sarungi.
Lameck Airo ametangaza nia ya kugombea ubunge ili kushindana na baba yake mdogo kupitia Chama Cha Mapindizi (CCM) katika jimbo la Rorya mkoani Mara.
Airo ambaye ni diwani wa kata ya Koryo (CCM) na kamanda wa vijana wa wilaya ya Rorya ni mtoto wa mdogo wake mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Prof. Phillemon Sarungi.
Ingawa hajatangaza nia, kuna kila dalili kwamba Sarungi ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 10, atatetea tena kiti chake.
Airo alitangaza uamuzi huo katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa jumuia ya wanawake wa chama hicho (UWT) ikiwa ni mara yake ya pili kutangaza nia hiyo.
Alisema kama mwana-CCM ni haki yake ya msingi kujitokeza kugombea ubunge katika jimbo hilo ili aweze kutoa mchango wake wa kuharakisha maendeleo.
Alisema kwa muda mrefu alikuwa mpiga debe mkubwa kwa mgombea wa CCM ambaye ni baba yake mkubwa, hivyo ni wakati wake sasa na yeye kupigiwa debe.
Akifungua mkutano huo, Airo ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliwataka wanawake wa chama hicho kuunganisha nguvu zao pamoja katika kuhakikisha chama hicho kinaibuka na ushindi wa kimbunga kwa nafasi za Udiwani, Ubunge na Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
Akitoa salamu za serikali za wilaya hiyo, mkuu wa wilaya ya Rorya, Kanali mstaafu Benedict Kitenga, alisema kuwa serikali ya wilaya yake inasikitishwa na mila za wakazi wa wilaya ya Rorya kuwakandamiza wanawake kwa kushindwa kuwapa nafasi za maamuzi hasa za kugombea uongozi.
Mimi nawaomba hali hii ninayoiona hapa kwetu ya kuwatenga wanawake kwa kushindwa kuwapa nafasi za maamuzi itasababisha tusifikie kauli yetu ya uwakilishi wa 50 kwa 50. Nawa ombeni tubadilike ili wanawake wawezeshwe na wakiwezeshwa wanaweza, alisema kanali Kitenga
CHANZO: NIPASHE