Che Guevara
JF-Expert Member
- May 22, 2009
- 1,236
- 346
Mwananchi, Tuesday, 18 May 2010 21:36
Anna Kinkande na Naomi Maeda, MSJ
DUNIANI kuna mambo. Ukishangaa ya Mussa, utayaona ya firauni.
Ndivyo unavyoweza kujisemea moyoni mara baada ya kusikia mkasa wa mkazi mmoja wa jijini Dar es salaam ambaye jana alifika mahakamani kutaka ndoa yake ivunjwe kwa madai kuwa amebaini mkewe ni kikongwe.
Mkazi huyo, Peter Nyoni, 39, amefungua kesi Mahakama ya Mwanzo ya Buguruni akitaka chombo hicho cha sheria kimruhusu kumpa talaka mkewe, Sara Kweka, akidai kuwa mwanamke huyo alimdanganya wakati wakioana.
Nyoni anadai katika kesi hiyo kuwa mbali na mwanamke huyo kumdanganya, pia amekuwa akitishia kumtoa uhai kila anapomueleza suala la kumpa talaka.
Kesi hiyo ya aina yake na nadra kwa mwanamke kuiomba mahakama imruhusu kutoa talaka, ilivuta hisia za wengi jana wakati ilipofikishwa mbele ya Hakimu Anthony Sanchole wa mahakama hiyo.
Nyoni aliiambia mahakama hiyo kuwa mwanamke huyo, ambaye alimuoa mwaka 2002, alimweleza wakati wanakutana kwa mara ya kwanza kuwa yeye bado ni mbichi na hakuwahi kuzaa.
Mume huyo alidai kuwa baada ya miaka minane aligundua kuwa mkewe hakuwa kigori na kwamba alishazaa na tayari ana wajukuu watano na hivyo akaamua kuachana naye.
Lakini Nyoni alisema amekuwa akishindwa kutekeleza azma yake ya kumpa talaka nyumbani kwao kwa kuwa mwanamke huyo amekuwa akimtishia kumuua kila wakati suala hilo linapoibuka.
"Amekuwa pia ananiambia kuwa nikimwacha atanifanyia kitendo kibaya cha kunitoa duniani," Nyoni alidai mahakamani hapo.
Awali karani wa mahakama hiyo, Mwanabibi Ramadhani alisema kuwa mtuhumiwa alitishia kumuua mumewe Mei 14, mwaka huu wakati wakiwa maeneo ya Buguruni Chama.
Alisema Sara amekuwa akitoa vitsho hivyo baada ya mumewe kutaka kumpa talaka baada ya kugungua kuwa mkewe si mkweli katika ndoa yao.
Hakimu Sanchole aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 28 mwaka huu itakapotajwa tena.
Anna Kinkande na Naomi Maeda, MSJ
DUNIANI kuna mambo. Ukishangaa ya Mussa, utayaona ya firauni.
Ndivyo unavyoweza kujisemea moyoni mara baada ya kusikia mkasa wa mkazi mmoja wa jijini Dar es salaam ambaye jana alifika mahakamani kutaka ndoa yake ivunjwe kwa madai kuwa amebaini mkewe ni kikongwe.
Mkazi huyo, Peter Nyoni, 39, amefungua kesi Mahakama ya Mwanzo ya Buguruni akitaka chombo hicho cha sheria kimruhusu kumpa talaka mkewe, Sara Kweka, akidai kuwa mwanamke huyo alimdanganya wakati wakioana.
Nyoni anadai katika kesi hiyo kuwa mbali na mwanamke huyo kumdanganya, pia amekuwa akitishia kumtoa uhai kila anapomueleza suala la kumpa talaka.
Kesi hiyo ya aina yake na nadra kwa mwanamke kuiomba mahakama imruhusu kutoa talaka, ilivuta hisia za wengi jana wakati ilipofikishwa mbele ya Hakimu Anthony Sanchole wa mahakama hiyo.
Nyoni aliiambia mahakama hiyo kuwa mwanamke huyo, ambaye alimuoa mwaka 2002, alimweleza wakati wanakutana kwa mara ya kwanza kuwa yeye bado ni mbichi na hakuwahi kuzaa.
Mume huyo alidai kuwa baada ya miaka minane aligundua kuwa mkewe hakuwa kigori na kwamba alishazaa na tayari ana wajukuu watano na hivyo akaamua kuachana naye.
Lakini Nyoni alisema amekuwa akishindwa kutekeleza azma yake ya kumpa talaka nyumbani kwao kwa kuwa mwanamke huyo amekuwa akimtishia kumuua kila wakati suala hilo linapoibuka.
"Amekuwa pia ananiambia kuwa nikimwacha atanifanyia kitendo kibaya cha kunitoa duniani," Nyoni alidai mahakamani hapo.
Awali karani wa mahakama hiyo, Mwanabibi Ramadhani alisema kuwa mtuhumiwa alitishia kumuua mumewe Mei 14, mwaka huu wakati wakiwa maeneo ya Buguruni Chama.
Alisema Sara amekuwa akitoa vitsho hivyo baada ya mumewe kutaka kumpa talaka baada ya kugungua kuwa mkewe si mkweli katika ndoa yao.
Hakimu Sanchole aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 28 mwaka huu itakapotajwa tena.