Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
SIASA zisizozingatia thamani ya utaifa zimetajwa kusababisha baadhi ya wanasiasa kutolewa kafara na wananchi kushawishika kuamini kwamba wanasiasa hao ndiyo wabaya wakati watu wanaofanya mambo mabaya nchini ni wengi.
Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Askofu Dk. Valentino Mokiwa,amesema, kukosekana kwa siasa zinazozingatia utaifa, kumesababisha watu kutukanana, kuchimbana na kunyosheana vidole, huku kundi la wachache likionekana ndilo lenye watu wabaya katika jamii.
Mfano hivi sasa neno ufisadi limegeuka kuwa silaha ya baadhi ya watu kupigana; wabaya wako wengi, lakini kuna watu wamepandikizwa kuonekana ndiyo wabaya miongoni mwa jamii.
Kumbuka hata asiyefanya kazi ni mtu mbaya, mwizi ni mtu mbaya, wabaya ni wengi tu, lakini wachache ndiyo wamefanywa kuwa wabaya, alisema jana wakati anazungumza na HABARILEO. Askofu Mokiwa alisema hayo wakati akizungumzia ujumbe wake wa Pasaka mwaka huu.
Alisema, Tanzania limekuwa Taifa la wavivu, lakini lenye watu wasemaji sana na wajuzi wa kunyoosheana vidole, kwa sababu kuna baadhi ya watu wajanja ambao wanavuruga amani kwa kujiona ni bora zaidi ya wengine na kugeuza wenzao wabaya katika jamii.
Askofu Mokiwa alisema, yote haya yanatokana na Taifa kukumbwa na msongo wa mawazo, ambao unaonekana kuongezeka kwa kasi na matokeo yake ni kuwa na nchi inayoamini demokrasia lakini ikipoteza mwelekeo wa demokrasia.
Hivi sasa tuna viongozi ambao hawaongozi, kwa sababu wana mamlaka, lakini wanategemea kuongozwa na wengine na kama hali itaendelea hivi, Taifa litakuwa likielekea pabaya, alisema.
Alisema, pia kutokana na Taifa kuwa na msongo wa mawazo, gharama za maisha zimekuwa zikiongezeka, ingawa kuna wachumi wengi lakini hawajui wanachokifanya na kuongeza kuwa kilichobaki ni kumwomba Mungu.
Kwa mujibu wa Askofu Mokiwa, hali ilivyo sasa, Watanzania wamekuwa wakifikirishwa na vyombo vya habari na wanasiasa, na kueleza kuwa hiyo ni dalili mbaya kwa Taifa na kulielekeza tukio lililotokea hivi karibuni bungeni, kuwa ni mfano halisi wa mwelekeo wa kutetereka kwa Taifa.
Alikuwa akimaanisha wabunge kuzomeana na baadhi yao kutaka mlango ufungwe ili wapigane kutokana na kutofautiana juu ya masuala mbalimbali, ambapo alisema ni jambo la aibu.
Askofu Mokiwa alisema, wakati Watanzania wakisherehekea Pasaka, wanapaswa kubadilika kwa kupunguza kusemana na kunyoosheana vidole na kuwataka kuacha tabia ya kujichukulia sheria midomoni kwa kuhukumu wengine, ili nchi isielekee kubaya.
Alisema dhambi ya kusema sana na kunyoosheana vidole, imekuwa shida kubwa, kwani imeingia hata makanisani na kusababisha kukosekana kwa amani. Waumini hawana amani, viongozi wa dini hawana amani, kwa sababu kila mmoja anaona ndiye bora kuliko mwingine.
Tujiheshimu, tuache dhuluma, wanaotuongoza wasiwe wavivu na wasimame katika nafasi zao tuishi kwa umoja na kuthamini utaifa wetu, kwani ndicho chanzo cha amani, alisema.
Akitoa mtazamo wake wa kidunia, alisema amani imechafuka ndiyo maana maeneo ya Mashariki ya Kati, viongozi wanaondolewa madarakani, lakini wanaowaondoa hawajui nani wa kuwaweka badala, huku mataifa ya Magharibi nayo yakiendelea kuonesha ubabe na vitisho dhidi ya mataifa mengine.
Wakati huo huo, Askofu wa Kanisa la Amani Christian Center la Tabata, Dar es Salaam, Lawrence Kameta, alisema Watanzania wanatakiwa kusherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kutambua kusudi la Bwana Yesu ambaye alikuja duniani kuwaletea wanadamu uzima na amani katika maisha.
Tunatakiwa kujua Yesu alikuja ili wanadamu tupate uzima na amani katika maisha kwa njia ya kumrudia Mungu kiroho na kumrudia kiroho ni mabadiliko ya ndani ambayo matokeo yake yanamfanya mtu kuwa mwadilifu kwa Mungu na wanadamu, alisema.
Hata hivyo alisema mabadiliko hayo hayawezi kupatikana bila kumkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha ya mtu binafsi na kwamba watu wote wakipokea Pasaka kwa njia hiyo itakuwa haina maana ya kuendelea kuishi maisha ya uovu na kuonewa na ibilisi.
Aliitaka jamii isherehekee kwa kuchukua hatua ya kuyatenda na kutambua kusudi la Yesu katika sikukuu ya Pasaka.
Habari Leo
Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Askofu Dk. Valentino Mokiwa,amesema, kukosekana kwa siasa zinazozingatia utaifa, kumesababisha watu kutukanana, kuchimbana na kunyosheana vidole, huku kundi la wachache likionekana ndilo lenye watu wabaya katika jamii.
Mfano hivi sasa neno ufisadi limegeuka kuwa silaha ya baadhi ya watu kupigana; wabaya wako wengi, lakini kuna watu wamepandikizwa kuonekana ndiyo wabaya miongoni mwa jamii.
Kumbuka hata asiyefanya kazi ni mtu mbaya, mwizi ni mtu mbaya, wabaya ni wengi tu, lakini wachache ndiyo wamefanywa kuwa wabaya, alisema jana wakati anazungumza na HABARILEO. Askofu Mokiwa alisema hayo wakati akizungumzia ujumbe wake wa Pasaka mwaka huu.
Alisema, Tanzania limekuwa Taifa la wavivu, lakini lenye watu wasemaji sana na wajuzi wa kunyoosheana vidole, kwa sababu kuna baadhi ya watu wajanja ambao wanavuruga amani kwa kujiona ni bora zaidi ya wengine na kugeuza wenzao wabaya katika jamii.
Askofu Mokiwa alisema, yote haya yanatokana na Taifa kukumbwa na msongo wa mawazo, ambao unaonekana kuongezeka kwa kasi na matokeo yake ni kuwa na nchi inayoamini demokrasia lakini ikipoteza mwelekeo wa demokrasia.
Hivi sasa tuna viongozi ambao hawaongozi, kwa sababu wana mamlaka, lakini wanategemea kuongozwa na wengine na kama hali itaendelea hivi, Taifa litakuwa likielekea pabaya, alisema.
Alisema, pia kutokana na Taifa kuwa na msongo wa mawazo, gharama za maisha zimekuwa zikiongezeka, ingawa kuna wachumi wengi lakini hawajui wanachokifanya na kuongeza kuwa kilichobaki ni kumwomba Mungu.
Kwa mujibu wa Askofu Mokiwa, hali ilivyo sasa, Watanzania wamekuwa wakifikirishwa na vyombo vya habari na wanasiasa, na kueleza kuwa hiyo ni dalili mbaya kwa Taifa na kulielekeza tukio lililotokea hivi karibuni bungeni, kuwa ni mfano halisi wa mwelekeo wa kutetereka kwa Taifa.
Alikuwa akimaanisha wabunge kuzomeana na baadhi yao kutaka mlango ufungwe ili wapigane kutokana na kutofautiana juu ya masuala mbalimbali, ambapo alisema ni jambo la aibu.
Askofu Mokiwa alisema, wakati Watanzania wakisherehekea Pasaka, wanapaswa kubadilika kwa kupunguza kusemana na kunyoosheana vidole na kuwataka kuacha tabia ya kujichukulia sheria midomoni kwa kuhukumu wengine, ili nchi isielekee kubaya.
Alisema dhambi ya kusema sana na kunyoosheana vidole, imekuwa shida kubwa, kwani imeingia hata makanisani na kusababisha kukosekana kwa amani. Waumini hawana amani, viongozi wa dini hawana amani, kwa sababu kila mmoja anaona ndiye bora kuliko mwingine.
Tujiheshimu, tuache dhuluma, wanaotuongoza wasiwe wavivu na wasimame katika nafasi zao tuishi kwa umoja na kuthamini utaifa wetu, kwani ndicho chanzo cha amani, alisema.
Akitoa mtazamo wake wa kidunia, alisema amani imechafuka ndiyo maana maeneo ya Mashariki ya Kati, viongozi wanaondolewa madarakani, lakini wanaowaondoa hawajui nani wa kuwaweka badala, huku mataifa ya Magharibi nayo yakiendelea kuonesha ubabe na vitisho dhidi ya mataifa mengine.
Wakati huo huo, Askofu wa Kanisa la Amani Christian Center la Tabata, Dar es Salaam, Lawrence Kameta, alisema Watanzania wanatakiwa kusherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kutambua kusudi la Bwana Yesu ambaye alikuja duniani kuwaletea wanadamu uzima na amani katika maisha.
Tunatakiwa kujua Yesu alikuja ili wanadamu tupate uzima na amani katika maisha kwa njia ya kumrudia Mungu kiroho na kumrudia kiroho ni mabadiliko ya ndani ambayo matokeo yake yanamfanya mtu kuwa mwadilifu kwa Mungu na wanadamu, alisema.
Hata hivyo alisema mabadiliko hayo hayawezi kupatikana bila kumkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha ya mtu binafsi na kwamba watu wote wakipokea Pasaka kwa njia hiyo itakuwa haina maana ya kuendelea kuishi maisha ya uovu na kuonewa na ibilisi.
Aliitaka jamii isherehekee kwa kuchukua hatua ya kuyatenda na kutambua kusudi la Yesu katika sikukuu ya Pasaka.
Habari Leo