Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,462
- 21,334
ndugu watanzania nadhani hivi sasa watanzania tunatakiwa tuanalie na watu wa chini jamani...ufisadi umeanza kufika hadi vyuo vikuu vya dini...tuna mwezi sasa tunaona tangazo la chuo cha tumaini
**ASKOFU MKUU MALASUSA ANAOMBA WALE WENYE MAPENZI MEMA KUCHANGIA CHUO KIKUU CHA TUMAINI""
mmmhhh sasa huyu anaomba maskini wachangie chuo wkati huo huo anashabikia ongezeko la ada ya wanafunzi kutoka millin 1.5-2.5...sasa kuna haja ya kuchangia kweli chuo kama hiki...kwa mtaji huu naona hiki watasoma watoto wa mafisadist tu...na sioni kama mkuu wetu ana haki ya kupinga ufisadi kama anasema mwenye uwezo atakuja kusoma.....
Askofu Malasusa aunga mkono ongezeko la ada vyuo vikuu
Na Nora Damian
MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania (KKKT), Askofu Alex Malasusa ametetea mpango wa kuongezwa ada kwa Chuo Kikuu cha Tumaini kwa kuwa mpango huo, una lengo la kuboresha elimu nchini.
Akizungumza katika kituo cha televisheni cha TBC jana, Malasusa alisema halilengi kuwatenga wanyonge bali linataka kuwawezesha kuwepo kwa shule nyingi kama zilivyo hospitali na huduma zingine za jamii.
Malasusa aliwataka watu wenye uwezo wawasaidie wanafunzi wasiokuwa na uwezo ili wapate elimu bora.
Hata igekuwa shilingi moja lazima watu wakajua msingi wa ada iliyopo na elimu yoyote nzuri lazima igharamiwe,alisema Malasusa.
Hivi karibuni chuo hicho, kilitangaza kupandisha ada kwa asilimia 60 kwa wanafunzi wa shahada ya kwanza na kiwango cha awali kilikuwa Sh 1.5 milioni na kimepanda hadi Sh 2.5 milioni.
Hatua hiyo ya kupandisha ada imelalamikiwa na baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika chuo hicho na kufafanua kuwa ongezeko hilo ni kubwa.
Baadhi ya wanafunzi hao wameuomba uongozi wa chuo hicho kufikiria upya ongezeko hilo la ada kwa kuwa wanafunzi wengi wanalipiwa ada na wazazi wao.
**ASKOFU MKUU MALASUSA ANAOMBA WALE WENYE MAPENZI MEMA KUCHANGIA CHUO KIKUU CHA TUMAINI""
mmmhhh sasa huyu anaomba maskini wachangie chuo wkati huo huo anashabikia ongezeko la ada ya wanafunzi kutoka millin 1.5-2.5...sasa kuna haja ya kuchangia kweli chuo kama hiki...kwa mtaji huu naona hiki watasoma watoto wa mafisadist tu...na sioni kama mkuu wetu ana haki ya kupinga ufisadi kama anasema mwenye uwezo atakuja kusoma.....
Askofu Malasusa aunga mkono ongezeko la ada vyuo vikuu
Na Nora Damian
MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania (KKKT), Askofu Alex Malasusa ametetea mpango wa kuongezwa ada kwa Chuo Kikuu cha Tumaini kwa kuwa mpango huo, una lengo la kuboresha elimu nchini.
Akizungumza katika kituo cha televisheni cha TBC jana, Malasusa alisema halilengi kuwatenga wanyonge bali linataka kuwawezesha kuwepo kwa shule nyingi kama zilivyo hospitali na huduma zingine za jamii.
Malasusa aliwataka watu wenye uwezo wawasaidie wanafunzi wasiokuwa na uwezo ili wapate elimu bora.
Hata igekuwa shilingi moja lazima watu wakajua msingi wa ada iliyopo na elimu yoyote nzuri lazima igharamiwe,alisema Malasusa.
Hivi karibuni chuo hicho, kilitangaza kupandisha ada kwa asilimia 60 kwa wanafunzi wa shahada ya kwanza na kiwango cha awali kilikuwa Sh 1.5 milioni na kimepanda hadi Sh 2.5 milioni.
Hatua hiyo ya kupandisha ada imelalamikiwa na baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika chuo hicho na kufafanua kuwa ongezeko hilo ni kubwa.
Baadhi ya wanafunzi hao wameuomba uongozi wa chuo hicho kufikiria upya ongezeko hilo la ada kwa kuwa wanafunzi wengi wanalipiwa ada na wazazi wao.