Hi JF members
Leo asubuhi kupitia BBC Mkapa Rais wa awamu ya 3 wa JMT amezungumza yafuatayo;
Wengi hawajui katiba mpya inaandikwaje wanafikiri tunachukua plane paper tunaanza kuandika kila kitu Nooo hatufanyi hivyi isipo kuwa marekebisho makubwa yanafanyika nchi nyingi zinafanya hivyo
Tulipo anzisha mfumo wa vyama vingi tulitegemea kuona vyama vipya vinakuja na mfumo,sera tofauti na CCM lakini sasa vyama vingi vina mfumo na muundo sawa na CCM.
Wengi wanafiri katiba mpya ikianza kutumika tu basi upinzani utashina Nooo si rahisi kuishinda CCM
Wengi wanalalamika kuwa tume ya Uchaguzi si huru ukiwauliza si huru kivipi hawasemi wanashindwa kueleza
Alikuwa akijibu maswali ya mtangazaji wa BBC. Mazungumzo haya yataendelea wiki ijayo ikiwa ni sehemu ya maadhamisho ya miaka 50 ya UHURU wa Tanganyika
Nawasilisha