Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
* Aonya walio chini yake kutojiingiza, Tume yasema ni hatari
NA MWANDISHI WETU
MKUU wa makanisa ya Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu Mosses Kulola, ametoboa kuwa kuna mtandao wa kisiasa makanisani ambao unampigia debe mmoja wa wanasiasa nchini. Kutokana na hali hiyo, amepiga marufuku watumishi na waumini wa kanisa hilo kushiriki katika mipango ya uchochezi wa kidini unaofanywa na makanisa hapa nchini. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Askofu Kulola, alisema: ìNapiga marufuku makanisa yote yaliyo chini yangu hapa nchini, kujiingiza katika mpango huo wa kishetani unaondaliwa kuleta uvunjifu wa amani."
Alisema haoni sababu ya kuungwa na ëforumí ya makanisa kama chombo cha kuutetea Ukristo unaodaiwa uko mbioni kutokomezwa na Uislamu kwa kumkataa Rais Jakaya Kikwete na kuona Rais mkristo ndiye atakayenusuru ukristo hapa nchini. ìKanisa limejisahau, limeacha maombi sasa linataka kulazimisha kupata kiongozi wa nchi nje kabisa ya mpango wa Mungu,î alitahadharisha Askofu Kulola.
Askofu huyo ambaye ni miongoni wa viongozi wa kidini wanaoheshimika hapa nchini, aliongeza kuwa anashangaa kuona jinsi viongozi wa makanisa wanavyokaa pamoja kuwapotosha waumini wao juu ya ukweli wa Mungu wakati awnaelewa wazi staili ya kanisa ya kuomba kitu chochote ni kwa njia ya maombi na siyo kutumia nguvu kama wanavyofanya sasa. Kulola aliendelea kusema kuwa baadhi ya viongozi wa makanisa wametanguliza maslahi binafsi badala ya kulitanguliza taifa na kuwa nenola Mungu linaeleza kuwa serikali au mamlaka yoyote inayotoka kwa Mungu hakuna budi kuitii na jukumu la watumishi wa Mungu ni kuiombea mamlaka hiyo.
Askofu Kulola alisema katika Biblia hakuna kifungu chochote kinachoeleza nchi lazima iongozwe na mkristo, Mungu hana upendeleo, chuki wala wivu kama ilivyo kwa binadamu. Rais Kikwete hana baya katika nchi yetu, ameongoza kwa amani na utulivu. Hajamzuia mkristo yeyote kueneza na kuhubiri Injili amekuwa akiwapa ushirikiano na wakati mwingine mmekuwa mkumtumia kwa shughuli zenu, leo mnamkataa eti mnataka Rais mkristo,îalihoji kiongozi huyo. Aliwakumbusha viongozi hao wa makanisa kuwa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni muislamu aliwajengea kanisa Wakristo mkoani Kilimanjaro na ambalo hakuna kiongozi aliyelikataa kwa kuwa limejengwa na muislamu. Alitoa wito wa kudumisha amani ya Tanzania kwa kupinga kwa nguvu zote tamko lolote lenye misingi ya udini na kuwataka watanzania wa dini zote kudumisha mshikamano katika nchi pasipo kubaguana.
Kwa misingi hiyo, alisema hawawezi kumkataa Rais Kikwete kwa uislamu wake na kumweka Rais mkristo kwa nguvu pasipo mpango wa Mungu. Ameagiza kuwepo kwa ibada za Jumapili katika makanisa yote ya EAGT kama kawaida na tofauti na ibada zilizopendekezwa na ëforumí ambazo zitafanyika Jumamosi badala ya Jumapili ya wiki ijayo ambayo itakuwa siku ya kupiga kura. Pia ameagiza makanisa yote ya EAGT kufunga na kuomba kwa ajili ya nchi na serikali. Katika hatua nyingine, Hamis Shimye, anaripoti kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa dini kuwaelekeza wananchi kupiga kura kwa misingi ya udini ni hatari kwa taifa.
Hali ambayo NEC imevitaka vyama vya siasa nchini kuhakikisha haviwatumii viongozi wa dini kuwapigia kampeni kwa ajili ya wagombea wao. Mkurugenzi wa uchaguzi, Rajabu Kiravu, aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa dini. Alisema viongozi wa dini nao wanapaswa kuheshimu maadili ya uchaguzi nchini kama walivyofanya viongozi wa vyama vya siasa. ìViongozi wa vyama vya siasa walisaini fomu za maadili ya uchaguzi zenye mwelekeo wa kuacha kutumia udini kwenye kampeni zao,ííalisema
Kiravu alisema kifungu cha 2.1(i) na 2.2(j) vinaeleza wazi kwa viongozi, wagombea au wafuasi wa vyama vya siasa kuhakikisha majengo wanayoyatumia kwa ajili ya kampeni sio ya ibada. Kutokana na hali hiyo, Kiravu alisema viongozi wa dini walipaswa kuliheshimu hili ambalo viongozi wa vyama vya siasa wanalitambua. Hivyo aliwataka viongozi wa dini kuacha kuwashinikiza au kuwaelekeza wananchi wawachague viongozi kwa misingi ya udini kwa kuwa inahatarisha amani ya nchi. Kwa upande wake, Baraza la Maadili ya Kiislamu Tanzania (BAMAKITA) limewashukia viongozi wa dini wanaogeuza madhabahu kuwa majukwaa ya kisiasa jambo ambalo linahatarisha umoja na mshikamano, anaripoti Khadija Mussa.
