Mbeya= Ibheya..wenyeji walienda kutafuta ama kununua chumvi.
TUKUYU = kulikuwa na miti midogo mitatu aina ya Mikuyu, ambapo wenyeji waliweka bidhaa zao kwa biashara walipaita Patukujhu.
KYELA= ikyela (chuma)
SUMBAWANGA =tupa uchawi..
 
Hivi umepata kujiuliza unapopita katika mitaa mbalimbali ya mjini Dar au mji mwingine wowote Tanzania, jina la mtaa au eneo husika limetokana na nini?

Kwa mfano, Kijito Nyama limetokana na nini? Au Mlalakuwa, Au Mtoni kwa Aziz Ali n.k, n.k. Labda utadhani imetokea tu ... just ipo ipo, hapana! Baadhi ya majina ya mitaa yana historia ndefu na yenye kukumbukwa hata kwa vizazi vijavyo.

Hapa napenda kuwahabarisha maana ya mtaa au eneo la nje kidogo ya jiji la Dar liitwalo Gongo la Mboto.Jina hili limetokana na nini? Nakumbuka nilipata kusimuliwa na mwalimu wangu mmoja miaka ile pale Tambaza Sekondari nikiwa kidato cha pili.

Alisema palikuwa na mzee mmoja mashuhuri ambaye alipata kuishi katika eneo hilo.Huyu jamaa alikuwa mkulima. Jina lake aliitwa Mboto. Siku moja alijilawa kwenda katika konde lake kwa ajili ya kujipatia riziki.

Wakati ule, maeneo yale yalikuwa na giza la mapori na vichaka kadhaa. Jioni yake asirudi nyumbani. Kesho yake hadi mchana Mboto haonekani.

Mbiu ikapigwa watu wakakusanyika,kilichofuata ni msako mkali wa kumtafuta mzee huyu.Baada ya siku kadhaa wakakuta nyayo za mnyama mkubwa mithili ya Simba na ishara ya purukushani kadhaa.

Walipochunguza zaidi wakafanikiwa kukuta Gongo ambalo alipenda kutembea nalo mzee huyu.Wakahisi kuwa Mboto huenda amekutwa na maafa ya kuliwa na Simba. Walichokiona pale ni Gongo lake,Ndipo hilo eneo hadi leo lajulikana kama Gongo la Mboto.

Tuhabarishane maana ya maneno mengine kama Msasani, Mikocheni,Mto wa Mbu n.k.
Keep in zero (waswahili kiponzelo)

Long tree ( waswahili lilongoti )
 
Kiboriloni...keep rolling
Arusha... rarusa(kimaasai) mzungu akashindwa kutamka
Mzumbe...ensumbe mzungu alishindwa kutamka..hii inahistoria kidogo mpaka naona uvivu kuandika.
Olduvai...Oldupai
Cairo....gailo kimaasai(sina uhakika)
Ha haaaaa
 
Kiboriloni...keep rolling
Arusha... rarusa(kimaasai) mzungu akashindwa kutamka
Mzumbe...ensumbe mzungu alishindwa kutamka..hii inahistoria kidogo mpaka naona uvivu kuandika.
Olduvai...Oldupai
Cairo....gailo kimaasai(sina uhakika)
umenikumbusha home kbs KB nimepamis mno
 
Si ya nyaga maana yake kisukuma nchi ya upepo wazungu wakashindwa kutamka wakasema shinyanga
 
Pangani: Mwaka 1873 Sultani wa Zanzibar alipotiliana sahihi na Serikali ya Uingereza mkataba wa kusimamisha biashara ya utumwa, eneo la Pangani ya sasa ilitumika kama soko la magendo la utumwa kwa kupitia Kisiwa cha Pemba ilikukwepa manowari za Kiiingereza. Hivyo wakati watumwa wanapangwa kwa kuuzwa waliamriwa "jipangeni" Tunaambiwa hiyo ndiyo asili ya Pangani.
Pangani linatokana na lugha ya kizigua, "wapangani hano" yaani wapangeni hapa( watumwa)
 
Jina la karasha ni kila sehemu palipokuwa pamejengwa mashine za kusaga mawe, ipo kilwa eneo la nangurukuru, hoteli Tatu kwenda Lindi, barabara ya tunduma eneo la mpemba, njia panda kwenda hospitali ya misheni mbozi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom