Askofu Anthony Mayalla is no more

Kutoka mwanakijiji.com

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Mwanza Mhashamu Antony Mayalla amefariki duniani. Hadi tunaingia mitamboni hatujajua bado chanzo cha kifo chake. Askofu Mayalla alizaliwa tarehe 23 Aprili, 1940 huko Mwabagole, Kwimba mkoani Mwanza. Baada ya masomo ya msingi na Sekondari na baadaye Useminari alipewa daraja takatifu la Upadrisho tarehe 20 Disemba mwaka 1970.

Aliteuliwa kuwa Askofu wa Musoma mwaka 1979 (miaka tisa tu baada ya upadrisho) na kuwa miongoni mwa maaskofu vijana wa Kanisa Katoliki akiwa na miaka 39 tu. Alisimikwa kuwa Askofu wa Jimbo la Musoma tarehe 22 Aprili, 1979 na Muadhama Kardinali Laurean Rugambwa akishirikiana na Maaskofu James Rubin M.Mafr. na Askofu Renatus Butibubage aliyekuwa Askofu wa Mwanza wa wakati huo. Kufuatia kujiuzulu kwa Askofu Butibubage mwaka 1987, Baba Mtakatifu Yohanne Paulo wa Pili alimteua Askofu Mayalla wa Musoma kuliongoza Jimbo Kuu la Mwanza kama Askofu wake Mkuu Novemba mwaka huo. Alisimikwa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Mwanza 28 Februari, 1988 na hivyo kuanza utawala wa Utume wake wa kiaskofu.
Baada ya kusimikwa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo hilo Askofu Mayalla alisimamia kwa kiasi kikubwa uhamishaji wa Makao Makuu ya Askofu kutoka Bugando kwenda kilima kingine cha Kawekamo maili chache toka Uwanja wa ndege wa Mwanza.
askofu Mayalla ameweza kusimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kichungaji jimboni mwake huku akiongoza kwa kupata waseminari na mapadre wapya, kufungua seminari ya kwanza ya Wasichana Jimboni na vile vile kuendelea kufungua vituo vya afya, shule za sekondari na programu mbalimbali za Afya. Jimbo la Mwanza chini ya Askofu Mayalla limendelea kutoa mojawapo ya mafunzo ambayo kwa muda mrefu yalikuwa yanatolewa Mwanza tu nayo ni yale ya Clinical Pastoral Education ambayo yalikuwa yanahusisha watu wa dini mbalimbali kujifunza jinsi ya kuhudumia wagonjwa.



Wengi watamkumbuka katika maadhimisho ya Misa ya Papa Yohanne Paulo wa 2 kwenye viwanja vya Kawekamo Mwanza na pia katika misa ya kumuaga marehemu Baba wa Taifa huko Butiama ambayo yeye aliiongoza.



Mipango ya mazishi itajulikana baadaye.

Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi, Amina

Thank you man. Angalau Mwanakijiji ana vi detail detail kwenye taarifa zake sometimes, unapata ka biography ka marehemu kujua what kinda man we are dealing with here. Poleni wafiwa, wakatoliki na Watanzania sote.
 
Asante Lunyungu kwa post hii. Masanilo alishatoka na breaking news yake dakika 42 kabla ya post yako. Nashauri umuombe mod aiunganishe ili tuendelee na eulogy moja for this great man
RIP Bishop Mayalla.


Mayala is our hero kanda ya Ziwa
Fika Parokia za Komuge, Zanaki, Mugumu,Tarime ,Sirari , Mwisenge , Fika kule Nyamiongo, Makoko Seminary , Kiagata , utajua kwamba Mayala alitumia muda wake kuwatumia Watanzania na kuleta maendeleo
 
Unafiki gani aliokufanyia? Weka wazi watu tujue.
RIP askofu Mayalla, utakumbukwa daima hapa chuoni bugando.

Mkuu Yo Yo ana agenda zake za siri au hajui analolisema au anasema tu ili kukuza wachangiaji

RIP Mayalla
 
Yo Yo kweli watu wamefiwa wewe unawabeza! Great thinkers ni watu wenye mitazamo ya ndani zaidi ya hisia. Humfahamu huyu marehemu, huelekei hata kuwafahamu hao maaskofu, au kwa lugha nyingine huna ushahidi wa huo unafiki, sidhani kama utakuwa nao (evidence ni jinsi unavyoandika). Kwa nini kama inakukera wenzio kumkumbuka mtu wao wanaomheshimu usiende kwenye thread nyingine. Hivi MOD hawezi akawazuia watu kama hawa humu ndani?
 
Inna lillah wa inna ilayhi rajiun
We All Belong to God and To Him We Shall Return.’

Poleni wafiwa na wakatoliki wote kwa ujumla!

 
sina la kusema maana huyu baba askofu kanisaidia sana, wakati niko pale sengerema seminari.pumzika baba

naomba chanzo cha kifo chake jamani
 
Jamani wenzetu wakatoliki wa jimbo la Mwanza poleni sana kwa msiba huu.
Mungu awatie nguvu katika wakati huu mgumu.
 