Mwenyekiti wa BAMAKITA, Sheikh, Athumani Mkambaku, alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa kampeni za uchaguzi mkuu. ìTunawaona baadhi ya viongozi wa makanisa wamejiingiza kwenye kampeni ndani ya nyumba za ibada, kitendo chenu cha kumpigia debe makanisani mgombea wenu kinatufanya sisi Waislamu na wananchi tumuogope kuliko ukoma," alisema. Mkambaku aliwataka wananchi kuwa makini na viongozi wa aina hiyo na wajitokeze siku ya kupiga kura ili watumie haki yao kwa kuwachagua viongozi bora wasioendekeza udini na ukabila na ambao wataendeleza amani na mshikamano wa Watanzania. Alisema taifa linaweza kuingia kwenye mgogoro usio wa lazima kama wapiga kura hawatakuwa makini kuchagua viongozi. Mwenyekiti huyo aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na NEC.
Chanzo: Gazeti la Uhuru
UPDATE
ASKOFU KULOLA AFARIKI DUNIA....!!
Thursday, August 29, 2013 | 3:50 PM
Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde zinasema kuwa Askofu Mkuu wa Evangelistic Assemblies God Tanzania, Moses Kulola amefariki dunia takriban dakika 25 zilizopita.
Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika kutoka kwa watu wa ndani wa familia hiyo, zinaeleza kuwa Askofu Kulola amefariki katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam.
Askofu Kulola, ambaye amezaliwa mwaka 1928, amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu na hata kufikia hatua ya kupelekwa nchini India kwa matibabu.
Katika uhai wake, amepata watoto wengi wa kiroho ikiwemo Dr Daniel Kulola, Mchungaji Florian Katunzi, Zakaria Kakobe, Mzee wa Upako, Maboya, Mwasota na wengineo wengi.
BWANA ametoa na BWANA ametwaa, jina la BWANA lihimidiwe.
MJUE ASKOFU MOSES KULOLA
Moses Kulola, alizaliwa mwezi Juni 1928, katika familia ya watoto kumi, na watano kati yao bado ni hai. alisajiliwa katika shule ya kwanza mwaka 1939 iitwayo Ligsha Sukuma shule ya misheni baada ya Ligsha, alijiunga na taasisi ya usanifu mwaka 1949. Alibatizwa mwaka 1950 katika Kanisa la AIC Makongoro.
Ni mume wa Elizabeth na wamezaa watoto10 ambapo saba bado hai.alianza kazi za kimisionari mwaka1950 japokuwa aliitwa mwaka 1949 mara tu baada ya kubatizwa.
Mwaka 1959 alianza kufanya kazi serikalini, wakati huo huo akihubiri Injili katika miji na vijiji. Utumishi wake mkubwa kwa nchi ulifika mwisho mwaka 1962, ambapo aliamua kujitolea moja kwa moja nguvu zake zote, mwili na nafsi. Mwaka 1964 alijiunga na chuo cha kiteolojia na 1966 alitunukiwa stashahada.
Hakuacha elimu pale tu, aliendelea na masomo mbalimbali ambapo alitunukiwa vyeti mbalimbali katika mataifa mbalimbali.
Alihudumu kikazi kwa miaka miwili kama Mchungaji kabla ya kuwa mpentekoste mnamo 1961-1962, alifanya kazi katika kanisa la TAG 1966 mpaka 1991 ambapo aliamua kuanzishaa makanisa Evangelistic Assemblies God (EAGT), ambapo yalifanikiwa kukua kwa kasi kubwa katika nchi za Tanzania, Zambia , Malawi na kwa ujumla kuna makanisa yapatayo 4000 katika nchi mbalimbali yakiwemo makubwa na madogo Askofu Moses Kulola anayeongoza makanisa elfu nne, Askofu Msaidizi wake ni Mwaisabila.
Mchakato wa kuongoza makanisa elfu nne si rahisi na kwamba kumefanyika mgawanyiko wa majimbo yasiyopungua 34 ya kazi na kanda tano kwa ajili ya kurahisisha kazi na kila kanda na jimbo lina mwangalizi wake.
Askofu Kulola aliyeketi akiwa na waimbaji wa injili nchini Mwinjilisti Faustin Munishi mkono wa kushoto pamoja na Emmanuel Mwasota. mwanzoni mwa mwaka 1970
Nampenda sana Askofu Moses Kulola maana anafanya kazi ya MUNGU kwa moyo na kwa mujibu wa kitabu cha historia yake Askofu Kulola amezunguka Tanzania nzima tena wakati mwingine kwa kutembea kwa miguu na kwenye mazingira magumu sana kiasi kwamba ni wito mkuu wa MUNGU mkuu alionao Askofu Kulola na kwa miaka zaidi ya 60 amekuwa akihubiri neno la MUNGU na hadi sasa MUNGU anamtumia sana, katika mkutano uliopita wa askofu Kulola pale viwanja vya jangwani jijini Dar es salaam maelfu ya watu walihudhulia na wengi sana kufunguliwa na injili anayohubiri askofu Kulola ni injili iliyonyooka na akiwataka wanadamu kumpa YESU KRISTO maisha yao ili wapate uzima wa milele bure.
Ukiacha mengi ambayo Mungu anaendelea kumtumia mtumishi wake huyu, kuna suala la nywele zake, askofu Kulola kama tulivyowahi kuandika siku zilizopita, hajanyoa nywele zake kwa takribani miaka 47 sasa, kwakuwa hakupendezwa na suala la kwenda salon kunyoa nywele zake hivyo akamwambia Mungu nywele alizokuwa nazo kwa wakati huo zisikue zaidi au kupungua, na ndivyo ilivyo mpaka sasa wembe haujapita kichwani mwake.
Askofu Kulola akipeana mkono na mwanae Daniel Kulola ambaye ni mchungaji.
Chanzo. Global Publishers