Elections 2010 Askofu amshangaa Mbunge Lema kutotambua mwafaka

Kishongo

JF-Expert Member
May 4, 2010
932
64
Askofu wa Kanisa la Blessing Alter lililopo mkoani Arusha, Isaya Sizya, amesema anashangazwa na hatua ya Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kukataa mwafaka uliofikiwa hivi karibuni na kuondoa chuki na hofu miongoni mwa wakazi wa Arusha.

Pia askofu alimtaka Mbunge huyo kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa uchaguzi ambazo alidai kuwalaghai wananchi kuzitekeleza ndani ya miezi sita.
Alisema Lema alipokuwa kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kwa wananchi kujenga kituo kikuu cha mabasi Ngulelo na Kisongo, jengo la Machinga Complex, hospitali kubwa tatu, mfumo wa majitaka na barabara.

Alisema tangu alipoingia madarakani hajawahi kuitisha mkutano na wananchi na kuwaeleza ahadi ngapi amezitekeleza badala yake amekuwa akiendesha siasa za majitaka ambazo hazilengi kuleta maendeleo badala yake zinaleta chuki kwa madiwani na wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Askofu Sizya alisema viongozi wa dini walikuwa wakifunga na kusali juu ya amani mkoani hapa na kusisitiza kuwa viongozi hao hawataki kuona damu ya wanaArusha ikirudia kumwagika tena.

Askofu Sizzya alisema Lema anapaswa kuacha siasa za vurugu na vitisho kwa madai ya kutotambua mwafaka wa kumtambua Meya, Gaudence Lyimo na Naibu Meya Estomi Mallah.

Alisema kupinga mwafaka ni kuendeleza unazi wa kisiasa ambao hauna maana hivyo Lema anapaswa kuheshimu makubaliano ya mwafaka ya viongozi wengine yaliyofuata taratibu zote na moja ya sifa ya kiongoi bora ni kuheshimu watu na viongozi wengine.

Source: IPP MEDIA
 
Mbona hasemi kwa nn anamshangaa! Huyu askofu kama haelezi kinagaubaga kwa nini anamshangaa Lema nitamshangaa zaidi yeye. Mwafaka wa 'magumashi' wa kazi gani kwa Lema na wapenda maendeleo na demokrasia ya kweli?
 
haya makanisa ya voda fasta uaskofu unapatikanaje, maana mtu anaweza akaamka akajiita askofu, tusifedheheshe tittle ya uaskofu.
 
Huyu mchungaji namfahamu aliandaa tamasha mziki Wa Injili kuchangia yatima kuna mama mmoja wa UN alimsaidia hela akala alikuwa na kesi ya kula hela huyo njaa inamsumbua tu.QUOTE=Kishongo;2217491]Askofu wa Kanisa la Blessing Alter lililopo mkoani Arusha, Isaya Sizya, amesema anashangazwa na hatua ya Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kukataa mwafaka uliofikiwa hivi karibuni na kuondoa chuki na hofu miongoni mwa wakazi wa Arusha. Pia askofu alimtaka Mbunge huyo kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa uchaguzi ambazo alidai kuwalaghai wananchi kuzitekeleza ndani ya miezi sita.Alisema Lema alipokuwa kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kwa wananchi kujenga kituo kikuu cha mabasi Ngulelo na Kisongo, jengo la Machinga Complex, hospitali kubwa tatu, mfumo wa majitaka na barabara. Alisema tangu alipoingia madarakani hajawahi kuitisha mkutano na wananchi na kuwaeleza ahadi ngapi amezitekeleza badala yake amekuwa akiendesha siasa za majitaka ambazo hazilengi kuleta maendeleo badala yake zinaleta chuki kwa madiwani na wananchi.Akizungumza na waandishi wa habari jana, Askofu Sizya alisema viongozi wa dini walikuwa wakifunga na kusali juu ya amani mkoani hapa na kusisitiza kuwa viongozi hao hawataki kuona damu ya wanaArusha ikirudia kumwagika tena. Askofu Sizzya alisema Lema anapaswa kuacha siasa za vurugu na vitisho kwa madai ya kutotambua mwafaka wa kumtambua Meya, Gaudence Lyimo na Naibu Meya Estomi Mallah. Alisema kupinga mwafaka ni kuendeleza unazi wa kisiasa ambao hauna maana hivyo Lema anapaswa kuheshimu makubaliano ya mwafaka ya viongozi wengine yaliyofuata taratibu zote na moja ya sifa ya kiongoi bora ni kuheshimu watu na viongozi wengine.Source: IPP MEDIA[/QUOTE]
 
Askofu wa Kanisa la Blessing Alter lililopo mkoani Arusha, Isaya Sizya, amesema anashangazwa...

huyu ni kilaza sana anatumia siasa kujitanua....namashaka kama huyu mchungaji anajua wajibu wake kanisa lenyewe lipo arusha tena uchochoroni yeye mwenyewe ndo askofu na mchungaji alijichagua mwenyewe.....apeleke matatizo yake afanye mkakati aongeze waumini wachana na siasa.....
 
Mpaka viongozi wa dini wanawashangaa CDM, Baba Askofu endelea kuhubiri Amani ili nchi yetu isingie kwenye vita
 
Askofu wa Kanisa la Blessing Alter

kishongo@ work.
ndugu mmiliki wa "bold" unaabudu mungu wa wapi? muafaka haukubaliki.. tunchokitaka ni haki ifuatwe na tuone "sauti ya wengi sauti ya mungu" na mamlaka iliyowekwa na mungu na yenye baraka zote
 
Mpaka viongozi wa dini wanawashangaa CDM, Baba Askofu endelea kuhubiri Amani ili nchi yetu isingie kwenye vita
Unanikumbusha mbali sana mkuu!mwaka 2005 viongozi wa dini ya kikristu waliposema JK ni chaguo la mungu waislamu na wana CCM walifurahi sana na ilipofika 2010 waliposema JK hafai wakaitwa wadini!!kichekesho!na wewe unarudia yale yale maaskofu wanakuwa wazuri tu pale wanapoikosoa CHADEMA,wakiisifu mnawaita wadini!!kichekesho kingine!
 
Askofu wa Kanisa la Blessing Alter lililopo mkoani Arusha, Isaya Sizya, amesema anashangazwa na hatua ya Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kukataa mwafaka uliofikiwa hivi karibuni na kuondoa chuki na hofu miongoni mwa wakazi wa Arusha.

Pia askofu alimtaka Mbunge huyo kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa uchaguzi ambazo alidai kuwalaghai wananchi kuzitekeleza ndani ya miezi sita.
Alisema Lema alipokuwa kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kwa wananchi kujenga kituo kikuu cha mabasi Ngulelo na Kisongo, jengo la Machinga Complex, hospitali kubwa tatu, mfumo wa majitaka na barabara.

Alisema tangu alipoingia madarakani hajawahi kuitisha mkutano na wananchi na kuwaeleza ahadi ngapi amezitekeleza badala yake amekuwa akiendesha siasa za majitaka ambazo hazilengi kuleta maendeleo badala yake zinaleta chuki kwa madiwani na wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Askofu Sizya alisema viongozi wa dini walikuwa wakifunga na kusali juu ya amani mkoani hapa na kusisitiza kuwa viongozi hao hawataki kuona damu ya wanaArusha ikirudia kumwagika tena.

Askofu Sizzya alisema Lema anapaswa kuacha siasa za vurugu na vitisho kwa madai ya kutotambua mwafaka wa kumtambua Meya, Gaudence Lyimo na Naibu Meya Estomi Mallah.

Alisema kupinga mwafaka ni kuendeleza unazi wa kisiasa ambao hauna maana hivyo Lema anapaswa kuheshimu makubaliano ya mwafaka ya viongozi wengine yaliyofuata taratibu zote na moja ya sifa ya kiongoi bora ni kuheshimu watu na viongozi wengine.

Source: IPP MEDIA

watu wa dini kutaneni mweke vigezo vya mtu kuitwa askofu maana mtu akiamka anaanza kujiita askofu tayari anajua magazeti yatamwandika
 
Askofu wa Kanisa la Blessing Alter lililopo mkoani Arusha, Isaya Sizya, amesema anashangazwa na hatua ya Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kukataa mwafaka uliofikiwa hivi karibuni na kuondoa chuki na hofu miongoni mwa wakazi wa Arusha.

