KATIBU Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Pentekoste Tanzania (PCT), Askofu Dk. David Mwasota amesema Mungu amemvisha Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete joho la ufahamu na ujasiri kumuwezesha kupambana vita ya kukisafisha chama hicho na Serikali yake.
Askofu huyo alisema hayo baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kujivua gamba hivi karibuni. Amesema Rais Kikwete na CCM mpya ndio watakaoibuka washindi katika vita hiyo inayoendelea sasa baina yake na wanachama waliopewa siku 90 kujiondoa katika nafasi zote
za uongozi kutokana na kutajwa kuhusika na vitendo vya ufisadi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na HABARILEO Jumamosi mjini Dar es Salaam, Askofu Dk. Mwasota alisema Rais Kikwete atashinda vita hiyo kwa vile maaskofu hivi sasa wanakesha kumuombea kwa Mungu ashinde ili kukirejesha chama hicho kikongwe katika mikono ya wanyonge.
Kama kuna kipindi Rais Kikwete ametufurahisha maaskofu basi ni kipindi hiki. Hatuna sababu ya kupata tafsiri ya nini maana ya kujivua gamba, lakini kitendo alichokifanya hivi karibuni cha kusimamia mabadiliko makubwa ndani ya CCM ili kukiosha chama hicho dhidi ya vitendo vya rushwa na ufisadi ni cha kijasiri.
Kugundua uovu na kupambana nao ni hekima inayotokana na Mungu. Mungu amempa ufahamu na ujasiri wa kuanza kuchukua hatua.
Mwanzo tulikuwa na shaka kama anafahamu mambo yanayoendelea, baadaye tukalaumu kwa kushindwa kuchukua hatua hata pale tume anazounda zinapomweleza hali halisi ilivyo, sasa amechukua hatua nashangaa na nasikitika sana kuona kuna watu wanalaumu na kubeza hatua hiyo tena, alisema.
Askofu Dk. Mwasota alisema maaskofu pia wameridhishwa na ahadi kwamba hatua kama zilizochukuliwa na Rais Kikwete kwenye chama, zitachukuliwa pia kwa viongozi wa serikali wanaotajwa kuhusika na vitendo vya rushwa na ufisadi.
Sasa Rais wetu amevalishwa na Mungu, joho la ufahamu na ujasiri, ingawa vita ni kali, lakini atashinda. Ni kupitia kwa Rais Kikwete ndio nchi itatakasika kutokana na maombi, na Biblia inasema hivyo kwamba Rais wa nchi ndiye atakayeifanya nchi kutakasika au la, kutokana na kutokumbatia dhambi.
Akizungumzia habari iliyoandikwa na gazeti moja la kila siku litolewalo kwa lugha ya Kiswahili
(Si HABARILEO), kwamba alitoa kauli iliyomshutumu, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kuwa anatoa kauli za matusi dhidi ya viongozi wa dini, Askofu Dk. Mwasota alisema habari hiyo ilipotoshwa.
Namfahamu Nape ni mtu mzima, ni mtu msomi na ni mtu makini, najua anachokisema katika mikutano ya hadhara ya CCM kuhusiana na ufisadi ana ushahidi navyo, hakuna matusi aliyoyatoa nakumbuka nilimwambia hivyo mwandishi huyo, lakini nashangaa kilichoandikwa.
Nchi inaweza kuingia katika machafuko kutokana na kuwepo kwa uwezekano wa watu mbalimbali kama wanasiasa, wasanii na vyombo vya habari kuzusha madai yasiyo ya kweli kwa lengo la kukinufaisha kikundi fulani cha watu au chama cha siasa wakati habari hizo zimepotoshwa.
Alisema maaskofu wanao utaratibu wa kutoa kauli zilizofanyiwa utafiti wa kina bila kukurupuka baada ya sekretarieti kuyachuja na kuyafanyia kazi mambo ambayo yanaonekana kutishia uhai wa Taifa na watu wake.
Mimi si msemaji wa Sekretarieti ingawa ni Mratibu. Tunapotamka jambo ujue tuna ushahidi nalo.Tumesali sana na leo kilio chetu kimesikika kwa Mwenyezi Mungu kumvisha Rais wetu, joho la ufahamu na ujasiri ili kupambana na rushwa na ufisadi, tunafurahi sana kwa hatua hii, alisema.
Katika matamshi yake ya hivi karibuni, Nape ameeleza kuwepo kwa njama zinazopangwa na wanaCCM wanaoshutumiwa kuhusika na ufisadi, za kutaka kumchafua Rais Kikwete na familia yake.
Nape alisema ili kufikisha uzushi huo kwa wananchi, watuhumiwa wa ufisadi watawatumia
viongozi wa dini, wanasiasa, wasanii na vyombo vya habari, lakini akawataka wananchi kupuuza uzushi huo na kusema CCM itapambana kwa nguvu zake zote ili kuhakikisha njama hizo hazifanikiwi.
Tangu kufanyika kwa mabadiliko ya uongozi ndani ya CCM ulioshuhudia Sekretarieti yote, chini ya Yusuf Makamba kujiuzulu, huku baadhi ya wanachama wenye madoa ya kisiasa wakionywa kujisafisha wenyewe au kujiondoa katika chama, kumekuwa na mitazamo tofauti, hasa kutoka kwa baadhi ya watuhumiwa ambao kwa sasa wanadaiwa kutafuta njia za kujinasua. SOURCE HABARI L|EO, 23/04/2011
WATZ TUMPE MOYO NA KUMUONGEZEA UJASIRI JK AWASHINDE MAGAMBA. CDM KWA HILI MUONGE MKONO KWA FAIDA YA TANZANIA
Askofu huyo alisema hayo baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kujivua gamba hivi karibuni. Amesema Rais Kikwete na CCM mpya ndio watakaoibuka washindi katika vita hiyo inayoendelea sasa baina yake na wanachama waliopewa siku 90 kujiondoa katika nafasi zote
za uongozi kutokana na kutajwa kuhusika na vitendo vya ufisadi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na HABARILEO Jumamosi mjini Dar es Salaam, Askofu Dk. Mwasota alisema Rais Kikwete atashinda vita hiyo kwa vile maaskofu hivi sasa wanakesha kumuombea kwa Mungu ashinde ili kukirejesha chama hicho kikongwe katika mikono ya wanyonge.
Kama kuna kipindi Rais Kikwete ametufurahisha maaskofu basi ni kipindi hiki. Hatuna sababu ya kupata tafsiri ya nini maana ya kujivua gamba, lakini kitendo alichokifanya hivi karibuni cha kusimamia mabadiliko makubwa ndani ya CCM ili kukiosha chama hicho dhidi ya vitendo vya rushwa na ufisadi ni cha kijasiri.
Kugundua uovu na kupambana nao ni hekima inayotokana na Mungu. Mungu amempa ufahamu na ujasiri wa kuanza kuchukua hatua.
Mwanzo tulikuwa na shaka kama anafahamu mambo yanayoendelea, baadaye tukalaumu kwa kushindwa kuchukua hatua hata pale tume anazounda zinapomweleza hali halisi ilivyo, sasa amechukua hatua nashangaa na nasikitika sana kuona kuna watu wanalaumu na kubeza hatua hiyo tena, alisema.
Askofu Dk. Mwasota alisema maaskofu pia wameridhishwa na ahadi kwamba hatua kama zilizochukuliwa na Rais Kikwete kwenye chama, zitachukuliwa pia kwa viongozi wa serikali wanaotajwa kuhusika na vitendo vya rushwa na ufisadi.
Sasa Rais wetu amevalishwa na Mungu, joho la ufahamu na ujasiri, ingawa vita ni kali, lakini atashinda. Ni kupitia kwa Rais Kikwete ndio nchi itatakasika kutokana na maombi, na Biblia inasema hivyo kwamba Rais wa nchi ndiye atakayeifanya nchi kutakasika au la, kutokana na kutokumbatia dhambi.
Akizungumzia habari iliyoandikwa na gazeti moja la kila siku litolewalo kwa lugha ya Kiswahili
(Si HABARILEO), kwamba alitoa kauli iliyomshutumu, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kuwa anatoa kauli za matusi dhidi ya viongozi wa dini, Askofu Dk. Mwasota alisema habari hiyo ilipotoshwa.
Namfahamu Nape ni mtu mzima, ni mtu msomi na ni mtu makini, najua anachokisema katika mikutano ya hadhara ya CCM kuhusiana na ufisadi ana ushahidi navyo, hakuna matusi aliyoyatoa nakumbuka nilimwambia hivyo mwandishi huyo, lakini nashangaa kilichoandikwa.
Nchi inaweza kuingia katika machafuko kutokana na kuwepo kwa uwezekano wa watu mbalimbali kama wanasiasa, wasanii na vyombo vya habari kuzusha madai yasiyo ya kweli kwa lengo la kukinufaisha kikundi fulani cha watu au chama cha siasa wakati habari hizo zimepotoshwa.
Alisema maaskofu wanao utaratibu wa kutoa kauli zilizofanyiwa utafiti wa kina bila kukurupuka baada ya sekretarieti kuyachuja na kuyafanyia kazi mambo ambayo yanaonekana kutishia uhai wa Taifa na watu wake.
Mimi si msemaji wa Sekretarieti ingawa ni Mratibu. Tunapotamka jambo ujue tuna ushahidi nalo.Tumesali sana na leo kilio chetu kimesikika kwa Mwenyezi Mungu kumvisha Rais wetu, joho la ufahamu na ujasiri ili kupambana na rushwa na ufisadi, tunafurahi sana kwa hatua hii, alisema.
Katika matamshi yake ya hivi karibuni, Nape ameeleza kuwepo kwa njama zinazopangwa na wanaCCM wanaoshutumiwa kuhusika na ufisadi, za kutaka kumchafua Rais Kikwete na familia yake.
Nape alisema ili kufikisha uzushi huo kwa wananchi, watuhumiwa wa ufisadi watawatumia
viongozi wa dini, wanasiasa, wasanii na vyombo vya habari, lakini akawataka wananchi kupuuza uzushi huo na kusema CCM itapambana kwa nguvu zake zote ili kuhakikisha njama hizo hazifanikiwi.
Tangu kufanyika kwa mabadiliko ya uongozi ndani ya CCM ulioshuhudia Sekretarieti yote, chini ya Yusuf Makamba kujiuzulu, huku baadhi ya wanachama wenye madoa ya kisiasa wakionywa kujisafisha wenyewe au kujiondoa katika chama, kumekuwa na mitazamo tofauti, hasa kutoka kwa baadhi ya watuhumiwa ambao kwa sasa wanadaiwa kutafuta njia za kujinasua. SOURCE HABARI L|EO, 23/04/2011
WATZ TUMPE MOYO NA KUMUONGEZEA UJASIRI JK AWASHINDE MAGAMBA. CDM KWA HILI MUONGE MKONO KWA FAIDA YA TANZANIA