Askofu Pengo na Balozi Ndobho wamjibu Nape

Mkuu maneno sawa kabisa kwa mtazamo wako na ndio maana mimi sikuwa Mkristu kwa sababu sikubaliani na imani hiyo..
Kwa hiyo maadam mimi sikubaliani sintopenda kumsikia Pengo akizungumzia swala linalonihusu mimi hali sikubaliani na imani yake. Nitakupa Mfano mdogo sana.. Ktk Ukristu jitu linaweza kuua hadharani likakimbilia kanisani na likapewa hifadhi tena Askofu alitoe hata ushahidi dhidi ya hilo jambazi kwa sababu limeungama.. Hii ni imani yenu na naiheshimu lakini sikubaliani nayo kabisa na ndio maana sikuwa mkristu kwa sababu naamini jambazi ni jambazi lilikimbilia kanisani litolewe na kutupwa ndani hakuna kinga kama tunavyodai JK awaondolee kinga hawa Mafisadi na huyo Pengo mwenyewe analikubali hilo.. sasa iweje yeye atake kuwapa kinga hawa jamaa hali alichosema Nape ni kwamba hawa Mafisadi wanataka kukimbilia makanisani ili wasafishwe?

Sasa basi maadam hii ni ibada ya dini yenu, sisi tutaiheshimu na mnaitumia sana kuwalinda hata wahalifu maana wamekuja kutubu lakini usiiweke hii ibada yako kuwa ya kila Mtanzania na kinga kwa hata Mafisadi ambao hawatakiwi ktk uongozi wa jamii.

Mkitaka wasafisheni na wabakie raia wa kawaida tu lakini mnapotaka kuwasafisha ili warudi kisiasa hapo mtakuwa mnaniingilia hata mimi ktk imani yangu kwamba jambazi linastahili jela tu hata kama likikimbilia msikitini litolewe na kukabidhiowa vyombo vya serikali..

Ya Kaizali aachiwe Kaizali, dini zinapoingilia ya Kaizali nina haki ya kuyapiga vita kwani hata Biblia imetukanya.. Kardinal Pengo anatakiwa kufahamu hilo
Mkandara

Nafikiri umejijibu mwenyewe kuwa ndiyo maana hukuwa mkristo kwa hiyo waache wakristo wawapokee wenye dhambi kama dini yao inavyoelekeza, hata kiongozi wa wakristo (Yesu) alikuja kwa kondoo waliopotea si kwa waliokundini. Halafu usitake kupotosha kuwa Pengo anataka kuwakinga mafisadi (Mkandara JF ni waelewa) anachotaka Pengo ni kuwapa toba ya dhambi kiroho si kusafisha ufisadi, kama wewe una ushahidi bado unaruhusiwa kuwafikisha mahakamani hata baada ya toba.
 
Mkandara

Nafikiri umejijibu mwenyewe kuwa ndiyo maana hukuwa mkristo kwa hiyo waache wakristo wawapokee wenye dhambi kama dini yao inavyoelekeza, hata kiongozi wa wakristo (Yesu) alikuja kwa kondoo waliopotea si kwa waliokundini. Halafu usitake kupotosha kuwa Pengo anataka kuwakinga mafisadi (Mkandara JF ni waelewa) anachotaka Pengo ni kuwapa toba ya dhambi kiroho si kusafisha ufisadi, kama wewe una ushahidi bado unaruhusiwa kuwafikisha mahakamani hata baada ya toba.
Mkuu sasa wewe ndio umekuwa msemaji wa Pengo?

Soma aliyoyasema Nape Mnauye, kisha yachukue majibu ya Pengo kujibu hoja ya Nape...sikutunga mimi hadithi hii ila nimewasoma wote.
Na maadam unakubali kwamba mimi Muislaam na ndio sababu sikuwa Mkristu, namwomba Pengo asijewasafisha watu hawa warudi kutafuta kutawala hata kama inakubalika ktk imani yako na ndicho hiki kitapelekea mimi kuamini kwamba kweli kanisa ndio linatawala nchi.
Utanisamehe kama hukunisoma vizuri ukakurupuka tena kutoa hukumu...
 
Mkuu sasa wewe ndio umekuwa msemaji wa Pengo?

Soma aliyoyasema Nape Mnauye, kisha yachukue majibu ya Pengo kujibu hoja ya Nape...sikutunga mimi hadithi hii ila nimewasoma wote.
Na maadam unakubali kwamba mimi Muislaam na ndio sababu sikuwa Mkristu, namwomba Pengo asijewasafisha watu hawa warudi kutafuta kutawala hata kama inakubalika ktk imani yako na ndicho hiki kitapelekea mimi kuamini kwamba kweli kanisa ndio linatawala nchi.
Utanisamehe kama hukunisoma vizuri ukakurupuka tena kutoa hukumu...
Hivi wewe unajua maana ya toba au unasema unavyojua wewe, toba haikuondolei kosa kama wewe ni mwizi utabaki kuwa mwizi ila kiroho utakuwa umekiri mbele ya mwenyezi Mungu na Pengo yuko kiroho zaidi si kimwili. Sasa nyie mnaolazimisha kimwili/kisiasa ndio mnaotakiwa kuwapeleka mahakamani si Pengo.
 
Hivi wewe unajua maana ya toba au unasema unavyojua wewe, toba haikuondolei kosa kama wewe ni mwizi utabaki kuwa mwizi ila kiroho utakuwa umekiri mbele ya mwenyezi Mungu na Pengo yuko kiroho zaidi si kimwili. Sasa nyie mnaolazimisha kimwili/kisiasa ndio mnaotakiwa kuwapeleka mahakamani si Pengo.
Mkuu soma tena nilichoandika na kinnacho zungumziwa hapa. Aidha Pengo na wewe hamkumweleza Nape au ndio imani yenu inasema hivyo.

Kumsafisha mtu na uchafu alofanya ni somo jingine kabisa na toba kwani anachozungumzia Nape ni hawa MAFISADI kuwatumia viongozi wa dini KUJISAFISHA..Pengo kakuruka na kusema hawezi kuwakataa ikiwa ni waumini wake ni ktk maana ile ile ya kuwasafisha mafisadi iwe kiroho au kimwili maana makosa yao yapo kimwili na ndicho kinachozungumzwa hapa. Hakuna mtu mwenye roho mbaya (kiroho) akawa na matendo mazuri (kimwili). matendo yako ndio tafsiri ya roho yako.
Na nitahoji pia, kama Sheikh mkuu atajitokeza na kusema au kupinga hoja ya Nape kwa kuitumia dini kumsafisha Rostam sidhani kama utakuwa na majibu haya haya..
 
Mkuu soma tena nilichoandika na kinnacho zungumziwa hapa. Aidha Pengo na wewe hamkumweleza Nape au ndio imani yenu inasema hivyo.

Kumsafisha mtu na uchafu alofanya ni somo jingine kabisa na toba kwani anachozungumzia Nape ni hawa MAFISADI kuwatumia viongozi wa dini KUJISAFISHA..Pengo kakuruka na kusema hawezi kuwakataa ikiwa ni waumini wake ni ktk maana ile ile ya kuwasafisha mafisadi iwe kiroho au kimwili maana makosa yao yapo kimwili na ndicho kinachozungumzwa hapa. Hakuna mtu mwenye roho mbaya (kiroho) akawa na matendo mazuri (kimwili). matendo yako ndio tafsiri ya roho yako.
Na nitahoji pia, kama Sheikh mkuu atajitokeza na kusema au kupinga hoja ya Nape kwa kuitumia dini kumsafisha Rostam sidhani kama utakuwa na majibu haya haya..
‘Waislamu msikate tamaa kwenye elimu dunia'

na Abdallah Khamis (Tanzania daima) April 26, 2011.

WAISLAMU nchini kote wameshauriwa kutokata tamaa katika kujiendeleza kielimu hususan ya dunia ili kukabiliana na mabadiliko yanayojitokeza kila siku katika maisha yao.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Naibu Balozi wa Pakistan nchini Najib Burani alipokuwa akizindua tamasha la siku moja la usomaji wa vitabu vya Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Almuntanzir.

Burani alisema ufike wakati kwa Muislamu kutambuliwa kwa matendo yake na si kwa jina kama ilivyo sasa ambapo wengi wao wanajiita Waislamu bila kufuata maagizo ya dini hiyo.

"Uislamu unahimiza watu kujitafutia elimu kwa maana hiyo unapingana na ujinga… ni jukumu letu Waislamu kusoma ili tuepuke kuwa wasindikizaji katika kila jambo kwa kuwa kitabu chenu kina muongozo wa mambo yote yanayotendeka duniani," alisema naibu balozi huyo.

Aliongeza kusema kuwa mambo mengi yamegunduliwa katika ulimwengu wa leo baada ya watu kusoma na kufanya tafiti mbalimbali kupitia elimu zao.

Nae Sheikh Said Abri akichangia mada katika tamasha hilo alisema ni jambo la kusikitisha kuona Watanzania hawana mazoea ya kujisomea vitabu na magazeti kwa lengo la kujiongezea elimu.

Alisema ili mtu awe kiongozi kwa viumbe wengine, lazima awe na elimu ya kutawala mazingira yake na ifike wakati wa kuukataa msemo wa kwamba ukitaka kumficha Mtanzania jambo muhimu liweke kwenye kitabu.

Mratibu wa tamasha hilo la siku moja Abdulkarim Ahmed alisema wanatarajia kuwa na tamasha la aina hiyo kila mwaka.
 
‘Waislamu msikate tamaa kwenye elimu dunia'

na Abdallah Khamis (Tanzania daima) April 26, 2011.

WAISLAMU nchini kote wameshauriwa kutokata tamaa katika kujiendeleza kielimu hususan ya dunia ili kukabiliana na mabadiliko yanayojitokeza kila siku katika maisha yao.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Naibu Balozi wa Pakistan nchini Najib Burani alipokuwa akizindua tamasha la siku moja la usomaji wa vitabu vya Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Almuntanzir.

Burani alisema ufike wakati kwa Muislamu kutambuliwa kwa matendo yake na si kwa jina kama ilivyo sasa ambapo wengi wao wanajiita Waislamu bila kufuata maagizo ya dini hiyo.

"Uislamu unahimiza watu kujitafutia elimu kwa maana hiyo unapingana na ujinga… ni jukumu letu Waislamu kusoma ili tuepuke kuwa wasindikizaji katika kila jambo kwa kuwa kitabu chenu kina muongozo wa mambo yote yanayotendeka duniani," alisema naibu balozi huyo.

Aliongeza kusema kuwa mambo mengi yamegunduliwa katika ulimwengu wa leo baada ya watu kusoma na kufanya tafiti mbalimbali kupitia elimu zao.

Nae Sheikh Said Abri akichangia mada katika tamasha hilo alisema ni jambo la kusikitisha kuona Watanzania hawana mazoea ya kujisomea vitabu na magazeti kwa lengo la kujiongezea elimu.

Alisema ili mtu awe kiongozi kwa viumbe wengine, lazima awe na elimu ya kutawala mazingira yake na ifike wakati wa kuukataa msemo wa kwamba ukitaka kumficha Mtanzania jambo muhimu liweke kwenye kitabu.

Mratibu wa tamasha hilo la siku moja Abdulkarim Ahmed alisema wanatarajia kuwa na tamasha la aina hiyo kila mwaka.
ndio wanitukana au?
 
Nape ni Vuvuzela tu la Membe!

Ama kweli watu humu ndani mmelogwa. Ghafla wale waliokuwa wachafu leo hii wanashangiliwa kama vile mashujaa. Nape anachofanya ni kuutangazia umma yale yaliyojiri na kuamuliwa na NEC lakini kwa vile vita dhidi ya ufisadi ulikuwa ni mtaji wa baadhi ya wanasiasa kupata kisingizio cha maandamano na kupata uungwaji mkono sasa vita hivi vinapingwa na wale wale waliojifanya ni vinara. Leo Nape ni Vuvuzela la Membe, na je Malecela au wale wengine ambao wanazungumzia matatizo ya hawa mapacha watatu?

Nimeamini kweli kwamba mafisadi wana mbinu na very soon, tutaambiwa kwamba mafisadi hawa wanaandamwa kwa sababu za kidini. Leo hii haisahngazi gazeti la Mtanzania ambalo humu ndani lilikuwa halina heshima yoyote kutokana na habari zake zenye gilba na zilizochuja ndiyo linatumika kunukuu watu selectively and out of context mradi tu malengo ya wakubwa hawa yanafanikiwa. Ndilo gazeti hili hili na Rai yaliyokuwa yanaandama maisha binafsi ya Slaa na kuposha kwa kiasi kikubwa sana hoja mbalimbali zilizokuwa zinatolewa wakati wa kampeni za uchaguzi. Ndoa hii ya mafisadi na walikouwa wapiganaji inatuacha na maswali mengi lakini lililo dhahiri ni kwamba hakukuwa na nia thabiti ya kupambana na ufisadi na sasa watu wana hasira za kunyang'anywa hoja na sasa wamekuja juu.
 
Hii mistari katika biblia ina maana gani?
1.Mwenye vingi ataongezewa
2.Akupigae kofi upande wa kushoto mgeuzie na wakulia

Je pengo ataweza kuwarekebisha kweli? au atawatia sumu zaidi ya kutuibia?

Ina maana dini yako ndio inavokuelekeza? Kwamba ukiiba utaongezewa au ni nini unauliza?

Kwani hio sumu ya kuiba waliichukulia kwa Pengo tokea siku ya kwanza?? Maamuzi ya kuanza,kuacha,kuendelea na ufisadi yapo zaidi ndani ya nafsi zao.
 
Ama kweli watu humu ndani mmelogwa. Ghafla wale waliokuwa wachafu leo hii wanashangiliwa kama vile mashujaa. Nape anachofanya ni kuutangazia umma yale yaliyojiri na kuamuliwa na NEC lakini kwa vile vita dhidi ya ufisadi ulikuwa ni mtaji wa baadhi ya wanasiasa kupata kisingizio cha maandamano na kupata uungwaji mkono sasa vita hivi vinapingwa na wale wale waliojifanya ni vinara. Leo Nape ni Vuvuzela la Membe, na je Malecela au wale wengine ambao wanazungumzia matatizo ya hawa mapacha watatu?

Nimeamini kweli kwamba mafisadi wana mbinu na very soon, tutaambiwa kwamba mafisadi hawa wanaandamwa kwa sababu za kidini. Leo hii haisahngazi gazeti la Mtanzania ambalo humu ndani lilikuwa halina heshima yoyote kutokana na habari zake zenye gilba na zilizochuja ndiyo linatumika kunukuu watu selectively and out of context mradi tu malengo ya wakubwa hawa yanafanikiwa. Ndilo gazeti hili hili na Rai yaliyokuwa yanaandama maisha binafsi ya Slaa na kuposha kwa kiasi kikubwa sana hoja mbalimbali zilizokuwa zinatolewa wakati wa kampeni za uchaguzi. Ndoa hii ya mafisadi na walikouwa wapiganaji inatuacha na maswali mengi lakini lililo dhahiri ni kwamba hakukuwa na nia thabiti ya kupambana na ufisadi na sasa watu wana hasira za kunyang'anywa hoja na sasa wamekuja juu.
Hakuna mtu yeyote anayeshangilia mafisadi ila watu wanachosema kwanini wao tu???? na si wote waliohusika na ufisadi, sasa watu wanapohoji hivyo wengine (wenye assumptions zao) wana interpret vingine.
 
Ant fisadi mr mak wala si wa dini ambayo amekoti hivyo vitabu anachotaka yeye ni kupotosha tu!
Coz kulishawahi kuwa na thread yenye mwelekeo wa kidini na yeye alijiweka wazi yu wa upande gani
 
Kila siku kwenye magazeti lazima usome "Kiongozi fulani ametaka/amewataka hili", "Wananchi wametakiwa hiki"; imekuwa kero kubwa kwa kweli huu msemo wa "amewataka", "wametakiwa", "Government has urged this and that". Hii ni Rhetorical Style ya muda mrefu sana (tokea enzi za Ujamaa) kwenye Vyombo vya Habari ambayo Watawala na Waandishi wa Habari wamekuwa wakitumia kwa makusudi mbele ya Umma ya Wafuatiliaji Habari magazetini, Redioni, kwenye Runinga, nk. ili kuwafanya Wananchi wawe passive, subservient, obedient, and otherwise totally under control siku zote. Katika nchi zote nilizoishi sijawahi kusoma style hii ya Uandishi wa Habari inayoonyesha kujikomba kwa Waandishi Habari kwa Watawala.

Ingekuwa bora zaidi kama tukitumia neno 'Kusihi'
 
Huyu Kadinali kama nia yake ndio hiyo mbona haedni magerezani kuwapa kitubio waliofungwa? Huko ndio atawakuta hawa anaowatetea muda sio mrefu
 
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, amevitaka vyama vya siasa na serikali kwa ujumla kuacha mara moja kuwazuia watu wanaodaiwa kuwa mafisadi kwenda kupata huduma za kiroho.

Kauli ya Kardinari Pengo imekuja siku chache baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kusema mafisadi walioenguliwa na chama hicho wanataka kuwatumia viongozi wa dini ili kujisafisha.


Pengo alitoa rai hiyo jana baada ya kuhitimisha ibada ya misa takatifu ya sikukuu ya Pasaka katika Kanisa la Mt Vinsent wa Paulo, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.


“Kanisa Katoliki halitamfukuza mtu yeyote yule anayedaiwa na serikali au chama kuwa ni fisadi eti asipate huduma zinazomstahili! Kanisa litampokea iwapo ni muumini mzuri na amekwenda kwa ajili ya kupata huduma za kiroho,” alisema.


Kumtenga mtu ni kosa. Mbona Yesu hakumkataa Maria Madgalena na Zakayo mtoza ushuru sasa iweje leo kanisa liwatenge watu wanaodaiwa kuwa ni mafisadi huku wakiwa ni waumini wa kanisa?


Aidha, alisema iwapo mtu hakubaliki katika chama si kweli kuwa na katika kanisa hakubaliki kwa kuwa chama na kanisa ni vitu viwili tofauti. Alisema vyama vinahitaji watu wasafi, lakini kanisa linahitaji wenye dhambi (watu wachafu) ili wapate kutubu na kumrudia Mungu ndio maana Yesu alikuja kwa ajili ya watu wagonjwa na si wazima.


Source: Tanzania Daima

Muadhama,vipi kuhusu wale waumini ambao ni wafuasi wa CCM waliotengwa na Kanisa kule sumbawanga?
 
Mkuu maneno sawa kabisa kwa mtazamo wako na ndio maana mimi sikuwa Mkristu kwa sababu sikubaliani na imani hiyo..
Kwa hiyo maadam mimi sikubaliani sintopenda kumsikia Pengo akizungumzia swala linalonihusu mimi hali sikubaliani na imani yake. Nitakupa Mfano mdogo sana.. Ktk Ukristu jitu linaweza kuua hadharani likakimbilia kanisani na likapewa hifadhi tena Askofu alitoe hata ushahidi dhidi ya hilo jambazi kwa sababu limeungama.. Hii ni imani yenu na naiheshimu lakini sikubaliani nayo kabisa na ndio maana sikuwa mkristu kwa sababu naamini jambazi ni jambazi lilikimbilia kanisani litolewe na kutupwa ndani hakuna kinga kama tunavyodai JK awaondolee kinga hawa Mafisadi na huyo Pengo mwenyewe analikubali hilo.. sasa iweje yeye atake kuwapa kinga hawa jamaa hali alichosema Nape ni kwamba hawa Mafisadi wanataka kukimbilia makanisani ili wasafishwe?

Sasa basi maadam hii ni ibada ya dini yenu, sisi tutaiheshimu na mnaitumia sana kuwalinda hata wahalifu maana wamekuja kutubu lakini usiiweke hii ibada yako kuwa ya kila Mtanzania na kinga kwa hata Mafisadi ambao hawatakiwi ktk uongozi wa jamii.

Mkitaka wasafisheni na wabakie raia wa kawaida tu lakini mnapotaka kuwasafisha ili warudi kisiasa hapo mtakuwa mnaniingilia hata mimi ktk imani yangu kwamba jambazi linastahili jela tu hata kama likikimbilia msikitini litolewe na kukabidhiowa vyombo vya serikali..

Ya Kaizali aachiwe Kaizali, dini zinapoingilia ya Kaizali nina haki ya kuyapiga vita kwani hata Biblia imetukanya.. Kardinal Pengo anatakiwa kufahamu hilo

Mkuu Mkandara,
Leo umenipa sababu ya ziada kwanini wengine wameshindwa kuamini fundisho la Kristo juu ya kusamehe wengine waliotukosea hata 7 x 70. Wakristo hufundishwa hivyo. Kumbe wewe hili lilikushinda? Kwahiyo fundisho la Torati ya Musa la jino kwa jino linapendeza?
Mimi nionavyo ni kuwa, kuna tofauti kati ya malengo ya dini na siasa. Mara nyingine ukishindwa kuiona tofauti hiyo unaweza kulaumu dini au siasa kimakosa. Kwa mtizamo huo, Nape na Cardinary Pengo, wote wako sawa, kwa mujibu wa majukumu wao. Lakini tofauti inakuja katika mtiririko ufuatao:


Mtizamo wa Dini
(a) Anayetoa hukumu ni Mungu na si mwanadamu
(b) Anayeweza kumsamehe mwenye dhambi ni Mungu na siyo Cardinary Pengo
(c) Kanisa ni mlango wa Mungu kwa mwenye dhambi kukutana na Mungu na kusikia maagizo yake
(d) Mwenye dhambi hutafuta kukubalika na Mungu zaidi kuliko kukubalika na binadamu
(e) Mkosaji anaweza kuomba msamaha na kusamehewa kwa masharti Fulani au bila masharti


Mtizamo wa Siasa
(a) Lengo la mtu ni kuifurahisha jamii yake imkubali, na ikiwezekana impe fursa ya kuongoza
(b) Jamii huamua nani ni mkosaji (mtu anaweza kuwa amekosa kwa Mungu lkn jamii ikamwona kuwa ni mtu safi, mzuri, rafiki na kiongozi bora)
(c) Hukumu hutolewa na jamii, na wakati mwingine hukumu ya jamii haina nafasi ya msamaha kwa mkosaji
(d) Wakati mwingine jamii inahitaji kulipiza kisasi kwa mkosaji kama vile kuhukumiwa kifungo, kifo au kufilisiwa mali yake nk

Kutokana na tofauti hizo, mkosaji wa kisiasa, aliyekataliwa na jamii kama RACHEL, ana sehemu ya kukimbilia. Sehemu hiyo ni kwa Mungu wake. Kanisa kama agent wa Mungu, haliwezi kuamrishwa na wanasiasa, mf. Nape, kutenda kama agent wa siasa. Pia kanisa, haliwezi kufunga milango yake dhidi ya wakosaji wanaotaka kuja kufanya mapatano na Mungu wao. Kanisa lazima liwapokee…

Milango ya kanisa sharti iwe wazi wakati wote kwa watu wote, wakosaji na wema. Na kwa kufanya hivyo haimaanishi linasafisha wakosaji, la hasha, bali linatimiza wajibu wake kwa Kristo. Hata hivyo, kanisa litawataka watu wanaokuja kwake kutubu na kuacha dhambi, kufanya mapatano na jamii kwa kurudisha mali waliyoiba. Ndio huo mfano wa Zakayo mtoza ushuru. Vilevile, kanisa lina kemea viongozi dhalimu na fisadi wanaodhurumu wananchi na kuacha kutenda haki. Hilo ni jukumu la kanisa pia ili kusaidia kuleta haki na furaha kwa jamii ya watu wa Mungu.


Mwisho, mafundisho ya Kikristo, yanampa fursa mkosaji ya kujihoji binafsi na kufanya mapatano na Mungu na jamii yake pia. Sioni ubaya wa falsafa hiyo, bali uzuri wenye kutoa matumaini kwa wenye dhambi ambao mimi na wewe tuna hatia ya dhambi na tunahitaji msamaha huo.
 
Mkuu Mkandara,
Leo umenipa sababu ya ziada kwanini wengine wameshindwa kuamini fundisho la Kristo juu ya kusamehe wengine waliotukosea hata 7 x 70. Wakristo hufundishwa hivyo. Kumbe wewe hili lilikushinda? Kwahiyo fundisho la Torati ya Musa la jino kwa jino linapendeza?
Mimi nionavyo ni kuwa, kuna tofauti kati ya malengo ya dini na siasa. Mara nyingine ukishindwa kuiona tofauti hiyo unaweza kulaumu dini au siasa kimakosa. Kwa mtizamo huo, Nape na Cardinary Pengo, wote wako sawa, kwa mujibu wa majukumu wao. Lakini tofauti inakuja katika mtiririko ufuatao:
Mtizamo wa Dini
(a) Anayetoa hukumu ni Mungu na si mwanadamu
(b) Anayeweza kumsamehe mwenye dhambi ni Mungu na siyo Cardinary Pengo
(c) Kanisa ni mlango wa Mungu kwa mwenye dhambi kukutana na Mungu na kusikia maagizo yake
(d) Mwenye dhambi hutafuta kukubalika na Mungu zaidi kuliko kukubalika na binadamu
(e) Mkosaji anaweza kuomba msamaha na kusamehewa kwa masharti Fulani au bila masharti


Mtizamo wa Siasa
(a) Lengo la mtu ni kuifurahisha jamii yake imkubali, na ikiwezekana impe fursa ya kuongoza
(b) Jamii huamua nani ni mkosaji (mtu anaweza kuwa amekosa kwa Mungu lkn jamii ikamwona kuwa ni mtu safi, mzuri, rafiki na kiongozi bora)
(c) Hukumu hutolewa na jamii, na wakati mwingine hukumu ya jamii haina nafasi ya msamaha kwa mkosaji
(d) Wakati mwingine jamii inahitaji kulipiza kisasi kwa mkosaji kama vile kuhukumiwa kifungo, kifo au kufilisiwa mali yake nk

Kutokana na tofauti hizo, mkosaji wa kisiasa, aliyekataliwa na jamii kama RACHEL, ana sehemu ya kukimbilia. Sehemu hiyo ni kwa Mungu wake. Kanisa kama agent wa Mungu, haliwezi kuamrishwa na wanasiasa, mf. Nape, kutenda kama agent wa siasa. Pia kanisa, haliwezi kufunga milango yake dhidi ya wakosaji wanaotaka kuja kufanya mapatano na Mungu wao. Kanisa lazima liwapokee…

Milango ya kanisa sharti iwe wazi wakati wote kwa watu wote, wakosaji na wema. Na kwa kufanya hivyo haimaanishi linasafisha wakosaji, la hasha, bali linatimiza wajibu wake kwa Kristo. Hata hivyo, kanisa litawataka watu wanaokuja kwake kutubu na kuacha dhambi, kufanya mapatano na jamii kwa kurudisha mali waliyoiba. Ndio huo mfano wa Zakayo mtoza ushuru. Vilevile, kanisa lina kemea viongozi dhalimu na fisadi wanaodhurumu wananchi na kuacha kutenda haki. Hilo ni jukumu la kanisa pia ili kusaidia kuleta haki na furaha kwa jamii ya watu wa Mungu.


Mwisho, mafundisho ya Kikristo, yanampa fursa mkosaji ya kujihoji binafsi na kufanya mapatano na Mungu na jamii yake pia. Sioni ubaya wa falsafa hiyo, bali uzuri wenye kutoa matumaini kwa wenye dhambi ambao mimi na wewe tuna hatia ya dhambi na tunahitaji msamaha huo.
Mkuu wangu nadhani kubishana juu ya imani ya dini haiwezi kutupeleka popote na kaa nilivyosema ndio maana tunatofautiana kiimani.

Lakini hata hivyo nitakujibu ninavyoamini mimi na ukweli ni upi utatafuta jawabu wewe. Kwanza kabisa mnaposema kusameheana kunatoa tu ikiwa mkosaji aomba radhi hii inakubaika ktk dini zote na pengine madhehebu mengi lakini kumsafisha mtu aliyekosea hilo haliwezi kufanywa na binadamu. Yesu aliwapokea kondoo waliopotea ikiwa na maana wale ambao walikuwa hawana imani ya kiroho (imani ya kuamini Mungu yupo na ndiye muweza wa kila kitu) hivyo inaruhusiwa kuwapokea hawa watu na kuwapa dawa yaani kuwafundisha dini, lakini hakuna mahala popote ndani ya Biblia Yesu aliendelea kuwakumbatia wakosefu kwa sababu tu walikuwa wafuasi wake. Lowassa, Chenge na huyo Rostam tayari wanajua Mafundisho ya Mungu na wanajua mabaya ni yapi na adhabu zake hivyo unapowapokea makanisani hali ukijua hawafuati mafundisho yako unataka kuwasafisha kitu gani?

Kardinal Pengo katoa mfano wa Maria Magdalena ambaye hakuwa mfuasi hapo awali na Yesu akampokea, hivyo huyu ni tofauti kabisa na Lowassa au Chenge ambao tayari ni wanafunzi wa Pengo na wanapofanya maasi inabidi waungame na mwenye kusamehe ni Mungu peke yake na hakuna mahala imesema ni lazima uende kanisani au msikitini, hivyo huwezi kumsafisha mtu alokwisha kosa isipokuwa kwa nguvu ya Mungu au niseme mnavyoamini kwa jina la Yesu Kristu na haihitaji kuwa kanisani kwa Pengo - samahani lakini.

Ieleweke tunachozungumzia hapa ni dhamira ya hawa mafisadi na sii uwezo wa Kardinal au dini zao isipokuwa Jambazi kukimbilia kanisani likapewa kusafishwa ina maana mbaya zaidi kwa kanisa kuliko jambazi anayekubali makosa yake na kaenda kanisani kuungama..Kisha basi haya maswala ya Mussa na agano la kale au ya Yesu na agano jipya ni jinsi wewe unavyoamini kwa sababu kama kweli sisi ni watu wa kusamehe kwa nini kila nchi duniani ina Magereza (prisons) hali tumeamrishwa kuwasamehe?..
2.Na kama kweli ni Mungu tu ndiye anayehukumu mbona tuna mahakama na tunaomba hawa mafisadi wafikishwe mahakamani?...
3.Mbona leo tunamshambulia Gadaffi hali tumeamrishwa kuwapenda hata maadui zetu, hii biblia na Mafundisho yake kweli wakristu wanaifuata au ni tunapigizana makelele hapa wakati hatukuelemika tulipoisoma..Mkuu katika sifa za mtaji wa AKILI alotupa mwenyezi Mungu ni pamoja na sifa 99 za majina yake mwenyezi Mungu, sisi kuzitumia ktk maisha yetu yaani neno AKILI ni kuwezeshwa kwa uchache ubora wa mwenyezi Mungu mwenyewe.

Acheni kumtetea Pengo wakubwa zangu huyu ni binadamu na anaweza kukosea hasa pale anapojihusisha na maswala ya kisiasa kwani hilo sii taaluma yake..huwezi kuchanganya dini na siasa na biblia imesema wazi ya kaizali tumwachie yeye na hata ukiisoma Biblia hakuna mahala Yesu kaingilia utawala wa Kaizali isipokuwa pale haki ya kiimani inapotaka kupokonywa...

Nitarudia kusema hivi kama angekuwa Sheikh au Mufti kasema maneno hay haya msingeunga mkono hata kidogo na sishangai kwa sababu sijawahi kuona Mkristu akimpinga Kardinali hata kama amefanya kosa kwa sababu ndivyo mnavyotakiwa kufanya wakati mimi naruhusiwa kumkosoa mtu yeyote ikiwa amekosea. Kwetu sisi Waislaam, hakuna binadamu aliyekuwa na daraja la juu kiimani isipokuwa yule anayefanya ibada na ni mwenyezi Mungu pekee anayejua nani mbora kuliko mwingine.
 
huyo naye asipokuwa makini, hatakuwa makamba (mropokaji) mwengine anaongea vipi havina mwanzo wala mwisho
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, amevitaka vyama vya siasa na serikali kwa ujumla kuacha mara moja kuwazuia watu wanaodaiwa kuwa mafisadi kwenda kupata huduma za kiroho.

Kauli ya Kardinari Pengo imekuja siku chache baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kusema mafisadi walioenguliwa na chama hicho wanataka kuwatumia viongozi wa dini ili kujisafisha.


Pengo alitoa rai hiyo jana baada ya kuhitimisha ibada ya misa takatifu ya sikukuu ya Pasaka katika Kanisa la Mt Vinsent wa Paulo, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.


"Kanisa Katoliki halitamfukuza mtu yeyote yule anayedaiwa na serikali au chama kuwa ni fisadi eti asipate huduma zinazomstahili! Kanisa litampokea iwapo ni muumini mzuri na amekwenda kwa ajili ya kupata huduma za kiroho," alisema.


Kumtenga mtu ni kosa. Mbona Yesu hakumkataa Maria Madgalena na Zakayo mtoza ushuru sasa iweje leo kanisa liwatenge watu wanaodaiwa kuwa ni mafisadi huku wakiwa ni waumini wa kanisa?


Aidha, alisema iwapo mtu hakubaliki katika chama si kweli kuwa na katika kanisa hakubaliki kwa kuwa chama na kanisa ni vitu viwili tofauti. Alisema vyama vinahitaji watu wasafi, lakini kanisa linahitaji wenye dhambi (watu wachafu) ili wapate kutubu na kumrudia Mungu ndio maana Yesu alikuja kwa ajili ya watu wagonjwa na si wazima.


Source: Tanzania Daima
 
Mkuu wangu nadhani kubishana juu ya imani ya dini haiwezi kutupeleka popote na kaa nilivyosema ndio maana tunatofautiana kiimani.

Lakini hata hivyo nitakujibu ninavyoamini mimi na ukweli ni upi utatafuta jawabu wewe. Kwanza kabisa mnaposema kusameheana kunatoa tu ikiwa mkosaji aomba radhi hii inakubaika ktk dini zote na pengine madhehebu mengi lakini kumsafisha mtu aliyekosea hilo haliwezi kufanywa na binadamu. Yesu aliwapokea kondoo waliopotea ikiwa na maana wale ambao walikuwa hawana imani ya kiroho (imani ya kuamini Mungu yupo na ndiye muweza wa kila kitu) hivyo inaruhusiwa kuwapokea hawa watu na kuwapa dawa yaani kuwafundisha dini, lakini hakuna mahala popote ndani ya Biblia Yesu aliendelea kuwakumbatia wakosefu kwa sababu tu walikuwa wafuasi wake. Lowassa, Chenge na huyo Rostam tayari wanajua Mafundisho ya Mungu na wanajua mabaya ni yapi na adhabu zake hivyo unapowapokea makanisani hali ukijua hawafuati mafundisho yako unataka kuwasafisha kitu gani?

Kardinal Pengo katoa mfano wa Maria Magdalena ambaye hakuwa mfuasi hapo awali na Yesu akampokea, hivyo huyu ni tofauti kabisa na Lowassa au Chenge ambao tayari ni wanafunzi wa Pengo na wanapofanya maasi inabidi waungame na mwenye kusamehe ni Mungu peke yake na hakuna mahala imesema ni lazima uende kanisani au msikitini, hivyo huwezi kumsafisha mtu alokwisha kosa isipokuwa kwa nguvu ya Mungu au niseme mnavyoamini kwa jina la Yesu Kristu na haihitaji kuwa kanisani kwa Pengo - samahani lakini.

Ieleweke tunachozungumzia hapa ni dhamira ya hawa mafisadi na sii uwezo wa Kardinal au dini zao isipokuwa Jambazi kukimbilia kanisani likapewa kusafishwa ina maana mbaya zaidi kwa kanisa kuliko jambazi anayekubali makosa yake na kaenda kanisani kuungama..Kisha basi haya maswala ya Mussa na agano la kale au ya Yesu na agano jipya ni jinsi wewe unavyoamini kwa sababu kama kweli sisi ni watu wa kusamehe kwa nini kila nchi duniani ina Magereza (prisons) hali tumeamrishwa kuwasamehe?..
2.Na kama kweli ni Mungu tu ndiye anayehukumu mbona tuna mahakama na tunaomba hawa mafisadi wafikishwe mahakamani?...
3.Mbona leo tunamshambulia Gadaffi hali tumeamrishwa kuwapenda hata maadui zetu, hii biblia na Mafundisho yake kweli wakristu wanaifuata au ni tunapigizana makelele hapa wakati hatukuelemika tulipoisoma..Mkuu katika sifa za mtaji wa AKILI alotupa mwenyezi Mungu ni pamoja na sifa 99 za majina yake mwenyezi Mungu, sisi kuzitumia ktk maisha yetu yaani neno AKILI ni kuwezeshwa kwa uchache ubora wa mwenyezi Mungu mwenyewe.

Acheni kumtetea Pengo wakubwa zangu huyu ni binadamu na anaweza kukosea hasa pale anapojihusisha na maswala ya kisiasa kwani hilo sii taaluma yake..huwezi kuchanganya dini na siasa na biblia imesema wazi ya kaizali tumwachie yeye na hata ukiisoma Biblia hakuna mahala Yesu kaingilia utawala wa Kaizali isipokuwa pale haki ya kiimani inapotaka kupokonywa...

Nitarudia kusema hivi kama angekuwa Sheikh au Mufti kasema maneno hay haya msingeunga mkono hata kidogo na sishangai kwa sababu sijawahi kuona Mkristu akimpinga Kardinali hata kama amefanya kosa kwa sababu ndivyo mnavyotakiwa kufanya wakati mimi naruhusiwa kumkosoa mtu yeyote ikiwa amekosea. Kwetu sisi Waislaam, hakuna binadamu aliyekuwa na daraja la juu kiimani isipokuwa yule anayefanya ibada na ni mwenyezi Mungu pekee anayejua nani mbora kuliko mwingine.
Ndugu yangu Mkandara,
Nashukuru sana kwa majibu yako. Kwanza naomba nikiri kuwa majibu yako yanaonesha ama uwezo wako mkubwa wa ufahamu, ama shehena kubwa ya elimu uliyo nayo. Pamoja na uwezo huo mkubwa, umefanana na mtu mmoja mwenye akili, elimu na cheo kikubwa, Zacheus. Huyu jamaa alikuwa na maswali magumu na ya kifalsafa kama ya kwako Ndugu Mkandara. Kwasababu ya aibu alikwenda kwa Bwana Yesu usiku, na kumwuliza maswali yake...

Ndugu yangu Mkandara, naomba tukubaliane kuwa jambo usilolijua, ni kama usiku wa kiza, huwezi kulieleza kwa ufasaha na kina, hata kama utajaaliwa kufanana na Sir Isaac Newton, lazima utakosea tu. Maana yangu ni kuwa, wewe siyo mfuasi wa Yesu na Biblia, ni vigumu sana kuweza kutoa ufafanuzi uliozama na kutiririka kwa mwafaka.

1. Msamaha
Ktk Ukristo hilo ni swala zito sana na unaweza kulitizama katika tabaka mbili
(a) Msamaha kati ya binadamu. U-Kristo unataka kusameheana sisi kwa sisi kama binadamu, (na wakati mwingine bila hata ya masharti ya kuombwa radhi). Ni hali ya unyenyekevu na kujikana nafsi ambayo wa-Kristo wengi mara nyingi tunashindwa kutekeleza. Lakini hicho ndio kiwango cha Ukristo tunachotakiwa kukifikia siku zote. Na msamaha huu hauna kikomo, yaani hata 7 x 70
(b) Msamaha mbele za Mungu. Hii ni huduma ya pekee sana kwa watu wote. Hii ni fursa ya kusamehewa dhambi kupitia kafara ya kifo cha Kristo pale msalabani. Dhambi ni mbaya sana na Mungu hapendi dhambi kabisa! Ghalama yake ilibidi Yesu awe kafara ya dhambi za watu wote ulimwenguni ili kuweza kurejesha mapatano ya wa-dhambi na Mungu aliye kosewa. Hii ndio huduma ya Kristo kwa kila anayekuja kwake. Kanisa ni agent wa huduma hii. Na Cardinary Pengo amesimama kwenye hoja hii. Na katika kutekeleza hoja hii, si kusafisha mtu kisiasa, la hasha. Ni huduma ya kiroho kwa kila mkosaji. Mfano: Mwizi aliyesulubiwa pale msalabani pamoja na Kristo, alitumia fursa hiyo, ya kuwa karibu na Kristo, kuomba msamaha wa dhambi zake. Na Yesu alimsamehe na kumwahidi kuwa atakuwa naye mbinguni! Huyu mwizi hakusafishwa katika jamii. Jamii iliendelea kumona ni mwizi anayestahili kufa. Na kweli hukumu yake iliendelea, na linyongwa (crucified) hadi kufa. Lakini tayari alikuwa amepata msamaha kutoka kwa Mwokozi wa Ulimwengu. Hivyo jamii ilimkataa lakini Kristo alimpokea na kumkumbatia kwa msamaha wa dhambi zake.


Anachofanya Cardinary Pengo ni kuwakaribisha mafisadi (kama wenye dhambi wengine) waje kanisani ili wapate fursa ya utakaso kwa njia ya damu ya Yesu Kristo. Na inawezekana kabisa wakashitakiwa na kufungwa. Lakini kufungwa, au kufilisiwa mali, ama kunyongwa hakuwezi kuondoa dhambi zao. Hata kama tukiwaponda mawe hadi kufa, dhambi zao haziwezi kufutika asilani. Bali ni kwa huduma ya kwa njia ya damu ya Masihi Mkuu, aliyesulubiwa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Hii ndio falsafa iliyokushinda kuielewa na kuuchukia Ukristo.


2. Kondoo waliopotea
Katika majibu yako umehoji kwanini Cardinary Pengo anapokea waumini wake na kuwakumbatia badala ya kupokea wale ambao sio waumini ili apate kuwafundisha dini. Mkuu Mkandara, huujui Ukristo, malengo yake na taratibu zake. Una haki ya kusema hayo. Lakini ukweli ni kuwa, Kristo alikufa kwa ajili ya watu wote (wewe, mimi na Yule..). Kila mtu aliye na dhambi anaitwa na Yesu kuja kupumzishwa mizigo ya dhambi. Mpango wa ukombozi ni kwa watu wote, wenye dhambi na wasio na dhambi (kimsingi hakuna mtu asiye na dhambi!), waumini na wasio waumini, wa-Islam na wa-Budha, na Wapagani. Woote, milango iko wazi usiku na mchana kuja kupata huduma ya utakaso na uptanisho.

Umesema Magdalena hakuwa mwanafunzi wa Yesu? Mimi nasema hivi, Magdalene alikuwa muumini wa dini ya ki-Yahudi, lakini alikuwa amezama katika dhambi na kuasi sheria za dini. Kwahiyo, technically, Magdalena alikuwa mwanafunzi wa Yesu kama alivyo Chenge, Edward, mimi na wewe. Hivyo Yesu alimpokea kwa upendo na kumhudumia kiroho. Hata Andrew, Edward, Aziz, mimi na wewe, hakuna kizuizi kupata huduma hiyo leo, ni hiari tu ya kila mmoja wetu kama tunahitaji huduma ya Yesu. Haina malipo, ni bure.

3. Kanisa na Msamaha wa Dhambi
Ni kweli kama ulivyosema, kuwa mtu hahitaji kuwa kanisani ili kupata msamaha wa Kristo. Hata ukiwa peke yako nyumbani, au ndani ya ofisi yako unaweza kuomba msamaha. Lakini bado kanisa lina shemu kubwa katika mtiririko wa shughuli za kiroho. Kwa mfano mtu mwingine amezidiwa na dhambi, na zimemlemea. Unaweza kukuta mtu amehangaika na dhambi hadi amechafuka ndani ya jamii! Mtu mwingine hata jamii haijui shida yake, lakini mzigo wa dhambi moyoni mwake umezidi uwezo wake. Hapo ndipo palipo na nafasi ya kanisa. Mchungaji anaweza kumpa councelling, au kumpa msaada wa maombi, au kumfuta kwenye ushirika ili aanze upya tena akiwa amefanya ungamo la kweli. Taratibu zinaweza kuwa complicated hapa…kwasababu hili ni swala zito linalohusiana na wokovu wa roho ya mtu. Hapa siasa na kanisa ni mbali kama mbingu na nchi. Nakuomba umwache Cardinary Pengo, na watumishi wengine wa ki-Kristo wafanye kazi ya dini bila kuingiliwa na siasa. Haya ni mambo ya kiroho zaidi na ni tofauti na siasa.

4. Kushambuliwa kwa Gadaffi
Hili halina uhusiano wowote na dini ya Ukristo. Mataifa ya Maghalibi hayana masirahi yoyote katika u-Krsito. Kinachoendelea huko Libya ni mambo ya politics za dunia na masirahi ya kiuchumi ya nchi za Maghalibi.

Mwisho, napenda kusema hivi, mimi nimetoka kwenyea familia ya ki-Islam kama wewe. Baba yangu mzee Juma ni mwislam mzuri hadi dakika hii. Uislam naufahamu kuwa ni tofauti sana na u-Kristo. Hivyo ni vigumu kukubaliana katika mafundisho ya dini hizi mbili. Lakini, nfugu yangu Mkandara, dini hizi kamwe haziwezi, kuwakilisha mafundisho ya Mungu mmoja. Vinginevo huyo Mungu atakuwa amejaa mikanganyiko na kuwa confuse viumbe wake kiasi kikubwa sana. Hizi imani mbili ni tofauti mno Mkuu wangu. Mara zote huwa namwambia baba yangu kuwa, lazima dini moja inapotosha ukweli wa Mungu aliyeumba mbingu na ardhi. Lakini kwavile dini ni hiari ya mtu kuchagua, basi hiari zetu zitakuja kupimwa siku ya kiyama.
 
Mkuu sasa wewe ndio umekuwa msemaji wa Pengo?

Soma aliyoyasema Nape Mnauye, kisha yachukue majibu ya Pengo kujibu hoja ya Nape...sikutunga mimi hadithi hii ila nimewasoma wote.
Na maadam unakubali kwamba mimi Muislaam na ndio sababu sikuwa Mkristu, namwomba Pengo asijewasafisha watu hawa warudi kutafuta kutawala hata kama inakubalika ktk imani yako na ndicho hiki kitapelekea mimi kuamini kwamba kweli kanisa ndio linatawala nchi.
Utanisamehe kama hukunisoma vizuri ukakurupuka tena kutoa hukumu...

Una harufu kali ya udini!
 
Sn2139,
Mkuu wangu umezungumza maelezo mengi ambayo nayafahamu na labda nikwambie Biblia ni sehemu ya kuran isipokuwa tunatofautiana tafsiri ktk baadhi ya aya. Na nadhani hata madhehebu mengine hayakubaliani na tafisri ya aya za Kikatoliki ndio maana sisi wote humu tuna imani tofauti...

Sasa labda nirudi ktk issue yetu... Hawa Mafisadi ni mafisadi wa Taifa na wanafanya hawa wakiwa waumini wa dini zetu, ni wakosefu ambao wanahitaji sio tu kuondolewa madaraka bali kufikishwa hadi mahakamani na kupewa adhabu inayowastahili..Na Nape kasema wazi nia na lengo la hawa watu ni kuwatumia VIONGOZI wa dini wajisafishe! hakusema watakwenda makanisani wakatubu (toba) au kuungama, laa ila wanataka kuwatumia viongozi wa dini wasafishike na hakusema viongozi gani au wa dini gani.

Na tumewaona viongozi wa dini zetu jinsi wanavyojaribu kuwasafisha viongozi hata kupinga maandamano ya Chadema, wengine kumsema wazi JK kwa sifa na kejeri ili mradi tu ni nje ya toba au ibada za kidini, hivyo tunapomsikia Nape akisema hivyo tunajua fika kinafuata kitu gani.

Sasa Kardinal anapokurupuka na kudai hawezi kuwakataa mafisadi ina maana yupo tayari kuwasafisha hata kama sii toba maana muumini anatakiwa kwanza kukiri makosa yake apate kusamehewa kiroho (toba), nadhani yapo mashatri yake kama vile kurudisha mali za wale aliwadhurumu au vinginevyo. Na sidhani kama namwingilia Kardinali kazi zake isipokuwa yeye ndiye kaingilia kazi za Kaizali na nampinga kwa hilo tu, kinyume cha hapo naheshimu utaratibu wa kanisa Katoliki ingawa sii maji yangu.

Mkuu, hawa jamaa hawana lengo la kukiri makosa yao wasamehewe kiroho, isipokuwa kusafishwa kisiasa ili waonekane ni viongozi bora waliosingiziwa ama kuondolewa madaraka kwa kuonewa. Lowassa kafanya hivyo hata wakati wa kujiuzuru Uwaziri mkuu na wapo watu wanaamini alionewa na JK..
Na sikubaliani na maelezo yako kwamba Maria Magdalena alikuwa muumini wa dini ya Kiyahudi, isipokuwa alikuwa Mu Israel akifanya umalaya kinyume cha waumini..Siku zote imani inakuongoza kufanya mema na muumini wa dini ni yule anayefanya ibada za dini hiyo na sii kwa kuzaliwa. hata Kaizali alikuwa muumini wa Kiyahudi na alipingana na Yesu siku ya mwisho hivyo hakuwa mwanafunzi wa Yesu..iwe technically au reality.

Mifano mingine yote niliyoitoa hapo juu ni ktk kukueleza jinsi wanadamu tunavyoitafsiri Biblia vibaya ktk matumizi yake. Utasikia watu wakilaani kuhukumu mtu hali tunazo mahakama na wanashindwa kuzielezea ktk ngazi ya imani ya dini..Umesema kumshambulia Ghadaffi haihusiani na dini, ebu nambie wewe kulingana na dini yako, mathlan kiongozi muuaji wa watu wake anatakiwa kufanywa nini?...Mkuu wangu Pengo afanye kazi yake pale hawa watu watakuja kutubu madhambi yao na haitahusiana kabisa na hoja ya Nape kwani toba hiyo ni ya kiroho na sii kwa lengo la kuwasafisha kisiasa..
 
Back
Top Bottom