Pia askofu alimtaka Mbunge huyo kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa uchaguzi ambazo alidai kuwalaghai wananchi kuzitekeleza ndani ya miezi sita.
Alisema Lema alipokuwa kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kwa wananchi kujenga kituo kikuu cha mabasi Ngulelo na Kisongo, jengo la Machinga Complex, hospitali kubwa tatu, mfumo wa majitaka na barabara.

Alisema tangu alipoingia madarakani hajawahi kuitisha mkutano na wananchi na kuwaeleza ahadi ngapi amezitekeleza badala yake amekuwa akiendesha siasa za majitaka ambazo hazilengi kuleta maendeleo badala yake zinaleta chuki kwa madiwani na wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Askofu Sizya alisema viongozi wa dini walikuwa wakifunga na kusali juu ya amani mkoani hapa na kusisitiza kuwa viongozi hao hawataki kuona damu ya wanaArusha ikirudia kumwagika tena.

Askofu Sizzya alisema Lema anapaswa kuacha siasa za vurugu na vitisho kwa madai ya kutotambua mwafaka wa kumtambua Meya, Gaudence Lyimo na Naibu Meya Estomi Mallah.

Alisema kupinga mwafaka ni kuendeleza unazi wa kisiasa ambao hauna maana hivyo Lema anapaswa kuheshimu makubaliano ya mwafaka ya viongozi wengine yaliyofuata taratibu zote na moja ya sifa ya kiongoi bora ni kuheshimu watu na viongozi wengine.

Source: IPP MEDIA

Wana Arusha kweli waliingia mkenge kwa Lema, kumbe aliwapa ahadi zote hizo ? kwa kweli hana uwezo hata wakutekeleza 1%, jamaa itabidi aililie serikali ili imtekelezee hayo anayo yataka, la sivyo imekula kwake na kwa wana arusha
 
Unanikumbusha mbali sana mkuu!mwaka 2005 viongozi wa dini ya kikristu waliposema JK ni chaguo la mungu waislamu na wana CCM walifurahi sana na ilipofika 2010 waliposema JK hafai wakaitwa wadini!!kichekesho!na wewe unarudia yale yale maaskofu wanakuwa wazuri tu pale wanapoikosoa CHADEMA,wakiisifu mnawaita wadini!!kichekesho kingine!
Wakiristo mkachukia?
 
huyu askofu hili ni tamko la pili anatoa la kwanza alilipwa na Chatanda akawakemea maaskofu wa arusha kwa kupinga muafaka leo kapewa fedha na madiwani wa cdm naibu meya mala na katibu wa madiwani wa cdm kujaribu kuzuia hukumu yao inayosubiriwa isiwe ngumu
Mungu atakuathibu kwa kutumia madhabau yake kuganga njaa badala ya kueneza injili
 
Huyu Askofu sasa anataka watu tumkosee Mungu bure. Watu wetu wameuawa kwa risasi, wengine vilema, huku madiwani wanagawana vyeo then Askofu Isaya anasema eti muafaka umepatikana. Watumishi wa Mungu kuweni makini kama kweli mnawachunga kondoo wa Bwana.
 
Ngoja nimchane huyu bishop feki namfahamu vizuri sana isaya aliyeoa mwanamke aliyemzidi umri ambaye alifiwa na wazazi wake akaachiwa mali kidogo ambazo isaya alitumia vibaya na kuwafanya waishi kimasikini zaidi na kuahamia dhehebu la EAGT kama mchungaji na baada ya kuona vurugu zake zimezidi wakamchoka na ndipo akaachia kanisa alilokuwa analichunga la EAGT sanawari kwa kuwaambia washirika kila moja aende anakotaka yeye anavunja kanisa na kuendeleza tabia ya kuomba omba na kuwatapeli watu mbalimbali hapa mjini na hata kukopa na kutolipa madeni yake na hivyo kutafauta wadhili wa kujikingiliza na tabia zake hizo mpaka sasa anajiita askofu kwa kifupi ni mtu wa tamaa sana na huwa hakatai mwaliko wa harusi yoyote anapenda sana kujulikana hana lolote na kama ndiyo askofu wa kishongo hata sishangai maana nadhani akili zao zinafanana
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom