Asilimia 30 ya bajeti inaliwa na watumishi wasio waaminifu-J.K. Kikwete

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
UMOJA wa Ulaya (EU) umeipatia serikali ya Tanzania kiasi cha euro milioni 383 (sawa na sh bilioni 750) huku ikiionya juu ya ufisadi na utendaji mbovu unaozorotesha sekta ya miundombinu.
Kwa mwenendo huo, EU inataka yawepo mageuzi ya kweli na yanayoonekana, mijadala kwenye mambo magumu yanayohitaji kushughulikiwa pamoja na ahadi ya kuiweka Tanzania kwenye mstari wa mwendokasi.
Akisaini makubaliano ya kutoa kiasi hicho mbele ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, Balozi wa EU nchini, Tim Clarke alisema wengi wakiwemo wabia wa maendeleo watashangazwa na hatua hiyo, kwani kwa sasa habari zilizopo Tanzania ni rushwa na upotevu wa fedha za umma.
“Ndiyo, watu wengi wabia wa maendeleo wa Tanzania navyama vya kijamii wanaweza kuuliza mantiki ya kutoa misaada hii kipindi ambacho vyombo vya habari vimejaa habari za kashfa za rushwa na ufisadi na upotevu mkubwa wa fedha za umma,” alisema balozi huyo.
Kwa mujibu wa Clarke, wabia wa maendeleo na serikali wamekwishafanya mapitio ya mwaka na kugundua si mazuri (moderate satisfactory) huku mageuzi katika sekta ya umma yakiwa na hali mbaya.
Clarke alionyesha kushangazwa na utendaji wa hali ya chini wa bandari na reli, miundombinu ambayo ingeweza kuifanya Tanzania na Afrika Mashariki kuonekana kuwa kinara wa maendeleo ya biashara na uchumi, lakini badala yake hali katika maeneo hayo inasikitisha.
Balozi huyo alisema uendeshaji wa sekta hizo nyeti umebaki kuwa wa mazoea huku maslahi ya baadhi ya watu, urasimu na kukosa ubunifu ni mambo ambayo yamekuwa yamechangia kutofikiwa kwa malengo.
Kutokana na matatizo hayo ya utekelezaji aliyoyaainisha, Clarke aliieleza waziwazi kuwa EU haitaruhusu malipo kupitia kwenye hazina bila ya kuhakikishiwa fedha zinazotolewa zitatumika ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha walimu na watumishi wa afya vijijini wanapata fedha zao bila kupunjwa.
“Baada ya kusema hivyo, sisi pia tuna matatizo katika utawala, vita dhidi ya ufisadi, haki za binadamu, ujenzi wa demokrasia ya uwajibikaji na uwazi. Sisi pia hatuwezi na hatutaweza kufumbia macho haya,” alisisitiza.
Alieleza fedha zilizotolewa na EU licha ya mambo yote hayo ni ubia wa umoja huo na Tanzania ambao si wa fedha tu bali uanzishaji wa misingi ya kuaminiana kati ya serikali na wabia wengine na kutambua mchango wake kwa kutoa hifadhi kwa wakimbizi pamoja na ukombozi wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Alidokeza kuwa makubaliano ya kusaini kiasi hicho cha fedha yanakuja huku Ulaya ikibadilika, hasa baada ya kupitishwa kwa Mkataba wa Lisbon na haijulikani kitakachotokea.
Naye Waziri Mkulo baada ya kusaini mkataba huo, ambao umeifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi saba pekee kupewa fedha hizo, alisema kiasi hicho kitatoa mwongozo kwa EU katika kuisaidia Tanzania katika kupambana na umasikini katika mpango huo wa kuisaidia bajeti.
“Nimeelezwa ya kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi saba za Kiafrika katika mpango huu wa kipekee wa misaada,” alisema Mkulo.
Akieleza baadhi ya maeneo fedha hizo zitakapoelekezwa, Mkulo alisema euro milioni tano zitapelekwa Kituo cha Takwimu cha Taifa (NBS) wakati euro milioni mbili zitapelekwa katika kitengo cha sukari.
Alikiri kuwa nchi inakabiliwa na tatizo la miundombinu kiasi cha kutoweza kumudu changamoto za ukuaji wa uchumi.
Kwa mujibu wa taarifa ya EU juu ya fedha hizo, lengo lake ni kusaidia Tanzania kutimiza malengo ya milenia.
Hata hivyo, wahisani wamechangia fedha hizo licha ya kuwepo kwa tuhuma nyingi za ufisadi, huku Rais Jakaya Kikwete wakati akizindua jengo la Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU) akisema zaidi ya asilimia 30 ya bajeti inaliwa na watumishi wasio waaminifu.
Kiasi hicho kinakaribia asilimia 36 ya bajeti ambayo wahisani wanachangia, jambo lililowafanya wanasiasa kuuchachamalia utawala wa awamu hii kupambana na ufisadi.


h.sep3.gif
source.tanzania daima
 
Wana JF,

[quote=Mzee Mwanakijiji;700151]..... I have now become a suspicious of the motives of the so called "development partners". I think they are the one who have become in fact the enablers of corruption in the country. They have been for so many years now filling the gap created by corruption by providing grants and aids.

I believe if the donor community were to halt, freeze or in a certain ways restrict their foreign aid the Tanzanian people would finally feel the pain of corruption and they will ultimately link their welfare to the government in power.

It is for this reason, I believe these few coming weeks and early weeks of 2010 and as a matter of fact the whole coming year will witness record breaking foreign aid pouring into Tanzania to act as political anesthetics of corruption.......


It is a well known fact (at least I demonstrated it in my second part of "understanding a corrupt political system) that one of the beneficiaries of a corrupt culture is the foreign investor then it is only natural for foreign government to poor more aid into the country in order to act as local anesthetics. Others however, would poor more aid to act as general anesthetics on our people.....[/quote]

Ni 14th Dec 2009 juzi hapa mwanakijiji alisema hayo hapo juu, sasa wanakuja na style mpya ya kututawala, hawa ni watu wakututakia mema sindio hao hao watakao tuuzia siraha sikutukikorofishana humu nchi??
 
"Clarke aliieleza waziwazi kuwa EU haitaruhusu malipo kupitia kwenye hazina bila ya kuhakikishiwa fedha zinazotolewa zitatumika ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha walimu na watumishi wa afya vijijini wanapata fedha zao bila kupunjwa."
hili litawezekana kweli..kwanza mpaka sasa hivi wenye BOT washaanza kugawana mikopo
 
Mi sijui ila kunasiku bubu ataongea,nchi sasa hivi wahindi ndo wanaotawala kila kitu wanaamua wao kodi wanakwepa kwa kwenda mbele watz na wazugu wachache ndo tunaokamuliwa kodi,angalia kamshahara ndo hao lkn kodi yake
 
Wana JF,

[quote=Mzee Mwanakijiji;700151]..... I have now become a suspicious of the motives of the so called "development partners". I think they are the one who have become in fact the enablers of corruption in the country. They have been for so many years now filling the gap created by corruption by providing grants and aids.

I believe if the donor community were to halt, freeze or in a certain ways restrict their foreign aid the Tanzanian people would finally feel the pain of corruption and they will ultimately link their welfare to the government in power.

It is for this reason, I believe these few coming weeks and early weeks of 2010 and as a matter of fact the whole coming year will witness record breaking foreign aid pouring into Tanzania to act as political anesthetics of corruption.......

It is a well known fact (at least I demonstrated it in my second part of "understanding a corrupt political system) that one of the beneficiaries of a corrupt culture is the foreign investor then it is only natural for foreign government to poor more aid into the country in order to act as local anesthetics. Others however, would poor more aid to act as general anesthetics on our people.....

Ni 14th Dec 2009 juzi hapa mwanakijiji alisema hayo hapo juu, sasa wanakuja na style mpya ya kututawala, hawa ni watu wakututakia mema sindio hao hao watakao tuuzia siraha sikutukikorofishana humu nchi??
[/QUOTE]



Mkuu wakifreeze grants and aids watakaoteseka si waliokula hizo pesa bali wananchi wa hali chini kabisa.
 
Ni 14th Dec 2009 juzi hapa mwanakijiji alisema hayo hapo juu, sasa wanakuja na style mpya ya kututawala, hawa ni watu wakututakia mema sindio hao hao watakao tuuzia siraha sikutukikorofishana humu nchi??



Mkuu wakifreeze grants and aids watakaoteseka si waliokula hizo pesa bali wananchi wa hali chini kabisa.[/QUOTE]
ni kweli sasa kinachotakiwa ni wananchi wenyewe kubadilika jambo ambalo bado ni gumu sana
 
Jakaya Kikwete wakati akizindua jengo la Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU) akisema zaidi ya asilimia 30 ya bajeti inaliwa na watumishi wasio waaminifu.
Kiasi hicho kinakaribia asilimia 36 ya bajeti ambayo wahisani wanachangia, jambo lililowafanya wanasiasa kuuchachamalia utawala wa awamu hii kupambana na ufisadi.


h.sep3.gif
source.tanzania daima[/QUOTE]

Yeye Kikwete amejiweka katika kundi gani ? watu wengine bwana !!!
 
Hata hivyo, wahisani wamechangia fedha hizo licha ya kuwepo kwa tuhuma nyingi za ufisadi, huku Rais Jakaya Kikwete wakati akizindua jengo la Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU) akisema zaidi ya asilimia 30 ya bajeti inaliwa na watumishi wasio waaminifu.


h.sep3.gif
source.tanzania daima
SASA Rais anamlalamikia nani, kwani ni nini wajibu wake, sisi atuambie kati ya walioiba amekamata wangapi huko ndiko kulinda raslimali za taifa na sio kulalamika, sasa mimi raia wakawaida nifanye nini kama mtawala mwenye nguvu mikononi mwake analalamika, Kikwete bwana kama wamekushinda hao wezi wa mali za UMMA achia ngazi usituzingue.
 
jk kibogoyo..........................anajua kinachofanyika lakini hawezi kuchukua hatua..............
 
Mi sijui ila kunasiku bubu ataongea,nchi sasa hivi wahindi ndo wanaotawala kila kitu wanaamua wao kodi wanakwepa kwa kwenda mbele watz na wazugu wachache ndo tunaokamuliwa kodi,angalia kamshahara ndo hao lkn kodi yake
yani na sisi tunajifanya tunaendesha nchi wakati wahindi ndio wenye nchi?
ona wanavyo jidai mitaani.............wanatemea watu mate wakiwa juu kwenye maghorofa..................wanawapiga watu vibao na wala hawachuliwi hatua yoyote........................nenda mitaa yote maarufu ya biashara ni wahindi tu....wachina tunauza nao tooth sticks
habari ndo hiyo....................nenda india km unaweza hata kupewa kibanda uuze urembo...thubutu
 
Back
Top Bottom