Elections 2010 Askofu Gamanywa kuongea na waandishi wa habari kesho

Rwechu

Member
Mar 17, 2009
85
20
Leo nilikuwa nasikiliza Redio wapo 98.0FM, Gamanywa ametangaza kuongea na waandishi wa habari hapo keso kuhusu mambo ya uchaguzi mkuu, kwa maana ya kuingizwa udini kwenye uchaguzi wa mwaka huu.

Nimjuavyo Gamanywa ni rafiki sana wa KIKWETE, siku chache kabla ya kampeni kuanza alikuwa mgeni rasmi kanisani kwake mbezi sijui alikuwa anafungua nini, kwenye maelezo yake kikwete alijinadi jinsi alivyowasaidia kwenye mgogoro wa uwanja wa kanisa hilo mpaka wakaumiliki, may be aliwalipia, vilevile Gawanywa ni mteule wa Rais Kikwete kwenye tume ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI.

Je Askofu huyu anaweza kweli kuongea akiwa huru bila kuegemea CCM ili kulinda kibarua chake na kulipa fadhila kwa kusaidiwa ile ishu ya uwanja? Maana alishaanza kuponda dhana ya baadhi ya Wachungaji wenzake kutangaza kufanya ibada jumamosi ili kupisha siku ya jumapili watu wawe huru kupiga kura.

Je tutegemee la maana hapo keszho? Karibu mchangie wana jamvi
 
Askofu gamanwya anapaswa amuogope Mwenyezi Mungu na kumtamkia JK kweli siyo Chaguo la Mungu
 
hawezi kupingana na mabadiliko yanayoletwa na Mungu!!!!
Nguvu ya mabadiliko ni kubwa sana,hakuna wa kuyazuia.
 
Tusubiri tuone kama nae ni nabii wa uongo kama walivyo wengine
 
Habari nzuri ila una bias ya wazi!

Ningependa kukumbusha kuwa mapenzi yetu yasitunyime uwezo wa kuona ukweli na tusipende chongo tukaita kengeza.

Katika hali ya kawaida ni kwa nini uanze kihivyo na kuwaandaa watu kukataa kile atakachokiongea ambacho hata hujakijua! Uchaguzi utakwisha na niwajuavyo watanzania wengi watakinai haraka kama ... wanavokinai haraka wenza wao siku chache baada ya ndoa!

Narudia, tujitahidi kutazama vitu hasa ambvyo vinaweza kutugawa kama taifa kwa jicho kali zaidi!
 
Hebu tusubiri tuone anachotaka kuongea" akiwasaliti watanzania tutajua tu. Kuliko aongee jambo tofauti na vuguvugu tunaloliona sasa ni heri anyamaze awahubirie tu waumini wake na siyo watanzania kupitia vyombo vya habari"
 
Gamanywa needs to tread with great care during a news conference, especially as a man of god, we expect him to stick to the truth, and not side with those who are perpetrating evils against innocent people.people are now tired of being cheated.it is time for a liberation of the people and not otherwise.
 
Gamanywa needs to tread with great care during a news conference, especially as a man of god, we expect him to stick to the truth, and not side with those who are perpetrating evils against innocent people.people are now tired of being cheated.it is time for a liberation of the people and not otherwise.

sio wote wamwitao bwana! bwana wataingia ufalme wa mbingu
 
Gamanywa ni Askofu anaejiheshimu na anaeheshimika . jamii imekua ikimpa hadhi amabayo hata maaskofu wengine wa Kilokole wamekua hawaipati.
kumtetea Kikwete inahitaji KUWA NA ROHO nGUMU, KUWA tAYARI KUCHAFUKA , MAANA KIKWETE HAKUMBATIWI, HAGUSIKI.
KAMA anataka kujiweka rehani , kwa hadhi na heshima yake , anapaswakuachana na agenda za kuitetea ccm, ingawa ni marafiki.
 
GAMANYWA
spaceball.gif
 
hapo tutapata picha kama anakuja kisiasa kama mwanajamii yeyote? ama anakuja kama mzalendo kwa nchi? ama anakuja kama kiongozi wa Dini? ama anakuja yeye kama Gamanywa na askofu....tusubiri tuangalie atakuja na akiwa mevaa kofia gani kati ya hizo
 
Mtume Mwingira bado naye? Mwaka huu kuna mengi yatatokea, tena bado wiki ijayo ndo kuna vibwagizo jiandae JF kusherehekea ushindi.
 
Ninavo hisi ni mwana ccm,tusubiri tuone asijesema "kaoteshwa jk chaguo la Mungu"
 
Back
Top Bottom