From Cananews:

Archbishop Anthony Mayala of the Archdiocese of Mwanza, Tanzania is dead.

According to the Very Rev. Fr. Pius Rutechura, the Secretary General for the Association of member Episcopal Conferences of Eastern Africa (AMECEA), Archbishop Mayala passed away on August 19, 2009 as he was undergoing treatment at Bugando Hospital, Mwanza where he had been rushed in the morning after experiencing some health complications.

“Actually, these news are coming too fast, for as early as yesterday, the archbishop spent the day in his office and was healthy,” said Fr. Rutechura.

The Secretary General could not immediately confirm the cause of the death, though he said the late bishop was suffering from hypertension.

The late former board member of the Catholic University of Eastern Africa was born in 1940, ordained Bishop of Musoma diocese, Tanzania in 1979, and later ordained the Archbishop of Mwanza in 1987, an archdiocese he was shepherding till his demise.

Fr. Rutechura, who, as the Secretary General of the Tanzania Episcopal Conference, worked with the deceased for six years described the late archbishop as ‘fatherly, caring, and strong believer of unity and togetherness’.

The burial plans are yet to be made.

Upumzike kwa amani Askofu Mayala
 
Hizi ni habari za kusikitisha sana hasa sisi ambaye tulikuwa nae karibu na ametulea vizuri sana kipindi chote tulichokuwa pale Seminary ya Nyegezi,kwa habari nilizopata toka kwenye source iliyokuwa karibu ni kwamba Mhashamu Baba Askofu alikumbwa na low pressure na alifikishiwa ICU pale hospitali ya rufaa ya Bugando majira ya mchana ambapo mauti yalimkumba.R.I.P....Amen
 
R.I.P Baba Mayala nitakukumbuka kwa ushauri wako ulionipa pindi nipo pale Makoko Seminary baba. Machozi yangu yatafutwa na Mungu. Enzi za uhamisho wa Baberi baada ya Seminary yetu Makoko kufungwa ulinisaidia kwa mengi sana.
 
Last edited:
ASKOFU mkuu wa jimbo kuu la Mwanza, kanisa Katoliki Mhashamu Anthony Petro Mayalla (69) amefariki dunia leo mchana kutokana na maradhi ya moyo baada ya kuugua ghafla akiwa ofisini kwake.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mkurungenzi wa mawasiliano wa baraza la Maaskofu (TEC) kanisa katoliki, Padri Revocatus.Makonge Askofu huyo amefariki baada ya madaktari wa Hospitali ya rufaa ya Bugando kuhangaika kumpatia matibabu bila ya mafanikio.

Alisema kuwa marehemu aliamuka salama leo na kuendelea na shughuli zake za kila siku ofisini kwake mpaka majira ya saa 4:00 asubuhi ambapo alizidiwa ghafla na kukimbizwa Hospitali ya rufaa ya Bugando.Habari kutoka katika ofisi ya aksofu huyo, zimeeleza kuwa alipatwa na maradhi hayo wakati akiwa katika maandalizi ya ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Vatican ambaye alikuwa akitarajiwa kufanya ziara jimboni kwake Oktoba 5 mwaka huu kwa ajili ya kufungua ujenzi wa hospitali ya watoto.“Baada ya kufikisha hospitalini hapo madaktari waliahangaika kuokoa maisha yake lakini nahati mbaya lifariki dunia majira ya saa 8;30 mchana,” alieleza Padri Revocatus Makonge.

Askofu Mayalla alizaliwa Aprili 23 mwaka 1940 katika katika kijiji cha Nera wilayani Kwimba na kupata elimu yake ya msingi katika wilaya hiyo na masomo ya sekondari.Askofu Mayalla alikuwa amehitimu shahada ya kwanza ya elimu aliyopita katika chuo kikuu cha Loyola huko Chicago Marekani mwaka 1973 hadi mwaka 1975.
Imetolewa na mwandishi wa habari hapa Mwanza.
 
We thank the Lord for the life of this good servant of His. He has run the good race, he has completed the journey. Now he has gone to the house of the Father. Our prayers accompany him there.
 
Masanha jambo hili mni zito lakini Mayala alikuja kunipa kipaimara ( Confirmation) na akasema atapenda kuniona niko Seminary , baada ya Ibada aliniombea baraka na kunishika kimwani na kweli nikatinga Seminary .Huyu mzee alikuwa mwelewa alipenda wasomi.Jimbo la Mwanza nina imani lina ongoza sana kwa kuwa na mapadre wasomi maana alifika kote Duniani kuulizia kama anaweza kusomesha mapadre huko.Kazi za injili ujenzi wa zahanati , mashule na misaada hakika the man worked hard .Again apumzike kwa amani .

Kwa hiyo wewe ni Baba Padre?

RIP Bishop Antony Mayala
 
Back
Top Bottom