Askofu Kilaini achemsha kwa ushauri huu!

Mh!
Hadithi ya vipofu na tembo katika ujinga wa mwafrika. Heshima kwenu wakuu endeleeni hivyo hivyo tuwajue eeh!
 
Cynic am sorry kusema kuwa umekuwa bias na kuaundermine uhuru wa mtu kutoa maoni,Kilaini ametoa wazo kama mtu mwingine alivyo na uhuru wa kutoa maoni.
Au unaogopa kwa kuwa ni mtu mkubwa kidogo basi serikali itakurupuka kuutekeleza bila kuwa na analysis.
If you belong to the so called churches with 200 WAUMINI WORRY NOT kuwa na amani ya roho na mwili bwana yale ni maoni yake kama mtanzania.
Kumbuka akili ni nywele kila mtu ana zake.
Afterall serikali imesema itajipanga to dig deep into that

Ok Njowepo. Ila kwangu issue hapa ni Liberty Liberty Liberty Liberty... and I don't belong to the so called churches with 200 - i just feel for them.

Kwanza yeye ndiye yuko biased na anataka kuaundermine uhuru wa watu wengine kuamua kufanya mambo wanayoruhusiwa kufanya kulingana na katiba.

Tatizo ni kwamba leo makanjanja ni makanisa yenye < 200 members - solution yasiandikishwe. Wakimaliza hapa kesho kanjanja atakuwa Father Nkwere na kundi lake, Balukta, etc. Keshokutwa ataibuka mwingine na kusema Kajanjas ni NGOs fulani, magazeti fulani, vyombo fulani vya habari, vyama fulani vya siasa, n.k. Sijui mwisho wa ukanjanja utakuwa upi? Ndo maana nikasema kwamba kwa maoni yangu huu ni ushauri wa hatari!

Ila you are right - wengine tunaogopa huyu ni mtu mkubwa - kuna chance (pengine ni finyu) ya serikali kurupuka kuutekeleza bila kuwa na analysis kama ilivyofanya kwenye kuwafuta kodi (baada ya malalamishi yao).
 
kichwa cha habari kipo biased. kwanini usiweke kilichopo Makanisa makanjanja yadhibitiwe – Kilaini ili watu wawe na uhuru wa ku comment?

maanake inaonyesha wazi una chuki binafsi otherwise kuratibu makanisa ni jambo la msingi sana kwani watu hawamwogopi Mungu angalia mfano mdogo wa DECI
 
hIVI MTU MWENYE KANISA AMBALO MAPATO NA MATUMIZI ANAYAJUA MWENYEWE NA MKE WAKE ANAHESABIWA KUWA NI KANISA???????????
 
This Mazee guy, i like him, he reasons out first and gives his comment. Attention People, Jamii Forum is a home of great thinkers, and some of what I see here is exactly the opposite. Think kwanza banaa! Shhhhindwe!
 
Mkuu nadhani una maanisha kinakuwa taaaabu kweli kweli na si inakuwa taaaaabu kwelikweli. Wakulu wataalamu wa lugha mnaweza kuni sahihisha.

Si unajuwa kuwa Nyani haoni desh deshi lake! Chuki zikizidi busara ukimbia zake...
..hata Kiswahili inakuwa taaaaabu kwelikweli

Badala ya kurekebisha ndio kwanza anakandia na kuharibu zaidi.
 
Si unajuwa kuwa Nyani haoni desh deshi lake! Chuki zikizidi busara ukimbia zake...


Badala ya kurekebisha ndio kwanza anakandia na kuharibu zaidi.

Onesha nilipokosea ..haya maneno ya jumlajumla na kuleta falsafa za uongo na kweli hazina nafasi.
 
Mkuu nadhani una maanisha kinakuwa taaaabu kweli kweli na si inakuwa taaaaabu kwelikweli. Wakulu wataalamu wa lugha mnaweza kuni sahihisha.

BTW,

kuni sahihisha sio kiswahili..neno sahihi ni kunisahihisha ...hicho ulichoandika kitakuwa kilugha chako cha kibara huko kwenu.
 
Onesha nilipokosea ..haya maneno ya jumlajumla na kuleta falsafa za uongo na kweli hazina nafasi.
Wewe ndio mwenye kuleta falsafa na ujuwaji mwingi bila ya kuonyesha kilicho kuwa sahihi. ...hazina nafasi. lol!
 
Nafikiri kwamba serikali hijipange kwenye hili makanisa yanaibuka kila kukicha na baadhi ya watu wanayatumia kwamaslai binafsi inauma sana, hivyo wabanwe kwakutumia vibaya makanisa.
 
Wewe ndio mwenye kuleta falsafa na ujuwaji mwingi bila ya kuonyesha kilicho kuwa sahihi. ...hazina nafasi. lol!

Kuonesha kilicho sahihi? Kijana naona kwenye hii post umejitahidi kidogo kuandika kiswahili. Piga moyo konde uje huku kwetu Chakechake tukufunze kiswahili fasaha. lol
 
Kuonesha kilicho sahihi? Kijana naona kwenye hii post umejitahidi kidogo kuandika kiswahili. Piga moyo konde uje huku kwetu Chakechake tukufunze kiswahili fasaha. lol
Ah ah ah ah poor XP... wanakwenda mbio wakiona jina... Maskini kijana mwenyewe hata mononi hajai.

Eeh eh! Lete stori zaidi...! Pemba... Kiswahili! Fasaha! ...Pemba! lol!
 
Last edited:
Ah ah ah ah poor XP... wanakwenda mbio wakiona jina... Maskini kijana mwenyewe hata mononi hajai.

Eeh eh! Lete stori zaidi...! Pemba... Kiwahili! Fasaha! ...Pemba! lol!


????????????????????????????????????/
 
Mpendwa kipimo kipi kitatumiwa na serikali kujua hili kweli kanisa na lipi si kanisa? Je idadi ya watu ndo calibration ya hiyo meter itakayopima hayo makanisa? Nadhani hayo yatakuwa si makanisa kwa maana ya kanisa bali NGOs, CBOs, or any other organizations. Jaribu kukubali ukweli bila kuweka hisia. Huoni kuwa Askofu Kilaini na Gamanywa hapo anatetea uhai wa Kanisa lake kwani serikali kutoa democracy ya kuamini chochote inawapa freedom wakatoliki na wapentekoste kuhama ukatoliki au upentekoste kwenda kwingine? Ndo maana siamini katika dini kabisa maana binadamu wachache wana monopolise dini kwa faida binafsi na kuacha agenda ya Mungu nje yaani Imani. Kama kweli Kilaini anaamini katika roho mtakatifu yeye anashida gani? maana Yesu alisema hataliacha kanisa mpaka ukamilifu wa dahari meaning anauwezo wakulilinda lisifutike sasa hilo lake mbona anataka kulilinda kwa nguvu ya kidunia badala ya kimungu? Kama Mungu yupo pamoja nae nani atakua kinyume nae? Na kama issue ni kodi kwani hata kanisa likiwa na watu milioni thelathini matapeli je hawata kwepa kulipa kodi? Je hata kama hao milioni thelathini ni waaminifu Askofu wao akawa tapeli je hilo kanisa halitakwepa kulipa kodi?

Mosi, kuhusu calibration sijui nini..Sheria za nchi zinatudai minimum vigezo ili kikundi fulani cha watu kikubaliwe kujisajili na kuitwa kama dhehebu au 'kanisa' for that matter. Na kwa jinsi muelekeo wa thread unavyoenda wengi wetu hatupo aware na hivi vigezo na badala yake tunabaki kuwalaumu maaskofu waliotoa mapendekezo yao kuhusu nini kifanyike kuhusu makanisa haya mapya ya mfukoni na ukwepaji kodi. Ninachopenda kuchangia hapa ni kuwa sheria za nchi ni suala moja..na maoni na mapendekezo ya maaskofu ni kitu kingine..tusichanganye hivi vitu viwili. Sheria ni za serikali na kama una matatizo nazo ilalamikie serikali ..

Pili naona unahusisha maonui yako kwamba eti hutaki 'dini', mazee hii sehemu ya kuongelea hilo suala. Huo ni mtazamo wako, na kama unaona unapaswa kuigwa unaweza kufungulia thread yake na kuwaelezea kinagaubaga hiyo concept yako.

Tatu, umeongelea kuhusu Kilaini na Gamanywa kutaka kutetea makanisa yao dhidi ya waumini wao kutaka kutoka na kujitenga. Sioni kama kuna uhusiano hapa. Kama nilivyosema hapo juu, criteria za kuandikisha makanisa zimewekwa na serikali, na suala lililopo mezani kuzuia makanisa ya mfukoni kuutumilia vibaya mwanya wa msamaha wa kodi kujinufaisha binafsi. Ila kwa kuwa wengine wana maono tofauti, mmeona hapa kuwa eti Kilaini na Gamanywa wanataka kuzuia madhehebu mapya kuwaibia waumini wao..lol.

Nne, unasema kuwa eti kama Kilaini anaamini ktk Roho Mtakatifu ana shida gani? Hii kauli yako inashangaza kwa sababu inaonesha so far unajikanganya na hujaelewa mpaka dakika hii kinachojadiliwa kwenye hii thread na wala hujui tatizo tunaloli-address. Nikukumbushe kuwa tatizo tunaloli-address sio tatizo la Kilaini wala Gamanywa ..tatizo ni la kila mTz mwenye uchungu na nchi hii kuona kuwa kuna baadhi ya watu wanatumia vibaya misamaha ya kodi kujinufaisha.. Sasa wewe unayeona imani ya wengine si sahihi ungetusaidia 'kutuombea huko juu' hili tatizo litoweke badla ya kukaa nyuma ya PC na kuzungumza vitu visivyo na tija.
 
Back
Top Bottom