Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Jamaa wawili wakitoka matembezini saa 6 usiku waliamua kutumia njia ya mkato kupitia makaburini kurudi makwao.Wakiwa katikati ya graveyard mara wakasikia mlio kama mtu anagonga kitu,tap-tap,jamaa wakapata woga wasijue la kufanya.Mara wakamkuta babu mmoja akiwa na nyundo na chisel(chizo) akichonga maandishi kwenye kaburi.Mmoja wao akasema,"aah! kumbe ni wewe babu,tulifikiri ni mzimu,mbona unafanya kazi usiku namna hii?". Babu akajibu,"washenzi hawa,walikosea spelling za jina langu!".