30th January 2011
Rais Jakaya Kikwete
Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelist Assembly of God, (EAGT), Mosses Kulola, amewataka Watanzania nchini kumwombea Rais Jakaya Kikwete na kuacha kuwasilikiza wanaosema hafai kuongoza kwa sababu ni wahaini wa neno la Mungu.
Aliyasema hayo wakati wa kukabidhi nyumba 15 kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu zilizojengwa na Shirika la Kimataifa la Compassion nchini, (CIT), wilayani Kongwa.
"Muwekeni mbele Rais Kikwete msikubali kuyumba pale na kusema aah sisi hatufai huyu msimsikilize huyo mtu ni haini wa neno la Mungu,"alisema.
Alisema Wakristo wanapaswa kumtii Mungu kwa kumpenda Rais Kikwete anayewajali watu maskini.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Lembris Kipuyo, alisema maofisa wa serikali wanapaswa kwenda kuangalia nyumba hizo kwa kuwa zimezingatia thamani halisi ya fedha.
"Nilikuwa namshangaa Mungu sana kazi ilivyofanyika, kazi hiyo ilifanyika vizuri sana, nyumba zimejengwa kwa kiwango cha ubora wa hali ya juu kwa kuzingatia value for money (thamani ya fedha),"alisema.
Mkurugenzi wa CIT, Joseph Mayala, alisema shirika hilo limekuwa likisaidia watoto 65,000 walioko katika mazingira magumu kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Dodoma , Singida, Morogoro, Mwanza, Tabora, Shinyanga, Mara na Iringa.
Alifafanua kuwa mbali ya shirika hilo kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu, pia limekuwa likisaidia wanawake wajawazito.
Nyumba hizo zilibomolewa na mafuriko yaliyotokea kati ya Desemba 24 mwaka juzi na Januari mwaka jana, zimegharimu sh. milioni 75.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Rais Jakaya Kikwete
Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelist Assembly of God, (EAGT), Mosses Kulola, amewataka Watanzania nchini kumwombea Rais Jakaya Kikwete na kuacha kuwasilikiza wanaosema hafai kuongoza kwa sababu ni wahaini wa neno la Mungu.
Aliyasema hayo wakati wa kukabidhi nyumba 15 kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu zilizojengwa na Shirika la Kimataifa la Compassion nchini, (CIT), wilayani Kongwa.
"Muwekeni mbele Rais Kikwete msikubali kuyumba pale na kusema aah sisi hatufai huyu msimsikilize huyo mtu ni haini wa neno la Mungu,"alisema.
Alisema Wakristo wanapaswa kumtii Mungu kwa kumpenda Rais Kikwete anayewajali watu maskini.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Lembris Kipuyo, alisema maofisa wa serikali wanapaswa kwenda kuangalia nyumba hizo kwa kuwa zimezingatia thamani halisi ya fedha.
"Nilikuwa namshangaa Mungu sana kazi ilivyofanyika, kazi hiyo ilifanyika vizuri sana, nyumba zimejengwa kwa kiwango cha ubora wa hali ya juu kwa kuzingatia value for money (thamani ya fedha),"alisema.
Mkurugenzi wa CIT, Joseph Mayala, alisema shirika hilo limekuwa likisaidia watoto 65,000 walioko katika mazingira magumu kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Dodoma , Singida, Morogoro, Mwanza, Tabora, Shinyanga, Mara na Iringa.
Alifafanua kuwa mbali ya shirika hilo kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu, pia limekuwa likisaidia wanawake wajawazito.
Nyumba hizo zilibomolewa na mafuriko yaliyotokea kati ya Desemba 24 mwaka juzi na Januari mwaka jana, zimegharimu sh. milioni 75.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI