Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Askari wa JWTZ auawa kwa ujambazi | Send to a friend |
Sunday, 11 December 2011 21:03 |
0digg Burhani Yakub, Korogwe. ASKARI wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) wa Lugalo jijini Dar es Salaam ameauawa kwa kuchomwa moto na wananchi wenye hasira baada ya kumakamata akivunja duka la mfanyabiashara wa Kijiji cha Magamba Kwalukonge Wilayani Korogwe. Askari huyo aliyetambuliwa kwa jina la Amoni Kashalankolo (35) mwenye kitambulisho namba MT.83200 alikuwa katika kundi la majambazi wanne waliovamia duka la mfanyabiashara James Lomwe wakiwa na silaha aina ya SMG yenye risasi saba.Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe ni kuwa tukio hilo lilifanyika juzi saa 3 usiku katika kijiji cha Magamba Kwalukonge Wilayani Korogwe. Watu walioshuhudia tukio hilo walisema, majambazi hao walivamia katika duka la mfanyabiashara huyo na kumtishia kwa silaha huku wakimuamuru awape fedha za mauzo na nyingine zilizopo ambapo waliweza kupewa. Walisema wakati wa purukushani hiyo, familia ya mfanyabiashara huyo ilipiga kelele za kuomba msaada ndipo wananchi walipozingira nyumba yenye duka hilo ambapo mwanajeshi huyo alifyatua risasi iliyompiga kwenye paja mmoja wa wanakijiji waliokwenda kusaidia. Katika purukushani hizo mjambazi wengine walifanikiwa kukimbia lakini wananchi waliweza kumkamata mwanajeshi huyo na kuanza kumuadhibu kwa kumpiga na baadaye wakamfunga tairi la gari shingoni na kumchoma moto, alisema Massawe wakati akithibitisha habari hizi. Kamanda huyo alisema baada ya kupewa taarifa askari walikwenda kijijini Magamba Kwalukonge ndipo wakaanza kufanya msako wa kuwanasa majambazi waliokimbia.Alisema katika msako huo askari wakishirikiana na wananchi waliingia katika msitu wa karibu na kijiji hicho wakakuta pikipiki moja, nguo maalumu za kufunika nyuso pamoja na sare za jeshi la JWTZ. Tupo katika msako mkali wa kufuatilia nyendo za majambazi waliotoroka baada ya kufanya tukuio hilo na tunapenda kuwahakikishia wananchi kuwa tutawanasa wakati wowote, alisema Massaw |