Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kama kuna kitu kinakera ni kuona watu wakitaka CCM iwe Manusura wa kimbunga cha mabadiliko ya kisiasa na kijamii kinachovuma nchini. Watu hao bila kujijua au kwa makusudi au kwa kusukumwa na hofu zao dhidi ya mabadiliko wamekuwa wakihimiza CCM ijerekebishe au wakitaka CCM isimamishe mgombea "anayefaa" kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
kila CCM ikichagua viongozi wanaoonekana kuwa "wabovu" au hawafai utasikia watu hao wakilalamika ni kwa nini CCM imeendelea kuchagua viongozi wabovu wasiofaa. Na kila mara huwataka wale walio "wasafi" watoke CCM na kujiunga na M4C kama vile hawaoni faida kwa taswira inayopatikana kwa watu hao kubaki, CCM kwani wanajenga taswira kwamba watu safi hawatakiwi ndani ya chama hicho hivyo kuvipa faida ya kuaminiwa vyama vingine.
Mtu yeyote anayesikitika kwa kufa kwa CCM basi ajue hasikitiki kwa kufa kwa Tanzania. Ili Tanzania iwe salama ni lazima CCM itoke madarakani na ili CCM itoke madarakani ni lazima iwe dhaifu na ili iwe dhaifu ni lazima iongozwe na viongozi wabovu wala na watoa rushwa, Mafisadi na vibaraka wa mfumo wa Ubepari uchwara. Anayetaka CCM iwe Imara haitakii mema Tanzania!!
kila CCM ikichagua viongozi wanaoonekana kuwa "wabovu" au hawafai utasikia watu hao wakilalamika ni kwa nini CCM imeendelea kuchagua viongozi wabovu wasiofaa. Na kila mara huwataka wale walio "wasafi" watoke CCM na kujiunga na M4C kama vile hawaoni faida kwa taswira inayopatikana kwa watu hao kubaki, CCM kwani wanajenga taswira kwamba watu safi hawatakiwi ndani ya chama hicho hivyo kuvipa faida ya kuaminiwa vyama vingine.
Mtu yeyote anayesikitika kwa kufa kwa CCM basi ajue hasikitiki kwa kufa kwa Tanzania. Ili Tanzania iwe salama ni lazima CCM itoke madarakani na ili CCM itoke madarakani ni lazima iwe dhaifu na ili iwe dhaifu ni lazima iongozwe na viongozi wabovu wala na watoa rushwa, Mafisadi na vibaraka wa mfumo wa Ubepari uchwara. Anayetaka CCM iwe Imara haitakii mema Tanzania!!