Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Chadema nao wana haki ya kushitaki kama wanaona wametukanwa kwani hiyo haiondoi kosa la mgombea wa chadema kumtukana wa CCM. Two wrongs don't make one right, kwa kiswahili kibovu....Makosa mawili hayafanyi kuwa kosa moja lililo sahihi. Tuhukumu kila kosa kwa hoja zake. Usije kwenda mahakamani/kizimbani ukamwambia hakimu kwamba, mheshimiwa hakimu niliamua kumwibia ng'ombe bwana X aliyenishitaki baada ya hapo awali yeye kuniibia mbuzi wawili.
Mie nawashangaa sana hawa CCM, jana Mrisho J.K kawadharau wanamageuzi hajafanywa chochote, Hadija Kopa nae kamkashifu Dr. Slaa lakini Selemani Kova hajasema chochote.
Kila siku Yusuph Makamba anatoa kauli za hovyo kabisa na manager wa kampeni Abdulhaman Kinana hakemei kabisa yeye analalamika tu CCM wanaposemwa.
Mie nafikiri mkuu wa jeshi la polisi ndugu Said Mwema anatakiwa awe makini sana na mambo haya.
Katika suala la matusi mimi si shabiki hata siku moja, kwa yeyote alimsikia yule mgombea wa chadema live pale mwembeyanga yale ni matusi na anaweza kukiharibia chama chake kukosa kura za watanzania wapiga kura za mlengo wa upande wa ustaarabu. John Mnyika na Anna Maulida Komu wanasitahili pongezi kwa kumiliki jukwaa vizuri na kuushawishi uuma kwamba hawako kwenye siasa kwa ajili ya matusi bali kujenga hoja zenye mantiki ya kuvuta hisia ya mpiga kura.Tutakuwa tunafanya makosa makubwa kwa mustakabari wa taifa letu tukifikiri kwamba siasa ni matusi, na hii si kwa sababu alimtukana Kikwete mgombea wa CCM bali hata angaekuwa ni mgombea wa chama chochote...TLP, NCCR, CUF n.k
Kusema kikwete hakufunzwa na mama yake mzazi wakati mama wa mgombea huyo alishakufa ni suala lisilokubarika na linaweza kukumbusha kifo cha mama ya mtu si uungwana
Mimi binafsi sitashangaa sana kama huyu bwana atafunguliwa mashitaka.
katika suala la matusi mimi si shabiki hata siku moja, kwa yeyote alimsikia yule mgombea wa chadema live pale mwembeyanga yale ni matusi na anaweza kukiharibia chama chake kukosa kura za watanzania wapiga kura za mlengo wa upande wa ustaarabu. John mnyika na anna maulida komu wanasitahili pongezi kwa kumiliki jukwaa vizuri na kuushawishi uuma kwamba hawako kwenye siasa kwa ajili ya matusi bali kujenga hoja zenye mantiki ya kuvuta hisia ya mpiga kura.tutakuwa tunafanya makosa makubwa kwa mustakabari wa taifa letu tukifikiri kwamba siasa ni matusi, na hii si kwa sababu alimtukana kikwete mgombea wa ccm bali hata angaekuwa ni mgombea wa chama chochote...tlp, nccr, cuf n.k
kusema kikwete hakufunzwa na mama yake mzazi wakati mama wa mgombea huyo alishakufa ni suala lisilokubarika na linaweza kukumbusha kifo cha mama ya mtu si uungwana
mimi binafsi sitashangaa sana kama huyu bwana atafunguliwa mashitaka.