KUTOKANA na kukua kwa kasi kwa tamaduni za nchi mbalimbali hasa za Magharibi nchini, Serikali imetakiwa kuwa makini na baadhi ya tamaduni hizo kwani zimeonekana kuharibu kwa kiasi kikubwa maadili na sifa ya nchi hasa kwa vijana walio wengi.
Kauli hiyo imetolewa leo na Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Jimbo la Kilimanjaro, Glorius Shoo, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mmomonyoko wa maadili hasa vitendo vya ushoga ulioshika kasi hivi sasa.
Askofu Shoo amesema, ni jambo la aibu na ni dhambi kubwa kwa watu wanaojiita mashoga na kutaka kutambuliwa na Serikali tena kupewa haki na heshima huku wakijua mapenzi ya jinsi moja ni chukizo kwa Mungu kwani huo haukuwa mpango wake tangu alipoumba dunia.
Jambo hili ni la kusikitisha, tena la aibu kubwa tumekuwa tunasikia mara nyingi watu wanaibuka na tena bila aibu wanajitangaza kuwa wanashiriki mapenzi ya jinsi moja ila cha ajabu hawachukuliwi hatua zozote, amesema Askofu Shoo.
Amesema, ushoga (mapenzi ya jinsi moja) ni kinyume cha utaratibu ila cha ajabu anashangazwa na mashoga hao kudai kutambuliwa katika Katiba mpya, jambo alilosema linaipeleka dunia pabaya.
Askofu amesema, baadhi ya nchi masikini zimekuwa zikiingia mikataba ambayo pengine athari zake ni pamoja na kuwepo kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja katika jamii ambao bila hofu ya Mungu, sasa imefikia mahali wanadai kutambuliwa kikatiba.
Askofu Shoo amesema ,Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kutokana na watu wake kuwa waadilifu pamoja na kumtii Mungu ila kundi la watu wachache wanaitia doa kwa kujiita mashoga, hivyo kutaka Serikali kutoa tamko juu ya jambo hilo kwani kwa kunyamaza, mashoga hao watajipa moyo kuwa Serikali inawathamini na kuwatambua.
sosi " Habari Leo"
Sheria zimekuwepo kuhusiana na mapenzi ya jinsi moja ila sasa zinaonekana kukosa nguvu au kukiukwa wazi wazi kwani sheria ya kujamiana watu wa jinsi moja hapo awali ilikuwa ni kifo japokuwa sheria hiyo inaonekana kutokufanya kazi hivi sasa, alisema.
Kauli hiyo imetolewa leo na Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Jimbo la Kilimanjaro, Glorius Shoo, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mmomonyoko wa maadili hasa vitendo vya ushoga ulioshika kasi hivi sasa.
Askofu Shoo amesema, ni jambo la aibu na ni dhambi kubwa kwa watu wanaojiita mashoga na kutaka kutambuliwa na Serikali tena kupewa haki na heshima huku wakijua mapenzi ya jinsi moja ni chukizo kwa Mungu kwani huo haukuwa mpango wake tangu alipoumba dunia.
Jambo hili ni la kusikitisha, tena la aibu kubwa tumekuwa tunasikia mara nyingi watu wanaibuka na tena bila aibu wanajitangaza kuwa wanashiriki mapenzi ya jinsi moja ila cha ajabu hawachukuliwi hatua zozote, amesema Askofu Shoo.
Amesema, ushoga (mapenzi ya jinsi moja) ni kinyume cha utaratibu ila cha ajabu anashangazwa na mashoga hao kudai kutambuliwa katika Katiba mpya, jambo alilosema linaipeleka dunia pabaya.
Askofu amesema, baadhi ya nchi masikini zimekuwa zikiingia mikataba ambayo pengine athari zake ni pamoja na kuwepo kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja katika jamii ambao bila hofu ya Mungu, sasa imefikia mahali wanadai kutambuliwa kikatiba.
Askofu Shoo amesema ,Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kutokana na watu wake kuwa waadilifu pamoja na kumtii Mungu ila kundi la watu wachache wanaitia doa kwa kujiita mashoga, hivyo kutaka Serikali kutoa tamko juu ya jambo hilo kwani kwa kunyamaza, mashoga hao watajipa moyo kuwa Serikali inawathamini na kuwatambua.
sosi " Habari Leo"
Sheria zimekuwepo kuhusiana na mapenzi ya jinsi moja ila sasa zinaonekana kukosa nguvu au kukiukwa wazi wazi kwani sheria ya kujamiana watu wa jinsi moja hapo awali ilikuwa ni kifo japokuwa sheria hiyo inaonekana kutokufanya kazi hivi sasa, alisema.