Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Jamaa mmoja akiwa na mizigo mingi bandarini dar,alikodi boti zima kuelekea Zanzibar.Safari ilianza vizuri tu,lakini walipofika katikati ya bahari,jamaa akaamuru boti isimame kidogo.Kwa mshangao wa nahodha,yule jamaa akaanza kutupa kitu kimoja baada ya kingine(magunia ya mchele,sukari,mafuta ya kupikia n.k) baharini akidai ndo kafika mwisho wa safari.Wakati nahodha akiwa mdomo wazi,yule jamaa akamwambia;'nisubiri nikakuchukulie pesa yako ya nauli nyumbani kwangu,nitarudi baada ya dakika 3,kisha akajitosa na kuzama baharini.Ungekuwa wewe ndo nahodha ungefanyaje?ungesubiri pesa yako au ndo spidi 240 kurudi bara?